Mechi ya Mbeya City na Yanga ilichabangwa Jumapili (juzi). Matokeo yalikuwa 1-1. Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Nani anapata nini? Ipo wazi kuwa kama Mbeya City wangesawazisha goli kipindi wakiwa na mchezaji wa ziada uwanjani, kisha refa asingeona, lakini akaripoti kwa mamlaka ya mashindano, ingewezekana City kunyang'anywa pointi yao moja waliyopata kisha Yanga kupewa pointi zote tatu.
Goli lilifungwa kabla ya mgogoro husika. Uamuzi ulikuwa kumtoa nje ya uwanja aliyeingia kimakosa na kama ingebidi, ingepigwa adhabu ndogo. Hivyo ndivyo sheria inasema. Kwa hiyo hakuna namna Yanga wanaweza kupewa pointi tatu. Itakuwa ni tukio la kuchekesha kama itaamuliwa hivyo.
Ameandika Luqman MALOTO