salimkabora
JF-Expert Member
- Nov 10, 2012
- 2,441
- 652
Wana jf hebu tusaidiane ni kwa nini hii nchi makampuni yanapora mali za wanyonge kwa jeuri kubwa na hakuna wa kuwasemesha? Ni hivi, nilkuwa na salio la tshs. 2,943,040 kwenye line yangu ya voda; natumia lain hii kwa miamala ya kibenki,kununua huduma, kuongea na jamaa zangu nje hata masaa matano mfulizo, nk. Lakini ghafla wamekwiba pesa zote hizi na kuniwekea salio la zero zero;ni siku tano sasa tangu jumatano sipigi simu wala kufanya miamala yoyote. Nimewaripotia tangu alhamisi na wanachofanya ni kunitumia mimeseji eti wanachunguza, ni hadi lini? hivi mtu anaingia kwenye akaunt ya mtu kwa jeuri na kuiba masalio na pasiwepo na la kufanya? au hizi ndio pesa wanazofanyia mapromosheni ya uongo na kweli? kampuni gani inaweza kutoa zawadi bilioni moja lakini inaiba salio la milioni mbili? namba yangu ni 0754 843388 na mwenye wazo la kunisaidia tuwasiliane