Ufafanuzi wa Mapigo Kumi ya Wamisri!

Ufafanuzi wa Mapigo Kumi ya Wamisri!

Kutokana na elimu niliyofundishwa mapigo hayo hayakutoka kwa Mungu, Zikikuwa ni chamgamoto za mabadiliko ya hali ya hewa tu
Hata kama uliyosema ni kweli,ila bado mungu mwenyewe ndo alisema atatoa hayo mapigo. ..baada ya kusema hivyo ndo yakatokea hayo yote...
 
Maji ya mto nili yaligeuka tope, sababu ya mvua kubwa iliyonyesha nyanda za juu. Chura si mvumilivu kwenye tope, hasa akitaka kuzaliana.
Nikuchekeshe kidogo? Chawa waliibuka baada ya wamisri kuishi siku nyingi bila kuoga wala kusafisha mavazi yao, baada ya kukosa maji safi.
[emoji23]
 
32.jpg
 
Haya mapigo kumi yana nadharia mbalimbali. Kuna nadhalia moja, ambayo na mimi naiamini sana inasema kama ifuatavyo:
  1. PIGO LA NILE KUWA DAMU: Mto naili hutiririsha maji yake kutoka nyanda za juu za Ethiopia na sudani. Huko unakoanzia kuna nchi yenye udongo mwekundu. Ilitokea mvua kubwe ilinyesha, udongo mwekundu ukasombwa na hatimae mto nile kuwa mwekundu sababu ya udongo. maji ya nili hayakugeuka damu, bali lilikuwa tope jekundu.
  2. PIGO LA VYURA: Baada ya mto nili kujaa tope jekundu, vyura wake (mtoni) walishindwa kuishi katika hali ile na iliwalazimu kutoka nje ya mto, hivyo kulandalanda katika nchi ya misri wakitafuta maji safi kwa ajili ya kuzaliana, ikizingatiwa kipindi cha maji mengi ndipo vyura huzaliana.
  3. PIGO LA NZI: Wale vyura waliokimbia mtoni na kurandaranda nchi kavu waliishia kufa kwa sababu ya kutozoea mazingira. hivyo inzi wakapata ahueni ya kuzaliana kwa sababu ya uchafu uliosababishwa na kufa kwa vyura hao.
  4. MARADHI: Kuenea kwa maiti/mizoga ya vyura, harufu mbaya na kuzagaa kwa mainzi kulisababisha nchi kukumbwa na maradhi ya mlipuko, ukiwemo ugonjwa wa majipu.
  5. NYOKA.: Hawa viumbe walienea nchini wakisaka vyura. vyura walipotoweka mitoni iliwalazimu nyoka kutafuta vyura wengine au chakula kingine popote kilipo.
  6. VIFO; hivi vilitokea sababu ya maradhi kama iliyoainishwa hapo juu, pamoja na kukosekana ka maji safi ya kunywa.
Bible yasema kuwa MAPIGO HAYO HAYAKUWAPATA WANA WA ISRAELI ..... yaliwapata WAMISRI TU .... Je hao vyura, chawa, maji kuwa damu, VIFO VYA WAZALIWA WA KWANZA nk. majanga yote hayo yaliwapata WAMISRI pekee kwa kuwa WANA WA ISRAEL hawakuwamo MISRI? .... Why na wao yasiwapate?
 
Back
Top Bottom