The fundamental question is: Did the court dismiss the charges? The answer is no; the court just ordered amendment of the charge sheet.
Curable defects shouldn’t result in downright dismissal of such serious charges!
Haya ni maoni yako ya kufikiri toka kichwani tu. Hayana uhusiano na matakwa ya kisheria 100%...
Ukitaka kuwa fair & just ktk kutoa maoni yako juu ya hili, basi ni vyema sana kabla ya yote ukajiuliza na kuwa na majibu sahihi ya maswali haya muhimu;
1. Kesi ya jinai (criminal case) kwa mujibu wa sheria ni nini..?
2. Utaratibu wa kuanzisha mashtaka ya kijinai kama haya yanayomkabili Mbowe na wenzake kisheria ukoje...?
3. Hati ya mashtaka [charge sheet] ni kitu gani? Na kazi yake ni nini? Ni nini umuhimu wake katika shauri zima? Kwanini imepingwa kisheria na hakimu kukubali kuwa kweli haijakidhi matakwa ya kisheria...?
4. Tukishajiuliza maswali hayo na kupata majibu yake, ndipo tunamaliza na kupata jibu la swali hili kuwa, kama mahakama imejiridhisha kuwa charge sheet haina hadhi kisheria, nini kinafuata...?
Ni mawili au manne:
1. Charge sheet ndiyo inatoa description ya kosa/makosa anayohumiwa nayo mtuhumiwa kuyatenda, yaani NINI, WAPI, LINI na KWA NAMNA GANI
Kwa ufupi, charge sheet ndiyo picha nzima ya kesi yote. Na sheria imeelekeza hatua kwa hatua nini yule anayeshtaki afanye...
Kukosea step yoyote ktk kuandaa charge sheet na ikathibitika hivyo kisheria, automatic kunakuwa hakuna shauri mahakamani au shauri zima linakuwa batili....!
2. Katika mchango wako umeuliza: Did the Court dismiss the charge?
Japo umejijibu mwenyewe kwa kusema "NO", lakini jibu sahihi linapaswa kuwa, "YES" kwa sababu bado hakuna kesi mbele ya mahakama kwa mujibu wa sheria..!
RWMEMBER:
Charge sheet ndiyo ina determine kuendelea na hatua inayofuata katika shauri au la; pande mbili zianze kusikilizwa au la. Sasa kama cha kusikilizwa hakipo, mahakama isikilize nini...?
3. Umesema pia, "the Court has just ordered the amendment of the charge sheet"
Yes, imesema hivyo. Na hapa ndipo kosa la hakimu/jaji/mahakama lilipo na ndiyo chanzo cha chaos hii yote hata sisi kujadiliana hapa...
Ni kama vile mahakama na Jaji Luvanda imechagua kuwa upande wa waendesha mashtaka jambo ambalo siyo jukumu lake na hii imeleta picha ya biasness...
Hili hata Jaji Luvanda mwenyewe aliliona na ndiyo maana hakusita kujitoa alipotamkiwa na washtakiwa kuwa hawana imani naye...!
On contrary, alichopaswa kutamka Jaji baada ya kujiridhisha kuwa charge sheet ina makosa ya kisheria, ilikuwa ni kuwaambia upande wa mashtaka kwenda kuandaa charge sheet upya kama wanadhani bado wana nia ya kushtaki...
Na kwa upande wa pili mahakama ilipaswa kutamka straight forward kuwa washtakiwa wako huru...!!
Kwa hili gumu kumeza lakini ndiyo matakwa ya sheria hayo!!
4. Umesema pia, "siyo sahihi kuacha makosa serious kama hili yapite"
Kwanza, kwa hoja hii unathibitisha kuwa unasukumwa na personal emotions kuandika....
Pili, siyo kazi ya mahakama kukaa na mtuhumiwa ambaye hajaletwa mbele yake bado na kuona kuwa ana kesi ya kujibu...!!
Kama Jamhuri wanaona mtu huyo bado anastahili kushtakiwa, basi wafuate utaratibu za kisheria kum - detain na kisha kumfungulia mashtaka upya bila kufanya makosa ya kijinga kama waliyofanya...!!!
Hiki ndicho kinachosemwa na watu wengine kama "anaachiwa na kisha anakamatwa tena"
Hili wala halina shida kama linafanyika kwa mujibu wa sheria...!!
Asante