Ufafanuzi kuhusu tetesi za kufungwa kwa benki zaidi nchini Tanzania

Mkuu naona hilo gamba John gauteng umelitandika za uso bila huruma. Asante sana.
 

Mkuu, hebu tufafanulie kidogo kuhusu NPL Ratio.

Inaashiria nini ikiwa ndogo au kubwa?
 
Naomba nikujibu mkuu kama ifuatavyo Bank perfomance hupimwa kwa Vigezo vingi sana ni zaidi ya vitano hivi, Pia kuna vigezo vingine vingi sana

Analysis zote zinapatikana kwenye statement za Bank husika wengi hawazielewi kwa kuwa zimewekwa kwa mfumo wa ratios zinapatikana chini kabisa kwenye statement kila robo mwaka hutolewa statement hizo
BoT wao kama msimamizi wana vigezo au Bench mark zao kuwa kiwango katika uwiano kiwe vipi? Nao BoT hufanya analysis zao Independent wanaweza fanya Onsite supervision au offsite supervision inategemea wao wenyewe uamuzi wao

Sasa tujadili vigezo vinatumiwa:

Liquidity measure ,Uwezo wa Bank kuwa na sufficient fund ambayo nirahisi kuipeleka katika fedha hapa tunaongelea raslimali zote ambazo Bank kwa muda mfupi ikiamua kuuza au kununua wanaweza kuwalipa wateja wao mara moja, BoT wana Bench mark yao pia

Capital adquacy, Hichi ndicho kilichosababisha Bank hizi kufungwa zile tano, Hicho ni kiwango ambacho Benk inatakiwa kuwa nacho kama mtaji huko Benk kuu, nacho BoT wana bench mark yao

Muda hautoshi wengine endelezeni kujadili hapa.

Hapo kwenye Mikopo mfu yaani Non performing loans, Hii inaaangaliwa kwa kila mkopo unaotolewa na Benk ni mingapi haitalipika, BOT huzilazimisha Bank na kuna percent ya kukokotoa hizo ni Finacial standard kabisa, ndio maana kuna kipindi CRDB walifanya makadirio makubwa kuwa mikopo haitalipika ikaonekana wamepata hasara

Mkopo unaitwa mfu usiolipika ni baada ya mteja kushindwa kufanya marejesho kwa miezi kadhaa zaidi ya siku 90 hivi

Ingawa baada ya muda huo kuna wateja wanaweza endelea kurudisha, Non performing loans ni makadirio tu wala sio kigezo cha Bank kuwa hovyo

Hivyo muda hautoshi ningejibu zaidi naomba wengine muendeleze vigezo vingine bye
 
Sijaona baadhi ya benki hapo kama bank of china,bank of india,na kuna ile benki ya marekani iko karibu na holiday inn au zile hazihesabiwi kama benki?
Zipo ila hazina mikopo mibaya
Tafuta list angalia namba 1-5
 
Mkuu, hebu tufafanulie kidogo kuhusu NPL Ratio.

Inaashiria nini ikiwa ndogo au kubwa?
Mkuu hii ni mikopo ambayo benki inadai wateja wake na hakuna dalili zozote za kulipwa.

A non performing loan (NPL) refers to a classification for loans on the books of financial institutions that are in default or are in arrears on scheduled payments of principal or interest. In most cases, debt is classified as nonperforming when loan payments have not been made for a period of 90 days.
 

Serikali ilitakiwa isizifilisi hizi Community Banks,ila wangezifutia Certificates ya kuwa bank na kuwa Financial instutions tu.

Hizi Bank zilikuwa ni msaada mkubwa kwa mkulima na ni zao la vitunguu na mahindi yao
 
Hii ni sawa na kua una milioni 10 mfukoni na umekopesha watu laki 5 na wamegoma kulipa afu mtu anasema umefulia na watu wawe na tahadhari na ww kwakua tu watu wamegoma kulipa io laki 5....kabla hujaangalia non perfoming loans za bank km CRDB angalia net profit waliopost last yr & divent zake kwa wanahisa uone ya kwamba hio non perfoming loans hazifikii faida zinazopata hizo bank kuzifanya tuzitilie shaka...
 
South africa ni nchi tajiri lakini BANK zake hazizidi 10 kwanini tanzania iwe hivyo?
Nikusahihishe...
South Africa ina zaidi ya benki 70. Za ndani na za nje.


Google uone. Nimeshindwa kukuwekea link hapa
 
S
Hapa kwetu biashara nyingi ni za kuigana, ukiona jirani ananufaika kwa kuuza nyanya basi nawe kesho asubuhi unajenga kichanja cha kuuzia nyanya
South Africa wana benk zaidi ya 70
 
Swala na non preforming loans ni tete sana kwa banks.Ila niseme jambo moja,banks zenyewe zinahusika na hali hii.Hivi bank zinajua kwamba utoaji mikopo imekuwa biashara inayolipa sana kwa wafanyakazi wa bank?Hivi bank zinajua kwamba rushwa imekithiri kwenye utoaji wa mikopo?Hivi bank zinajua kwamba watu wasiokidhi vigezo wanapewa mikopo bora watoa rushwa na wafanyakazi wa kitengo cha mikopo wasio waaminifu?Bank ziamke,rushwa imekithiri kwenye utoaji wa mikopo,and unless this is arrested quickly,bank nyingi zitafunga milango because of non performing loans.Something very unusual is going on in the banking sector.
 
benki lazima zijipange vizuri na kuangalia upya jinsi ya kutengeneza faida kwa mikopo kwa uhakika! wamekuwa watu wa kuwatishia watu kuwa watauza nyumba wasipomaliza mikopo matokeo yake mkopaji anaboronga akijua atakachopoteza ni nyumba.
wanaangalia kwa uchache sana mazingira ya biashara ya mtu ikiwemo jinsi ya mwitaji anavyoweza kusimamia biashara yake hii ni ndio imetufikisha hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…