Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 3,978
- 6,739
Habari ya uzima wanaJF ni matumaini yangu kuwa mnaendelea Vyema sana pia niwape Pole wagonjwa. Kama ilivyo Kawaida yangu ya kupitia vyanzo mbalimbali vya kimtandao pamoja na makala kadhaa basi leo Naomba nilete uzi huu maalumu kuhusu Moja kati ya mchezo wa kipekee barani Afrika unaopatikana nchini Afrika ya Kusini.
Kutana na Kabila la Wavenda linalopatikana huko Afrika ya Kusini; ambapo wanaume hukutana uwanjani na kutengeneza mfano wa duara la kiasi tu kisha wapambanaji wawili huingia ndani ya duara hilo mfano wa ulingo. Huku mashabiki waliotengeza duara hilo wakipiga makofi na kuongeza makeke kunongesha mpambano. Mchezo wa Musangwe.
Ni mchezo wa kipekee sana Kwani hufanyika siku Za Jumamosi kwenye kijiji cha Tshifundi. Ni wakati ambao wahusika huwa kwenye mapumziko na hujumuika kuendeleza utamaduni ambao umedumu kwa zaidi ya Miaka 200; yaani mtu achezee vitasa mpaka aombe radhi.
Mchezo wa Musangwe ni mchezo wa kikatili sana Kwani wapambanaji hupigana wakiwa hawana gloves wala kitu chochote hivyo ni mwendo wa makonde tu na vitasa vya kutosha. Ingawa Afrika ya Kusini pamoja na dunia imebadilika lakini Bado kuna sehemu kama Milima ya kaskazini mwa Afrika ya Kusini. Kila wiki watu hukusanyika kwa ajili ya musangwe; ili kuoneshana umwamba.
Sheria za mchezo huu ni rahisi ila hatari; hakuna kuvaa gloves, wala kilinda meno na hakuna kikomo cha muda wa kupigana. Hata kama utazidiwa; unaweza kusimama na kuendelea kupambana. Kitu kikubwa ni mmoja wao kunyoosha mikono kusurrender. Hakuna mambo ya kamari. Ukiachilia mbali majeraha; wapambanaji hutoka wakiwa na heshima na sifa kwa watazamaji.
Tshilidzi Ndevana almaarufu kama Sumu ndo bingwa mkali kwa sasa. Ana Miaka 56 Mwalimu wa shule na baba wa watoto watano. Na Bwana Tshilidzi aliingia kwenye mchezo huu akiwa na Miaka kumi tu.
Kukitokea kutokuelewana baina ya watu basi suluhu ni kwenda kwenye mpambano huu; ambapo uchukuliwa kama kuondoa kinyongo baina ya watu.
Naomba nimalizie Hapo kwa leo mpaka Wakati Mwingine tena wanaJF.
Shukrani sana kwa kuchukua muda wako kusoma uzi huu.
Kutana na Kabila la Wavenda linalopatikana huko Afrika ya Kusini; ambapo wanaume hukutana uwanjani na kutengeneza mfano wa duara la kiasi tu kisha wapambanaji wawili huingia ndani ya duara hilo mfano wa ulingo. Huku mashabiki waliotengeza duara hilo wakipiga makofi na kuongeza makeke kunongesha mpambano. Mchezo wa Musangwe.
Ni mchezo wa kipekee sana Kwani hufanyika siku Za Jumamosi kwenye kijiji cha Tshifundi. Ni wakati ambao wahusika huwa kwenye mapumziko na hujumuika kuendeleza utamaduni ambao umedumu kwa zaidi ya Miaka 200; yaani mtu achezee vitasa mpaka aombe radhi.
Mchezo wa Musangwe ni mchezo wa kikatili sana Kwani wapambanaji hupigana wakiwa hawana gloves wala kitu chochote hivyo ni mwendo wa makonde tu na vitasa vya kutosha. Ingawa Afrika ya Kusini pamoja na dunia imebadilika lakini Bado kuna sehemu kama Milima ya kaskazini mwa Afrika ya Kusini. Kila wiki watu hukusanyika kwa ajili ya musangwe; ili kuoneshana umwamba.
Sheria za mchezo huu ni rahisi ila hatari; hakuna kuvaa gloves, wala kilinda meno na hakuna kikomo cha muda wa kupigana. Hata kama utazidiwa; unaweza kusimama na kuendelea kupambana. Kitu kikubwa ni mmoja wao kunyoosha mikono kusurrender. Hakuna mambo ya kamari. Ukiachilia mbali majeraha; wapambanaji hutoka wakiwa na heshima na sifa kwa watazamaji.
Tshilidzi Ndevana almaarufu kama Sumu ndo bingwa mkali kwa sasa. Ana Miaka 56 Mwalimu wa shule na baba wa watoto watano. Na Bwana Tshilidzi aliingia kwenye mchezo huu akiwa na Miaka kumi tu.
Kukitokea kutokuelewana baina ya watu basi suluhu ni kwenda kwenye mpambano huu; ambapo uchukuliwa kama kuondoa kinyongo baina ya watu.
Naomba nimalizie Hapo kwa leo mpaka Wakati Mwingine tena wanaJF.
Shukrani sana kwa kuchukua muda wako kusoma uzi huu.