Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Kwa Watakao hitaji Vifaranga wa Aina mpya ya Kuku ambayo ni imroved Kienyeji KARI wanaweza oda hii ni breed inayo taga mayai mengi kuliko kuku wa kisasda wa mayai
 
Kwa Watakao hitaji Vifaranga wa Aina mpya ya Kuku ambayo ni imroved Kienyeji KARI wanaweza oda hii ni breed inayo taga mayai mengi kuliko kuku wa kisasda wa mayai

Hawa ni wa wapi? Na kwanini unasema wanataga mayai mengi kuliko wa kisasa? Kwani kwa siku wanataga mayai mangapi?
 
Mkuu Suip maximum siku saba ! Isizidi hapo maana yakikaa sana hata kama ikitokea kwa bahati yai likatotolewa kifaranga kinakuwa dhaifu sana kisiweze ku-survive.

Kama kuku anataga mayai 15 yai la kwanza kwa mfano si linakuwa limekaa siku 14. hapo inakuweje Kubota hebu fafanua kidogo
 

Well said Kubota and thanks
 
Wale wanaotaka vifaranga wa kuku wa kienyeji wasio chotara wanaweza kunitafuta. Vifaranga ni kwa oda. Acha ujumbe kwenye 0784222293 wakati wowote ukitaja idadi unayotaka.
 
mkuu uzi wako umenifunza mengi,
am putting haya mafunzo into practice na naona faida, kudos.
lkn na wewe wacha kuharibu mazingira kwa kuchoma choma miti ya mikaa
 
Wataalam Kubota, Liver mwenzangu na wengineo. Nimeanzisha ufugaji wa kuku wa kienyeji baada ya kuhamasika sana na huu mkanda. Nina kuku tetea 10 jogoo 1 hapo ni vp jogoo na mtesa au anatosha kwa kazi yake? Nina kanga 4 nimewachanganya kwenye banda moja na kuku je kuna athari yeyote? Maana athari ninayoona kwa sasa ni kanga kula mayai kila kuku wa kitaga. Je hawa kuku nimewanunua Tanga miezi miwili iliyopita je jina haja ya kuwapa chanjo kwa sasa hivi? Ni hayo tu wataalam wangu naomba msaada kujuzwa. Mengine yatafuata taratibu kutokana na mazingira nitakayokuwa naona.
 
Kama hauna hakika na huko ulipowatoa ni vyema kuwapatia chanjo,ugonjwa wa Newcastle Disease ni hatari unapowakumba kuku utauchukia ufugaji,
 
Kama hauna hakika na huko ulipowatoa ni vyema kuwapatia chanjo,ugonjwa wa Newcastle Disease ni hatari unapowakumba kuku utauchukia ufugaji,

Asante sana kwa ushauri . Leo nimeamka kukummoja amenionyesha dalili ya ndui, nikamuwahi kumtoa nje ya banda na nmeenda kupata dawa OTC nimempa kachangamka vizuri jioni hii. Kuku wengine nimewapa chanjo ya chicken pox. Kesho nataka niwape antibiotic na vitamin pamoja. Je kuna madhara kuwapa dawa hizo kesho baada ya leo kuwa wamepata chanjo ya chicken pox? Je huyu kuku mgonjwa naweza mrudisha bandani kesho?. Ni hayo tu kwa jiono hii wadau wangu.
 
Jamani hali siielewi kuku wangu wa 2 wamevimba macho upande mmoja tatizo ni nini? Maana nimewapa chanjo ya ndui na pia otc baada ya siku 5 kutoka chanjo. Ila hali inanitia shaka, kuku wanakula na kupiga mishe zao kama kawaida. Wadau wenzangu naomba msaada wenu hapo.
 
Nakushauri uwatenge na hao kanga. Wape antibiotic na vitamin ingawa ninahofu umwachanja wakiwa tayari wagonjwa, kama mgonjwa anaweza kula na hauna hofu anaweza ambukiza wenzie mrudishe, unapata ushauri wa mtaalam au hata famasi? Wakipona kabisa uwape ya kideri/ newcastle
 
Nilishawatenga na kanga muda mrefu maana mayai yalikuwa hayakai Mama Joe. Nitajaribu kwenda famasi nikapate ushauri pia. Hawa wengine wako safi kabisa. Asante sana .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…