mkuu si vyema kutoa conclusion kabla kesi haijaanza, kinachopambaniwa sasa hivi ni hati tu
Ingekuwa bora ungejielekeza kujibu msingi wa malalamiko ya mawakili upande wa utetezi...
Hakuna mtu ametoa conclusion ndugu...
Kama unasikiliza na kufuatilia mjadala huu kwa makini, unaweza kujua mara moja kuwa, kinacholeta shida ktk kesi hii hatua kwa hatua ni Jaji kuonesha dalili zote za kuwa biased akiweka giza kwa haki kuonekana ikitendeka na ndiyo maana washtakiwa wamesema wazi mbele yake kuwa hawana imani naye, dhamiri yake ikamshtaki na akakubali kukaa pembeni...
kesi yenyewe ya msingi bado haijaanza kutolewa ushahidi
Wote tunajua hili...
so kwa namna yeyote ile hata kama jaji angemuachia huru, ni lazima angekamatwa hapo hapo
Unarudi kulekule.
Hii siyo kazi ya hakimu/Jaji, ni kazi ya polisi na mwendesha mashtaka wao. Hata kama watamkamata mtuhumiwa mara 20....!
Kati hatua yoyote, kazi ya hakimu/Jaji ni kuitolea maamuzi hoja yoyote iliyo mbele yake kwa mujibu wa sheria...
Katika hatua hiyo, ishu ilikuwa ni Charge sheet kama inakidhi vigezo vya kisheria au la....
Jaji mwenyewe akafanya ruling kuwa, haina hadhi kisheria na kwa hatua hiyo maana yake, hakuna offence, hakuna mshtakiwa...!
Ni kipi tusichoelewana mpaka hapo...?
kwasababu serikali bado ina interest nae kwenye ile kesi ya msingi
Yes, hakuna abishae. Ifuate sheria na imlete mtuhumiwa tena na tena lakini KWA KUZINGATIA TARATIBU NA SHERIA. Huu ndiyo msisitizo...!!
kukosewa kwa hati ya mashitaka hakumuondolei makosa ndugu yetu
Yes, hakuna anayebisha. Fuata utaratibu na sheria sasa kumpeleka mahakamani na kumshtaki. Ni hilo tu boss. Mbona huelewi...?
kinachofanywa na mawakili wa utetezi ni tactics za kawaida kabisa kisheria, ambazo kiuhalisia zinachelewesha kesi tu na si kuondoa kosa la msingi mtuhumiwa(niko tayari kurekebishwa)
Wewe ndiyo unaelewa hivyo kuwa ni "tactics" za kuchelewesha lakini walio jikoni wanajua nini wafanyacho na maana yake...
Nyakubonga, sikiliza kidogo. From the first place, mawakili wa utetezi na ule wa mashtaka wote wanajua kuwa hii kesi ni ya kutengenezwa na haina uhalisia wowote...
Makosa haya kijinga unayoyaona na kuleta sintofahamu hii ni kwa sababu msingi wake ni UONGO WA KESI...!
Sasa upande wa defense, wanaujua mchezo vizuri zaidi. Wakataka kuumaliza mapema na kujenga hoja hiyo. Na infact hata mawakili wa upande wa mashtaka wanajua kuwa ni ngumu kujenga hoja ktk mashtaka ya uongo na indirectly wanakiri kushindwa...
Tatizo liko kwa mahakama/hakimu anayeshinikizwa kufanya maamuzi nje ya haki na sheria. Hapa ndipo kilipo chanzo cha shida yote hii...!