Ufugaji wa Mbwa wa kisasa ni almasi mpya kwa vijana

Ufugaji wa Mbwa wa kisasa ni almasi mpya kwa vijana

Agrey998

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2019
Posts
417
Reaction score
550
Miaka ya karibuni vijana wengi wamejiingiza katika biashara ya ufugaji wa Mbwa wa kisasa kwa kuimport mbwa nje kama Germany shepherds long coat, Boerbull, Caucasian shepherd, Rottweiler's na wengine na wakifika hapa huwazalisha na kuuza watoto (puppies) huku wateja wao wakubwa wakiwa ni matajiri au Watu ambao nao wanaingia kwenye biashara hiyo.

Puppy mmoja wa miezi miwili ukikuta ni hizi local breed za shepherd anapatikana kwa laki tano au lak nne
. Lakini ukikuta ni Germany shepherds original basi ni laki tisa hadi milioni na mbwa mwenye uzao mzuri anaweza kuzaa hata watoto kumi.

Ukiuza ni milioni 10 japo utaingia gharama za chanjo kama Dhlp na pavo virus ambazo ndio za muhimu ili mbwa wasikufie na pia usafi ni muhimu sana na ufanywe kila siku na pia kuwalisha lazima uwalishe kisasa tena wale hata mara mbili kwa siku na uwape protien suppliments ili kuwaboost . Hapo ndio utaona pesa.

N.B. Hii kazi kama ni mtu mwenye kinyaa Bora uache maana itakutesa .

Hii kazi ukitaka ikulipe lazima uipende sana.

Hii kazi inahitaji uvumilivu wa hali ya juu

Ukifanya hii kazi basi lazima uwe na mishe nyingine pembeni ya kukuingizia hela .

Mwisho ni kwamba pesa sio rahisi pia kwenye ufugaji huu lazima upambane.

Nawasilisha
 
Hii biashara ni nzuri Sana,ila mbwa ambao Wana soko Sana ni wale wenye midomo mipana na muhimu ni uwe na connection na wazungu na wale wafanyakaz wa UN hapa lazima upige hela
 
Hii ni biashara yenye pesa sana na wajanja sasa hv wanasajili mbwa wao kwenye east Africa kennels Club pale Nairobi mbwa akiwa registered anauzwa popote dunian
Aisee!!?
 
Miaka ya karibuni vijana wengi wamejiingiza katika biashara ya ufugaji wa Mbwa wa kisasa kwa kuimport mbwa nje kama Germany shepherds long coat, Boerbull, Caucasian shepherd, Rottweiler's na wengine na wakifika hapa huwazalisha na kuuza watoto (puppies) huku wateja wao wakubwa wakiwa ni matajiri au Watu ambao nao wanaingia kwenye biashara hiyo.

Puppy mmoja wa miezi miwili ukikuta ni hizi local breed za shepherd anapatikana kwa laki tano au lak nne
. Lakini ukikuta ni Germany shepherds original basi ni laki tisa hadi milioni na mbwa mwenye uzao mzuri anaweza kuzaa hata watoto kumi.

Ukiuza ni milioni 10 japo utaingia gharama za chanjo kama Dhlp na pavo virus ambazo ndio za muhimu ili mbwa wasikufie na pia usafi ni muhimu sana na ufanywe kila siku na pia kuwalisha lazima uwalishe kisasa tena wale hata mara mbili kwa siku na uwape protien suppliments ili kuwaboost . Hapo ndio utaona pesa.

N.B. Hii kazi kama ni mtu mwenye kinyaa Bora uache maana itakutesa .

Hii kazi ukitaka ikulipe lazima uipende sana.

Hii kazi inahitaji uvumilivu wa hali ya juu

Ukifanya hii kazi basi lazima uwe na mishe nyingine pembeni ya kukuingizia hela .

Mwisho ni kwamba pesa sio rahisi pia kwenye ufugaji huu lazima upambane.

Nawasilisha
Ukubwa wa soko kwa upande wa wateja likoje? Turn over rate ya commodity yenyewe ikoje ukizingatia swala la frequency ya mteja mmoja au mwingine kurudi/ kuja kununua tena bidhaa hiyo; kwamba tuseme mhitaji akinunua mbwa leo, ni baada ya muda gani anaweza akarudi tena kwako kuja kununua mbwa mwingine?
Kwa watu walliosoma business au marketing, apparently hii inaonekana kama ni biashara lakini kiukweli hii lazima ni biashara kichaa, and as a matter of fact, I myself would'nt dare advice anyone to involve themselves in this type of business
 
Back
Top Bottom