Habari wana JF,
Wataalam wa siasa walipata kusema kuwa ili utawale kundi ama jamii kwa namna unavyotaka wewe ni lazima ufanye mambo makubwa mawili, mosi ikiwa ni kuwafanya watu masikini ili wakunyenyekee na pili ni kuwafanya watu wajinga kwa kuwanyima elimu ili wasikuhoji.
Mbinu hutumika na watawala wenye chembechembe za kidictator na hutumia mwavuli wa democrasia kuwahadaa mataifa na wanaowatawala. Nami kuwa umasikini wa watanzania sio mpango wa Mungu bali ni mpango wa watawala kwani kama ni rasilimali nchi yetu ina rasilimali kila kona na sitazitaja kwani sote tunazifahamu. Licha ya rasilimali zote bado nchi ni masikini kiasi cha kuwa ombaomba.
Ni mwendawazimu pekee ndie atakaekuelewa pale utakapomwambia kuwa Tanzania ni kati ya nchi tatu duniani kwa kutegemea misaada ikiwa pamoja na Somalia ambayo haikuwa na serikali kwa zaidi ya miaka ishirini. Aibu hii yote watawala hawawezi kuikwepa kwani kwa mifano hai tumeshughudia wakiiuza nchi kwa wageni kwa kisingizio cha uwekezaji huwa wazawa wakibaki wanyonge na masikini katika nchi yao.
Tumeshughudia haya katika migodi,ardhi na sasa kwenye gesi. Ni mara nyingi sana wizi wa fedha za umma umefanyika na serikali kukaa kimaa na kuwadaa watanzania kwa maigizo.Nitatoa mfano wa sakata la EPA ambalo lilimuhusu mojamoja gavana wa benki kuu wakati huo Daudi Balali,wakati sakata likiendelea tukasikia kafariki dunia nchini marekani.
Ni nani anayeweza kutupa ushahidi pasipo na shaka juu ya kifo cha balali? kama viongozi wakubwa wa wanaweza kuhudhuria mazishi ya wasanii ni kiongozi gani aliyehudhuria? Kwa kukosa majibu ya maswali haya nakosa woga wa kusema kuna agenda ya siri ili kupoteza ushahidi dhidi ya sakata la EPA. Hii no mifano tu ya namna watanzania tunavyofanywa masikini kwa makusudi. Hapo sikuzingumzia kuuwa viwanda, kuuwa mashirika ya umma, kuuwa kilimo ikiwemo cha mkonge na kahawa na mengine mengi.
Tukija kwenye swala la elimu ndipo ambapo serikali imevurunda kwa makusudi kabisa ili kuendelea kuwahadaa watanzania waendelee kuwatawala.Elimu ya Taifa lolote hubebwa na Falsafa ya taifa hilo pamoja na malengo na matarajio ya taifa hilo.Kwa kuangalia msingi wa elimu ya nchi yetu iliwekwa kwa kuzingatia misingi ya azimio la arusha ambapo lengo la elimu lilikuwa no kuwafanya watu wanahitimu waweze kujitegemea.Hii iliwezekana kwani elimu iliwafanya watu wawe wadadisi, wabunifu, majasiri kwa maana ya watu wanaothubutu, pia iliwafanya watu kuwa wazalendo kwa taifa lao.
Misingi hii ya elimu imekiukwa na watawala kwa makusudi kabisa ndio maana ha mwanafunzi anaesoma shule sasa hajui falsafa wala itikadi ya nchi yake. Ni mwendawazimu pekee ndie atakaeweza kukubaliana na mfumo wa elimu wa nchi hii. Elimu ya nchi yetu imekuwa ikiangalia zaidi idadi ya wanafunzi na madarasa na sio ubora wa elimu inayotolewa. Tumefika mahali mpaka elimu yetu tumeiweka kwenye soko huria kila mtu atoe elimu atakavyo yeye. Utasikia shule hii inatumia mtaala wa kongo, mara malawi tusishangae siku tukasikia shule inatumia mtaa kisukuma ama kichaga.
Ni aibu nchi kuwa haina mitaala ya elimu. Ni aibu sana kusikia wanafunzi wanakaa chini wakati nchi imejaa misitu kila kona.Ni aibu sana mwalimu kuwa ni yule aliyefeli. Shule hazina walimu na wale waliopo wamekata tamaa kutokana na maslahi duni.Shule hazina masbara,vitabu, maktaba nk. Badala ya kutatua matatizo haya inaundwa Tume ya kuchunguza kwanini ufaulu mbovu wa kidato cha nne. Ni mwendawazimu pekee ndiye atakaekuelewa.
Pengine ni makusudi kuuwa elimu ya taifa letu ili wakitangaza ukabila, udini, ukanda na propaganda nyingine za kishenzi dhidi ya vyama vinaelekea kushika dola tuwaelewe. Si muda wote watatudanganya na kutukandamiza.
By Nicholaus Ngowi (mtoto wa seremala)
Wataalam wa siasa walipata kusema kuwa ili utawale kundi ama jamii kwa namna unavyotaka wewe ni lazima ufanye mambo makubwa mawili, mosi ikiwa ni kuwafanya watu masikini ili wakunyenyekee na pili ni kuwafanya watu wajinga kwa kuwanyima elimu ili wasikuhoji.
Mbinu hutumika na watawala wenye chembechembe za kidictator na hutumia mwavuli wa democrasia kuwahadaa mataifa na wanaowatawala. Nami kuwa umasikini wa watanzania sio mpango wa Mungu bali ni mpango wa watawala kwani kama ni rasilimali nchi yetu ina rasilimali kila kona na sitazitaja kwani sote tunazifahamu. Licha ya rasilimali zote bado nchi ni masikini kiasi cha kuwa ombaomba.
Ni mwendawazimu pekee ndie atakaekuelewa pale utakapomwambia kuwa Tanzania ni kati ya nchi tatu duniani kwa kutegemea misaada ikiwa pamoja na Somalia ambayo haikuwa na serikali kwa zaidi ya miaka ishirini. Aibu hii yote watawala hawawezi kuikwepa kwani kwa mifano hai tumeshughudia wakiiuza nchi kwa wageni kwa kisingizio cha uwekezaji huwa wazawa wakibaki wanyonge na masikini katika nchi yao.
Tumeshughudia haya katika migodi,ardhi na sasa kwenye gesi. Ni mara nyingi sana wizi wa fedha za umma umefanyika na serikali kukaa kimaa na kuwadaa watanzania kwa maigizo.Nitatoa mfano wa sakata la EPA ambalo lilimuhusu mojamoja gavana wa benki kuu wakati huo Daudi Balali,wakati sakata likiendelea tukasikia kafariki dunia nchini marekani.
Ni nani anayeweza kutupa ushahidi pasipo na shaka juu ya kifo cha balali? kama viongozi wakubwa wa wanaweza kuhudhuria mazishi ya wasanii ni kiongozi gani aliyehudhuria? Kwa kukosa majibu ya maswali haya nakosa woga wa kusema kuna agenda ya siri ili kupoteza ushahidi dhidi ya sakata la EPA. Hii no mifano tu ya namna watanzania tunavyofanywa masikini kwa makusudi. Hapo sikuzingumzia kuuwa viwanda, kuuwa mashirika ya umma, kuuwa kilimo ikiwemo cha mkonge na kahawa na mengine mengi.
Tukija kwenye swala la elimu ndipo ambapo serikali imevurunda kwa makusudi kabisa ili kuendelea kuwahadaa watanzania waendelee kuwatawala.Elimu ya Taifa lolote hubebwa na Falsafa ya taifa hilo pamoja na malengo na matarajio ya taifa hilo.Kwa kuangalia msingi wa elimu ya nchi yetu iliwekwa kwa kuzingatia misingi ya azimio la arusha ambapo lengo la elimu lilikuwa no kuwafanya watu wanahitimu waweze kujitegemea.Hii iliwezekana kwani elimu iliwafanya watu wawe wadadisi, wabunifu, majasiri kwa maana ya watu wanaothubutu, pia iliwafanya watu kuwa wazalendo kwa taifa lao.
Misingi hii ya elimu imekiukwa na watawala kwa makusudi kabisa ndio maana ha mwanafunzi anaesoma shule sasa hajui falsafa wala itikadi ya nchi yake. Ni mwendawazimu pekee ndie atakaeweza kukubaliana na mfumo wa elimu wa nchi hii. Elimu ya nchi yetu imekuwa ikiangalia zaidi idadi ya wanafunzi na madarasa na sio ubora wa elimu inayotolewa. Tumefika mahali mpaka elimu yetu tumeiweka kwenye soko huria kila mtu atoe elimu atakavyo yeye. Utasikia shule hii inatumia mtaala wa kongo, mara malawi tusishangae siku tukasikia shule inatumia mtaa kisukuma ama kichaga.
Ni aibu nchi kuwa haina mitaala ya elimu. Ni aibu sana kusikia wanafunzi wanakaa chini wakati nchi imejaa misitu kila kona.Ni aibu sana mwalimu kuwa ni yule aliyefeli. Shule hazina walimu na wale waliopo wamekata tamaa kutokana na maslahi duni.Shule hazina masbara,vitabu, maktaba nk. Badala ya kutatua matatizo haya inaundwa Tume ya kuchunguza kwanini ufaulu mbovu wa kidato cha nne. Ni mwendawazimu pekee ndiye atakaekuelewa.
Pengine ni makusudi kuuwa elimu ya taifa letu ili wakitangaza ukabila, udini, ukanda na propaganda nyingine za kishenzi dhidi ya vyama vinaelekea kushika dola tuwaelewe. Si muda wote watatudanganya na kutukandamiza.
By Nicholaus Ngowi (mtoto wa seremala)
