Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Suip,
Namba zangu ni hizo hizo uko sahihi. Usichukue hiyo Broiler premix,ni bora uiagizie hiyo DCP.
 
Habari mkuu Zantsan. Pole na majukumu ya kila siku.
Nimevutiwa sana uzi wako huu wa ufugaji wa kuku.
Nami napenda kuanza huu mradi mwakani mwanzoni.
Nimepanga nianze na kuku wa nyama kwanza wakat najipanga kwa wa mayai na kienyeji mradi ukichanganya.
Nategemea kuufanya huo mradi dodoma. Nina mtaji wa 1.5m. Je nianze na kuku wa ngap wa nyama?
je naweza kupata mchanganuo kwa hy 1.5m?cna mabanda. Ntashukuru kwa ushauri wako.
Mimi ni mfanyakazi wa manispaa nataka nijiongezee kipato kuptia huo mradi. Vp soko la kuku wa nyama dodoma mana mi ni mgeni kabs huko
 
Asante sana Teku kwa kuvutiwa na uzi huu. Kwa 1.5m utatakiwa uanze na kuku wa nyama 350 ambapo utatumia gharama ya tsh.1546250. Kutoka kwenye bajeti yako utatakiwa uongeze tsh 46250 kukamilisha mradi wako. Hesabu hiyo imezingatia kuwa huna mabanda ya kufugia na utakiwa ukodi chumba kimoja chenye ukubwa wa eneo la 3m x 6m. Baada ya wiki 6 utawauza kuku wako na utatengeneza mapato jumla ya sh 2275000. Faida utakayopata baada ya kutoa gharama zote ni tsh 728750/=.

Dodoma soko la kuku wa nyama lipo, japo kuna kuku wengi wa kienyeji lakini hawakidhi mahitaji kutokana idadi kubwa ya watu inayoongezeka kila siku hasa kutokana uwepo wa vyuo vingi vya kati na vikuu pamoja na serikali kuanza kuipa umuhimu kama makao makuu ya nchi, na kuhamishia baadhi ya wizara,pamoja na uwepo wa bunge kunakopelekea kuwepo kwa hotel nyingi sana. Pia kuku wa kienyeji wanauzwa kwa bei kubwa sana kitu ambacho walaji wengi hawabudu na hapo ndipo hitajio la kuku wa kisasa wa nyama linapokuja.

Ni mfanyakazi wa Idara gani hapo manispaa, maana hata mwenyewe niko hapa Dodoma, hivyo nadhani utakuwa na bahati kwani utaweza kupata msaada pamoja na ushauri wangu kwa ukaribu.

Kuhusu mchanganuo huwa tunaandaa kadiri mteja anavyohitaji na gharama zetu kwa ajili ya mchanganuo ni asilmia kumi ya mtaji uliowekezwa. Kwa wewe hapo gharama ya kukuandalia mchanguo itakuwa tsh laki moja na nusu, hii ikiwa ni asilimia 10 ya 1.5m. Michanganuo yetu tunayoandaa ni ya kiwango cha hali ya juu, licha ya kukuwezesha kuitumia kukopa bank, lakini pia inakupa mwongozo kamili ni namna gani utafuga kuku wako hatua kwa hatua na kukuwezesha upate tija uliyoikusudia.

Katika huo mchanganuo wa mradi wa ufugaji wa kuku wa nyama kila kitu kinachotakiwa kukuwezesha katika ufanisi wa ufugaji wako wa hao kuku hujumuishwa katika hiyo plan. Mradi wowote usiozingatia mchanganua sawa na kipofu anayetembea barabarani.
Asante.
 
kuna rafiki yangu anahitaji kufuga kuku wa Kienyeji elfu moja(yaani aanze na vifaranga mpaka hatua watakayoanza kutaga mayai ili atotoreshe kwa mara kadhaa kisha awauze kuku wakubwa),napenda kufahamu gharama za kuwakuza hawa kuku,banda tayari lipo,na gharama ya kuwahudumia kwa hiyo miezi sita itaweza kulipa.nitahitaji kufahamu gharama za kunifanyia mchanganuo huu.
 

Singo,
Ufugaji wa kuku wa kienyeji unalipa sana isipokuwa usiwe ule wa pure kuku wa kienyeji bali uwe ule wa kuku chotara kwasababu, kimsingi kuku chotara hana tofauti kubwa sana na kuku wa kienyeji kwenye ladha ya mayai na hata kile kiini chake nacho huwa kama cha kuku wa kienyeji, lakini pia hata ladha ya nyama yake huwa kama kuku wa kienyeji, hakuna tofauti hata kidogo.

Faida ya kufuga kuku chotara ni kuwa wanakuwa na ufanisi mkubwa kwenye utagaji na hata ukuaji wake tofauti na kuku wa kienyeji pure. Lakini pia kuku chotora wanachukua tabia ya kuku wa kienyeji kwenye suala la ustahimilivu dhidi ya magonjwa. Kwa mantiki hiyo nashauri huyo rafiki yako afuge kuku chotara badala ya kuku wa kienyeji. Hata hivyo,upatikanaji wa Kuku hawa chotara ni mkubwa na unaweza kupata kwa Idadi yoyote ile unayotaka.

Kuhusu gharama ya mradi wa ufugaji wa kuku chotara 1000 basipo banda ni tsh 20m. Gharama hizo zitahusisha mishahara ya wafanyakazi, gharama za chakula , gharama za kuwanunua wakiwa na umri wa siku moja(DOC), gharama za matangazo, tshirt,gharama za madawa pamoja na vitu vyote muhimu vinavyohitajika katika ufugaji wa kuku hao mfano vinyweo (drinkers),vilishio(feeders), mabox ya kutagia (nest box),bembea (peaches ),maranda nk.

Mradi wa ufugaji wa kuku aina ya chotara unalipa sana hasa kutokana na soko la aina hii ya kuku kuwa kubwa. Watu wengi wanahitaji kuku wa kienyeji na hawa chotara huwa wanauzwa kama kuku wa kienyeji. Kitu muhimu na cha msingi ni kuthibiti vifo.

Gharama ya kukutengenezea business plan ya kuku hawa elfu moja ni tsh.2m, lakini maelewano yapo. Kumbuka business plan tunazotengeneza ni business plan zinazokubalika bank, hivyo mtu anaweza kuzitumia kwa ajili ya kuombea mkopo bank kama atakuwa na dhamana, maana bank pamoja na kuwa na business plan nzuri huwezi pata mkopo mpaka uwe na dhamana (collateral).
 
Kwa wale wafugaji wa kuku wa mayai nina offer dawa mbili ambazo ni matokeo ya utafiti wangu ambao nimeufanya mwenyewe kama mtaalamu wa kuku na mifugo kwa ujumla, imekuwa ni dawa yenye mafanikio makubwa. Dawa ya kwanza ni dawa kwa ajili ya kuwafanya kuku wa mayai ambao hawaumwi na wanakula kawaida na ni wachangamfu ila hawatagi au wanaotaga chini ya kiwango, au walishituka kisha wakaacha kutaga kuna dawa ya kuwafanya kuku wenye hayo matatizo waweze kutaga zaidi. Dawa hii ya kuwafanya kuku watage zaidi naiuza kwa tsh laki moja, na yenyewe inachanganywa kwenye chakula cha kilo 300 sawa na mifuko sita kila mmoja ukiwa na kilo hamsini kisha watawekewa hawa kuku na watatakiwa wale chakula hicho kwa siku sita mfululizo. Pia sehemu ya dawa hiyo watatumia kwenye mji kadiri nitakavyoelekeza.

Ni hasara kubwa sana unakuta mtu umegharamia pesa nyingi kwa ajili ya kufanya uwekezaji kwenye mradi wa ufugaji wa kuku wa mayai lakini mara kuku wanapofika muda wa kuanza utagaji wanataga katika kiwango ambacho si cha kukupa faida au wakati mwingine hawatagi kabisa na hivyo kukufanya uendelee kuwagharamia katika kuwalisha nk, sasa utakapotumia dawa hiyo katika hali yoyote ile kuku wako watataga mayai mengi na faida ya ufugaji utaiyona.

Kwa kawaida kuku hushindwa kutaga kutokana na kwanza chakula tunachowapa kutokidhi kiwango kutokana na formula tunazotumia kutengeneza chakula kukosa ubora, lakini pili magonjwa nayo husababisha kuku kushindwa kutaga vizuri. Lakini sababu nyingine mishituko, kudonoana, kukatwa midomo nk nako pia huwafanya kuku kushindwa kutaga .

Ukiwa unahitaji kufundishwa namna ya kutengeneza dawa hiyo ada yake ni tsh laki moja na elfu hamsini.

Dawa ya pili ni dawa ya kuwafanya kuku wa kisasa watage mayai kama ya kienyeji yenye ladha na kiini cha njano kama yale mayai yanayotagwa na kuku wa kienyeji. Na unaweza ukayauza kama mayai ya kuku wa kienyeji. Dawa hiyo huchanganywa kwenye tani nzima ya chakula cha kuku yaani mifuko 20 kila mmoja ukiwa na kilo hamsini. Bei ya dawa hiyo ni tsh elfu hamsini.
Hakuna kitu kinachoshindikana. Leta tatizo lako la kuku usaidiwe.
 
Kuku wangu wanazubaa na kunya chokaa tatizo nini na dawa ya mioyoo
Kwa dalili ulizosema naamini watakuwa ni vifaranga,si ndiyo?Dalili zingine ni kuwa viranga wanaonekana wameshusha mabawa, wanasisinzia sinzia, wanaonekana kama wenye baridi, pia vifaranga wanakalia miguu na huwa hawawezi kutembea hadi uwasukume. Ikiwa tatizo ndiyo hilo,basi tafuta dawa ya trimazine 30% na dawa yoyote ya vitamini mfano vitalyte, amin'total, ant sress nk.Wakipewa dawa hizi kuku wako watapona.
 
Swali jingine mkuu je vifaranga bila source of heat kwenye room wanaweza kufa?
 
Mkuu Zantsan

hawa kuku chotara wanatabia ya kutoa wastani wa Mayai mangapi kwa mwaka au kwa kipindi fulani? je baada ya kutaga mzunguko mmoja hukaa muda gani na kuanza kutaga tena

je nikiwalisha layers mash wanaweza kutaga mfululizo kama kuku wa layers na hapo hapo wakiwa wanapandwa na jogoo?

je kuna uwezekano wa kuwahasi majogoo ili kuyanenepesha na ku-control male to female ratio bila kuondoa/kupunguza idadi ya majogoo bandani?
 
Last edited by a moderator:

jogoo langu la kienyeji limeacha kuwika,je hilo linasababishwa na nini?
 
jogoo langu la kienyeji limeacha kuwika,je hilo linasababishwa na nini?

Yawezakana ni mgonjwa wa mafua makali (coryza) ila wataalam akina Zantsan watakujibu mimi si mtaalam kihivyo.
 
Last edited by a moderator:
Habari yako naomba ni PM namna ya kutengeneza chakula cha kuku wa kienyeji kwani ninakuku wa kienyeji wapatao 30 ila najikuta nanunua tu chakula sasa nafikiria kutengeneza mwenyewe itanisaidia kupunguza garama naomba msaada wako.

Asante
 
Habari yako naomba ni PM namna ya kutengeneza chakula cha kuku wa kienyeji kwani ninakuku wa kienyeji wapatao 30 ila najikuta nanunua tu chakula sasa nafikiria kutengeneza mwenyewe itanisaidia kupunguza garama naomba msaada wako.

Asante
Gceline sijui kama wameshaku PM ila kwa manufaa ya wafugaji wa kuku katika kupitapita mitandaoni nimepata Link ambayo inamanufaa kwani ina PDF za 1.Kulea vifaranga
2.Kutengeneza vyakula
3.Sehemu ya kwanza ya Ufugaji bora wa kuku
4.Ufugaji bora wa kuku wa asili
5.Uuzaji wa Mazao ya kuku.
Ukibofya hiyo Link hapo chini kama una simu smart au Computer unadownload nakusoma kupitia PDF Reader au Adobe Reader.
Kazi kwako
BOFYA HAPA
 
Last edited by a moderator:
sory wadau, hv kuna tofauti kati ya NEW CASTLE VACCINEna GUMBORO VACCINE.

Tofauti ipo. Hizo ni chanjo za magonjwa mawili tofauti yaani new castle na Gumboro /Gomboro. Soma threads tofauti za ufugaji humu JF wataalam wameongelea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…