Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

misorgenes

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2010
Posts
206
Reaction score
50
Anayejua elimu/ujuzi wa ufugaji wa Nyuki, Mizinga bora,ulinaji asali na soko la asali atupe elimu. Natamani kufanya biashara hii.


===========
 
Habari mkuu,nenda pale LITI- Morogoro wana kitengo cha ushauri utajifunza mengi. Au for practical guide fika maili moja Kibaha mkoani karibu na Polisi kuna msitu wanafuga kisasa.
 
Dah afadhali umeamua kuanza harakati za kijiajiri mapema. Na mimi nataka kujiajiri nitafurahi kupata maelekezo juu ya ufugaji nyuki
 
Nakushauri project yako ianzie Tabora, kule kuna mapori safi kwa ufugaji wa nyuki.

Nakumbuka nilifanya project hii na babu yangu nikiwa primary, sikuipenda sababu lazima ujue kutengeneza nyumba ya nyuki (mzinga)
Kutafuta sehemu nzuri juu ya mti na kuupachika (lazima ujue kukwea miti)

Kilichonifanya nichane na hii project ni ile siku la kurina asali, hatukuwa na protective clothes, tulikoka moto moshi wake ndiyo ulitumika kuwazuia nyuki wasituume, mzee nikabandikwa na nyuki 2 duh, ni mbio home na toka siku hiyo nikaiacha kazi hiyo rasmi.

Jaribu pia kufanya upembuzi wa hili suala la ukusanyaji wa Bee Products yaani NTA na Asali katika mikoa hiyo, inalipa naona MO pia anafanya hizo katika ukanda huo.
 
Nadhani the best way to tackle hii issue ni kuangalia from selling point of view, market.... Je unaweza kununua asali lets say from Tabora ukaipackage vizuri na kuiza nchi za nje au sehemu nyingine.

From my research other people make more money from bees than the bee keepers just like the middle men wanavyotengeneza pesa zaidi kuliko wakulima wenyewe. Kwahiyo soma hiyo link niliyokupa hapo juu kuhusu kufuga nyuki ila kama unataka kama biashara pekee utatengeneza more money kuinunua kwa jumla from tabora (including nta) package vizuri na kuresale kwenye supermarkets, au nchi nyingine

My point being to make profit from eggs you dont need kufuga kuku unless you love and you are ready kufuga kuku na kuna forum ya wafuga nyuki Can you make a living with Bees - Beesource Beekeeping Forums
 
 
Ndio sababu nimesema kwenye post ya 7 unaweza kutengeneza pesa from honey na nta bila kufuga nyuki, unanunua kutoka tabora unapackage vizuri alafu unaiuza sababu huu ufugaji ili ufanye in big way you need good management na je utapata good return on investment kulingana na bei utakayouza (competition) au is it easier ukinunua tabora ambapo supply ni kubwa?

Je demand ni kubwa sana au utatafuta soko nje ya nchi? je kupata soko nje ya nchi ni lazima wewe ufuge au unaweza ukapata from tabora package na ukaaza nje na kubakia na profit nzuri? haya ni baadhi ya maswali ya kujiuliza.
 
voiceofreason: ngoja nifanye tafiti za kina! mana bado nipo kweny steji za kwanza kabisa!
 
Anza na kuuza bee products,then uingie ktk ufugaji,kwani kwa sasa wafugaji ni wengi,ila Distributors ni wachache mno na benefits za nyuki na Asali bado jamii yetu bado haijaitambua ipasavyo
 
 
lets be partners then!

Mkiunganisha nguvu mtafanikiwa haraka, kwa mfano,mwezi jana nilipokuwa kijiji kimoja kinaitwa Chogo huko Iringa,niliona mzinga mmoja unafikia Tsh 8000/ kuutengeneza kisasa pale pale kijijini na wenyewe wanasema una ujazo wa debe moja na nusu. Mavuno ni mara mbili kwa mwaka.
 
Mimi nashauri, kama una maanisha ktk plan zako, anza na shamba lako ili uweze kudhibiti ubora wa asali yako. Mashamba ambayo yanazungukwa na mashamba ya mazao mengine yanayotumia dawa za kilimo ni hatari kwa ubora wa asali yako. Kumbuka nyuki anaweza kwenda umbali wa kilomita 4 toka ulipo mzinga wake, hivyo tafuta shamba zuri lililo karibu na maji safi ya kuaminika na lisiwe karibu na mashamba yanayotumia dawa za kuulia wadudu.

Kutembelea wakulima wakubwa ni muhimu sana kwa ajili ya practical,kabla hujaanza ili wakupe mawili matatu.
 
embu nieleze vizur iyo propolis!

Kazi nyingine ya propolis ni kuvutia nyuki ili waingie ktk mzinga mpya,yaani ukishapata mzinga mpya,nenda shambani kwako, fungua ndani ya mzinga kisha paka ktk kuta za mzinga hiyo propolis yako,funika na uondoke. Usifanyie nyumbani kwako,kwa sababu unaweza ukasahau kupeleka shamba na nyuki wakaingia mchana, watoto wako au wa jirani wakachezea. Balaa lake si dogo.
 
Naamini umepewa mawazo mazuri mengi tu.
Kwa kuongezea, napenda kukukumbusha kuwa ktk modern beekeeping techniques hulazimiki kwenda porini kama unavyoelezwa kuwa utafute sehem zenye misitu mikubwa ila andaa shamba lako kwa kupanda miti ambayo inatoa maua yanayopendwa na nyuki.
Congrats.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…