Ufugaji wa Bata: Aina za bata, ujuzi, gharama, changamoto, faida na masoko

 
1)Hivi nikifuga bata wa kawaida lazima niwatengenezee sehemu ya wao kuchezea maji?maana kuna eneo hapa nyumbani la wao kujiachia kwenye nyasi huku wakizila kama chakula ila sina hakika kama natakiwa niweke pia na bwawa la maji ili wacheze humo
2)Je bata sio waharibifu wa migomba?eneo ambalo ninampango wa kujenga banda lipo karibu na migomba na sitaki kuipoteza(i.e sitakuwa nawafungia kwenye banda muda wote,nitakuwa nawaachia nje,hawataratibu migomba?)
wenye uzoefu tafadhali mnijuze
 
Ni waharibifu wazuri tu, hasa kwa migomba midogo

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mie nahitaji kufuga njiwa, kama una elimu hiyo unaweza nipatia!
 
Wadau kama kuna mtu ana mbinu ya kuzuia na kupambana na wizi wa mifugo mjini tupeane. Hii ni kikwazo kikubwa kwa wafugaji wa mjini pengine kuliko hata magonjwa.
Kwa ushauri wangu mimi kupunguza ama kuzuia wizi wa mifugo
1.Kujenga mabanda imara
2.Kuweka ulinzi kwa mifugo yako
3.Kutumia mfumo wa kufugia ndani na sio mfumo huria unawaruhusu wanyama wako kuzurula hapa na pale
 
Offcoz ni vizuri ukaweka sehemu ya wao kuchezea maji maana bata wanapenda maji maji na pia haina shida kuwafuga kwenye migomba we fuga tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…