Ufunuo wa Mchungaji!


Binti Sayuni,

Kanisani kuna ule wimbo "Toa kwanza boriti, kwenye jicho lako, ndipo utaona kibanzi, kwenye jicho la mwenzako...."
 
As a nation tumepoteza mwelekeo, hakuna moral wala ethics zozote. Hatueshimiana wenyewe kwa wenyewe, mfano utakuta mmepanga mstari benki kwa masaa na mtu mwingine bila aibu anakuja na anaingia mbele ya mstari bila hata aibu.Na mara nyingine raia au wateja wengine hatakusema lolote hawasemi.....its a shame.
 


Mimi nadhani tungeweza kuanza na vitu vidogo vidogo tu. Tukiweza hivyo basi tunasonga mbele kugusa vikubwa. Huwa nashangaa sana Ulaya jinsi watu wanavyoheshimu mistari mfano kwenye kupanda basi. Najiuliza sana kama itawezekana siku moja na sisi tukae kwenye mstari wa kupanda dala dala ya Mbagala. Napata kizunguzungu.

Lakini tunapochefua zaidi ni pale tunaposhindwa kufanya usafi wa mazingira yetu nyumbani. Niliwahi kuishi kwenye nyumba moja huko Morogoro (tulikuwa kama familia kama 6 hivi). Suala la kusafisha choo tu (acha mazingira kwa ujumla) ilikuwa ni vita.
 
Rev. Kishoka,
Naam huyu ndiye mchungaji haswaaa ambaye siku zote amekuwa aikihubiri imani ya Uhuru wa mwafrika dhidi Kutawaliwa. Shukran kwa kuendeleza gospel hii ambayo pengine (ni matumaini yangu) itaweza kumwokoa kifikra Mdanganyika wa asili..

Ndivyo Tulivyo ni pamoja na Utumwa wa akili, Ulimbukeni na imani dhoofu ya dini, jambo ambalo linatokana na kutakuwa na ELIMU inayohusu Watu na Mazingira yake.
Mkuu wangu Ndivyo Tulivyo inaanza toka enzi ya Utumwa wakati waarabu wawili wenye magobole ya kushindilia risasi waliweza kusanya watumwa 1,000 toka pande pande zote za nchi na kuwaburuza wadangayika hawa hadi Bwagamoyo, wasifikirie nguvu ya umoja wao unaweza kuwashinda waarabu wawili badala yake wengi wa watumwa waliona fahari kujiunga na Unyapala kuwakandamiza ndugu na jamaa zao ili mradi wapate unafuu wa muda..mwisho wa safari hata wao Manyapala waliuzwa kwa mafungu na kusafirishwa kwa mashua hadi Zanzibar kwa usafiri ua utumwani ng'ambo.

Kati ya kuchukuliwa utumwa hadi kupelekwa ng'ambo hakuna historia yoyote ya resistance toka kwa Wadanganyika na historia itaendelea kutusuta kwamba sio sisi waafirka tuliolaani Utumwa na kuutokomeza isipokuwa ni wazungu na watu wa mataifa mengine walioweza komesha biashara hii, sisi hatukuwa na njia wala mbinu ya kujikomboa sisi wenyewe, it never cross our mind.
Hivyo utumwa wa akili ukajenga taifa jingine la kesho (kina sisi) ambalo ni tegemezi la gospel (msahafu) toka kwa waliobarikiwa yaani wazungu. Hatuna elimu ya historia yoyote inayoweza kuwa mfano bora kama tunavyosoma historia za wenzetu ambao kwa kila adha waliyoipata walitokea mitume ama wakozi baina yao.
Na ndio elimu tunayojifunza leo shule, historia ya wengine kina King Arthur, Kaizal, Yesu na Muhammad walivyoweza kuokoa watu wao kuwa ndio somo kubwa kuwatazama wao badala ya messege ya mafundisho yao tunaweza vipi sisi kuitumia katika maisha yetu. Lakini tazama basi focus kubwa ya Mdanganyika ni kwamba matukio yote yale yalikuwa kazi ya MUNGU..

Niarudia kusema tena kwamba mataifa yote duniani yamepitia Utumwa, toka Wataliani, Wayahudi, Wahindi, Wachina hadi sisi Wabantu sote tumepitia utumwa wa aina moja hadi nyingine lakini ni kundi moja tu la Watumwa yaani sisi Wabantu ndio pekee tulioshindwa kabisa kujitetea ndani ya utumwa huo. Hatuna historia ya mitume amam wozkozi wetu na kama ipo basi ilifutwa haraka sana kama tunavyofuta historia nyingi za matendo ya viongozi wokovu toka kina Chaka Zulu, Mirambo, Mkwawa, Magi Sina na hata Mwl Nyerere ambao walikuwa pingamizi wa kutawaliwa kwa hali na mali..

Leo hii, mwalimu Nyerere anazungumziwa kwa taabu tulizopitia ktk Ujamaa, taabu mabzo huwezi linganisha hata kwa chembe na taabu za wayahudi walipookolewa na Moses toka Misri, au David na utawala dhalimu wa Maphalesia kina Goliath, Waingereza na mataifa ya Ulaya dhidi ya utumwa na kutawaliwa..Waumini wa Yesu na Muhammad toka tokana na imani potovu za uuungu yote haya ni mafundisho ambao wenzetu wameyatukuza na kuwa msingi wa mafundisho ya ELIMU yao.

Huwezi kumwambia kitu Myahudi na Moses hata kama historia inaonyesha mateso makubwa waliyoyapata Jangwani. Huwezi kuwaambia kitu Waingereza, Wataliani na mataifa mengine ya Ulaya juu ya falme zao kwa sababu wanaelewa chimboko la falme hizo ktk kuwakomboa wao toka utumwani na historia yao inaendelea kujengeka ktk kuboresha zaidi mfumo wa maisha yao ili hali ile isiweze tena tokea. Ni kutokana na historia ya matatizo na mahitaji yao ndipo ubunifu wa kisayansi na kiteknolojia unapokuja kuziba pengo hilo na elimu hiyo kuhakikisha pengo hilo halitaweza tokea tena kwa kupitia njia zile zile..Ndivyo wenzetu wanavyoweza kuendelea.

Lakini sio sisi Miafrika.. ndio kwanza tunatafuta mbinu za kutokomeza historia na hata jiografia zetu, kwa sababu elimu kwetu ni sawa na msahafu ulokwisha andikwa na mzungu kiasi kwamba mikakati yetu haifuati wala kutazama matatizo na mahitaji yetu isipokuwa tunataka tufanane na wazungu au uzunguni hivyo ni vitu gani vinatakiwa kuwepo. Ndio maana kilimo hakikupewa nafasi, Umeme haukupewa nafasi, Maji hayakupewa nafasi na HATUNA elimu yoyote ktk utatuzi wa maswala hayo kiasi kwamba hata Ubunifu hakuna.
.
Mkuu wangu Rev. Kishoka mimi hadi leo sijui msingi wa ELIMU yetu hata kidogo ikiwa elimu hiyo haina manufaa kwa jamii ktk matumizi yake. Sioni faida ya kusomea hali ya mazingira wakati huo huo toxic zote mbaya dampo lake ni Afrika. Maradhi kama maleria, kipindupindu, Ukoma, Utapia mlo ni maradhi yalikuwepo Afrika toka enzi ya Adam lakini yamepatiwa ufumbuzi gani - Hakuna, na wasomi tunao wengi tu madaktari (phd) lakini maradhi na njaa ni pamoja na mfulululizo wa maisha yetu hivyo kuwa Id ya mwafrika.
Nguvu kubwa ipo ktk kutibu mtu alokwsiha athirika na sii swala la kinga au kutokomeza virusi vinavyoambukiza kwani hatuna utamaduni wa kuzuia ama kuweka kinga..Ndio maana unaona taka zimejazana kila sehemu, madimbwi ya maji machafu, mito ya maji hutumika kwa kufulia, kuoga na kunywa watu na wanyama ili mradi elimu yetu haina manufaa kabisa. Yote haya unaambiwa ni kazi ya MUNGU!

Tunasomea Udaktari wakati sisi ndio waagizaji wakubwa wa bidhaa zinazoambukiza maradhi ya ajabu ajabu.. Leo hii hesabu kubwa ya wanawake wanakufa ktk uzazi kuliko wakati wowote ule. Uzazi imekuwa ni tatizo kubwa mwanamke anaposhika Mimba ni mguu ndani mguu akhera hakuna ubunifu wowote zaidi ya kumwomba MUNGU.


Swala la Njaa lipotoka liijue dunia hii, nakumbuka enzi za mkoloni tulikuwa tukila Bulga na nakumbuka vizuri maziwa ya unga ya misaada toka Marekani nikiwa shule ya msingi miaka ya 60, lakini matatizo hayo bado yanaendelea hadi leo miaka 40 baadaye pasipo kupumzika tukitegemea MUNGU atuokoe yeye. Kwa hiyo ukitazama ktk matatizo na mahitaji yetu hapa mwokozi ni MUNGU, na bahati mbaya hata imani za dini zetu zinatupeleka kuamini hivyo kwamba matatizo ya binadamu ni mitihani ya MUNGU..subira ndio dawa kubwa Mungu atafungua tu.

Lakini ktk kutafuta maendeleo kuelekea Uzunguni au kufanana na wazungu hilo ndilo jukumu kubwa la Utawala bora. Na wananchi wote wanategemea kuona Tanzania ikifanana na London au Ulaya. Hivyo mahitaji na matatizo yetu yataweza tu kujondoa kama tutaweza kuijenga Tanzania ya leo kuwa kama Ulaya..while tukijua fika kwamba Wadagananyika wote ukiwapeleka London kesho na kuondoa Wazungu matatizo yote ya Afrika na waafrika yatahamia London. London itakuwa Mogadishu, Somalia within 10 years na tutaanza tena kujaribu kuigeuza London iwe kama Dar es Salaam ya wazungu..We never identify our PROBLEMS and our NEEDS! na itakuwa vigumu sana kwa sababu kwanza hatukubali tuna matatizo (in denial)..
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO
 
Mkandara
Miafrika ndivyo Ukiwemo wewe? na Rev. Kishoka?? huko ni kukata tamaa. kuna watu wengi tu wanajitahidi kujikwamua kwenye makucha ya manyang'au na mafisadi...afadhali uwatafute uungane nao kuliko kukata tamaa.
 
Mkandara
Miafrika ndivyo Ukiwemo wewe? na Rev. Kishoka?? huko ni kukata tamaa. kuna watu wengi tu wanajitahidi kujikwamua kwenye makucha ya manyang'au na mafisadi...afadhali uwatafute uungane nao kuliko kukata tamaa.


Miafrika ndivyo tulivyo.
 
Mkandara
Miafrika ndivyo Ukiwemo wewe? na Rev. Kishoka?? huko ni kukata tamaa. kuna watu wengi tu wanajitahidi kujikwamua kwenye makucha ya manyang'au na mafisadi...afadhali uwatafute uungane nao kuliko kukata tamaa.
mkuu unauliza kitu ambacho ni wazi kabisa?.. hivi ukisikia Miafrika ndivyo TULIVYO, wewe unaelewa vipi?
 
Miiafrika makandara anayosema ndio sisi wote ambao tunakubali kuburutwa kila siku, na kuja kwenye forum hii kuandika tu bila kuchukua initiative yoyote.

Inasikitisha kuona Mkuu Jk alipochukua nchi akawapeleka mawaziri wake wote Ngurdoto kwa "retreat" iliwapange mikakati yakutuondoa kwenye umasikini. Niliambiwa mawaziri wote waliimbiwa wareport airport ya Dar na wakasafiri hadi KIA then waakanyang'anywa simu zao za mikononi. Kisa ili waweke focus kwenye mambo yatakoyozungumzwa huko kwenye retreat. kama hizo strategy ndio hizi tunazoziona how they run the country sasa hivi, ule ulikuwa ni ufyoroo mtupu. Jk alitakiwa awapeleke huko vijijini washinde na familia ya mkulima, waamke saa kumi na moja asubuhi wakatafute maji, then waende wakatafute kuni. washinde siku nzima shambani wakilima huku hawajui watakula nini jioni wakirudi nyumbani. Na kama mmoja wao akikatwa na jembe abebwe na baiskeli kwa kilomita arobaini kwenda kwenye dispensari ambayo haina dawa. wakirudi nyumbani walale kwenye ngozi wakati dari linavuja na kibatari hakina mafuta ya kuchoma utambi. Nafikiri wangepata uchungu wakujua ni nini asilimia 80 ya watanzania maisha yao yalivyo. Kuishi kwao daresalaam na kupanda Emirates na KLM first class wanasahau walipotoka kabisa.

Kingine kinachonistaajabisha hatasiku moja huyu JK(Vasko Dagama) sijamuona akisimama au kuongelea jambo lolote huku akiwa na kundi la watu wanaomshahuri, nikiwa na maanisha kama tunavyomuona Obama akizungumzia Economy huwa anasimama na washauri wake na kuwaambia wananchi hawa ndio watu wanonishauri kwenye hili swala, na credibility zao zinajulikana lakini kwetu Jk akizungumzia umeme hatakumuona yuko na Waziri wa nishati au maengineer wa umeme or consultants...hakuna. Je huo ushauri anaopata hana hata pride ya hao watu?
 
MSOME HUYU;
WITO KWA WANANCHI KUHUSU KUKABILIANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA, HUSUSAN AIBU YA UCHAFU

02 AGOSTI, 2009

UTANGULIZI
Katika chama chetu, tumekuwa tukitafakari kwa muda mrefu sasa kuhusu suala la utunzaji wa mazingira na usafi hapa nchini na kwingineko duniani. Tumegundua kwamba taifa letu lipo hatarini kutokana na uharibifu wa mazingira, na kukithiri kwa uchafu hususan mijini.

Kama tunavyoelewa, Utunzaji wa mazingira ni muhimu kwa uhai na afya ya jamii. Wataalam katika tafiti zao mbalimbali wamethibitisha kuwa gharama zitumikazo katika utunzaji wa mazingira huokoa maisha ya wanadamu na viumbe vingine. Tena utunzaji wa mazingira ni hatua inyoweza kuhesabika kuwa kinga au tahadhari muhafaka kiafya. Tukichukulia mfano wa matokeo ya utafiti uliofanywa na shirika la Water Aid (la Uingereza) kwamba shilingi moja ikitumika katika kutunza mazingira/kuhakikisha uwepo wa usafi, inaokoa shilingi tisa ambazo zingetumika katika matibabu ya magonjwa mbalimbali, hususan yatokanayo na hewa chafu, maji machafu na taka zinazozagaa.

Suala la usafi na utunzaji wa mazingira ni miongoni mwa ajenda nyeti duniani, likiwa ni mojawapo ya changamoto zinazoukabili ulimwengu kwa sasa. Tumesikia mara nyingi juu ya ongezeko la joto duniani, upungufu wa hewa safi na maji safi, na kadhalika. Ni jambo la kutia matumaini kwamba zipo jitihada za kimataifa za kukabiliana na changamoto hii, ili kudumisha ustawi wa mwanadamu hapa duniani kwa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UHARIBIFU WA MAZINGIRA NA UCHAFU KATIKA TAIFA LETU
Wakati mataifa ya wenzetu yakifanya kila linalowezekana dhidi ya changamoto hii, hivi leo, sisi watanzania katika nchi yetu, tumekuwa wachafu kupindukia na waharibifu wa mazingira katika namna isiyo ya kibinadamu kabisa.
Mifano ya haya si ya kutafuta;
Sote ni mashahidi wa mlundikano mkubwa wa takataka katika masoko barabara za hapa nchini. Zipo habari kuwa baadhi ya watu wamefikia kujisaidia katika mifuko ya plastiki kwa sababu ya kukosa vyoo wanapo kuwa masokoni (matharani soko la Ilala). Kadhalika siku hizi mtu kula muwa au kitu kingine chochote na kurusha mabaki ovyo tu barabarani/njiani.
Kana kwamba haitoshi, imekuwa ni tabia ya kawaida kwa baadhi ya wananchi kutapakaza vinyesi barabarani, almaarufu ‘kutapisha chemba’ pindi mvua zinaponyesha. Hili linaendelea bila watanzania kuonekana kujali na viongozi wetu katika ngazi zote kutolikemea.

Aidha, miji ya Tanzania imekithiri kwa ujenzi holela, yaani usiofuata mipango miji wala viwango, kiasi kwamba mitaa haipitiki na mfumo wa usafishaji mitaa hiyo unakuwa mgumu kabisa.
Kadhalika kana kwamba hatujaelewa, watanzania tumeendela na matumizi ya mifuko ya plastiki, licha ya kuambiwa madhara ya mifuko hiyo, tunauziana michicha inayoooteshwa kando ya barabara bila kujali kwamba michicha hiyo ni myepesi kunyonya madini ya Lead yasababishayo kansa. Haishangazi kwamba wagonjwa wa kansa wameongezeka nchini.
Matatizo haya yakujumlisha na uwepo wa kelele za bar katika maeneo ya makazi ya watu, uwepo wa karakana ‘Gereji-bubu’ katika makazi ya watu, uvuvi haramu, uchomaji misitu na mbuga, uharibifu wa vyanzo vya maji, kutapakazwa ovyo kwa sumu za viwandani na migodini, yanaifanya nchi yetu isiwe mahali bora pa kuishi.

Ndugu wananchi, leo hii jiji la Dar es Salaam linapigiwa mfano wa majiji yanayongoza kwa uchafu duniani. Kwa mujibu wa Takwimu za mwaka jana (2008), Dar es salaam ni jiji la 12 kwa uchafu duniani (mwaka huu 2009, ni la 10), na la tatu Afrika Mashariki na kati. Na wala halisingiziwi, sijui tunaweza kukanushaje sifa hii katikati ya uwepo wa harufu mbaya ya Ocean Road, na milipuko ya mara kwa mara ya gonjwa la kipindupindu katika mitaa ya jiji. Katika karne ya 21, ni aibu kubwa kwa mji kama Dar es Salaam kukithiri kwa uchafu namna hii .

Kwa ujumla katika maeneo ya miji, takataka zinazotoka katika viwada zina metali kama vile zebaki (Mercury), Chromium, lead, Cadmium, chumvi ya cyanide, nitrite na natrate, organic matter, na sumu za kemikali zinazotokana na bidhaa zinazotengenezwa na viwanda hivi, zinaenda moja kwa moja katika vyanzo vya maji. Tatizo hili liko katika maeneo mbalimbali ya nchi, ilikwa ni pamoja na; Tukuyu, Korogwe, Chunya, Singida, Arusha, Tanga, Dar es Salaam, mto Msimbazi, mto Ngerengere Morogoro, Themi Arusha, ziwa Victoria, mto Karanga, Njoro, Rau- Moshi na mto Kiwira ( Wilaya ya Tukuyu)

Vilevile takwimu zinaonesha kuwa Tanzania ni nchi ya 4 Afrika katika ukataji miti, hukata zaidi ya hekta 500,000 kwa mwaka. Zaidi 60%ya ardhi ya Tanzania inakabiliwa na hatari ya kuwa jangwa.


Hapo ndipo tulipo kwa nchi ambayo, wakati wa Serikali ya awamu ya tatu, tulipewa heshima ya kuongoza dunia katika suala la utunzaji mazingira, pale Mhe. Arcado Mtagazwa, aliyekuwa waziri katika ofisi ya makamu wa rais inayoshughulikia mazingira alipopewa dhamana na ulimwengu kuwa rais wa baraza la mazingira duniani.

Tanzania ni chafu isivyomithirika, licha katiba ya nchi kuzingatia haki za watu kuishi, na licha ya kuwepo kwa sheria mbali mbali za kudhibiti uharibifu wa mazingira.
Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania katika ibara ya 14 inatamka jambo ambalo undani wake una uhusiano na suala la usafi na usalama wa mazingira. Katiba inatambua haki ya mtu kuishi, haki hii inafungamanisha hifadhi yak maisha yak mtu, haki ya kuishi katika mazingira safi na salama, katika nyumba bora, kupata huduma bora za afya, kuishi katika makazi yenye heshima (sio kwenye nyumba za maboksi na uchafu) ni wajibu wa serikali kuhakikisha upatiukanaji wa haki hii.
Matharani, hata serikali inapobomoa nyumba za watu, jukumu lake la maana halipaswi kuwa kuwalipa fidia bali kujenga nyumba mbadala, katika eneo mbadala la kuishi. Serikali inatakiwa kujenga nyumba za kisasa za kuishi, lakini badala ya serikali kufanya hivyo imewaachia watu binafsi kujenga na kuendesha kwa ufisadi nyumba za kupanga mijini hata kwa ajili ya watumishi wa umma. Wakati tunayo sheria yak sheria ya pango (the rent restriction act of 1971) inayokataza kuchukua kodi ya nyumba kabla yak mpangaji kukaa katika nyumba kwa kipindi husika, imekuwa kana kwamba sheria hiyo haipo na serikali iko likizo wakati wenye nyumba binafsi wakiendelea kuwatoza kodi kwa miezi 6 hadi mwaka mzima kabla kwakipindi ambacho mpangaji hajakaa katika nyumba.
Tunasema hivi, licha ya kwamba nyumba nyingi mijini hazina hadhi ya kulinda haki ya mtu kuishi katika mazingira safi na salama, si halali kisheria kwa wenye nyumba kutoza kodi kwa kipindi cha zaidi yak mwezi mmoja kwa mara moja tena kabla yak mpangaji hajakaa kwenye nyumba.

Vile vile haki ya kuishi inabeba ndani yake suala zima la afya. Kwa maana hiyo kila mtu ana haki ya kulindwa afya yake.
Wakati wa serikali ya awamu ya kwanza, serikali ilikuwa na sera ya afya iliyokuwa na mtazamo wa preventive medicine (kinga dhidi ya magonjwa). Chini ya sera hiyo serikali iliwajibika kuweka mazingira mazingira anamoishi mtu kuwa katika hali ya usafi na usalama. Enzi za mwalimu mabwana afya na wasaidizi wao walipita mitaani wakifukiza madawa kwenye madimbi ili kuharibu mazalia ya wadudu wasababishao magonjwa, hususan mbu. Zoezi hili lilifanyika kila wiki kwa sababu za kitaalam kwamba kuzaliana kwa mbu huchukua takribani siku saba.
Bahati mbaya serikali ya sasa haina habari na wajibu huo. Badala yake imegeukia sera au mtazamo wa curative medicine (tiba tu dhidi yak magonjwa) mtazamo ambao ni aghali sana, na mara nyingi hauna matunda mazuri. Vile vile mtazamo huu umetoa fursa kwa mafisadi kuchezea maisha ya watu, kwa kuingiza nchini madawa yaliyo chini ya viwango, ndio maana leo hii kila uchao tuaambiwa dawa hii na hii hazifai tena katika matibabu ya malaria n.k. yamkini viongozi wan chi hawajali maana wanajua kutibiwa kwao ni nchi za nje.
Suala la mzingira na haki ya kuishi linaathiriwa kwa kiasi kikubwa na sera ya uwekezaji. Sera hii kwa jinsi inavyotekelezwa na serikali ya CCM, haizingatii usafi na usalama wa mazingira. CCM inaruhusu uwekezaji katika miradi chafuzi yak mazingira, inayozalisha taka mbali mbali za sumu. Matharani Uwekezaji katika Asbestos uliokataliwa katika bara la Ulaya hapa Tanzania unakumbatiwa; Kampuni yak Barrick Gold ambayo haizingatii viwango vilivyowekwa kimataifa vinavyokubaliwa na World health Organization, kwa mfano inapotumia Zebaki kusafisha dhahabu na kutililisha mabaki yake katika mito, imefanya uharibifu katika nchi nyingi, nasi ilihali tukijua hilo tumeipokea nchini.
Migodi mingi nchini yenye uwekezaji wa kigeni, licha ya kwamba taifa halipati faida ya maana kutokana na migodi hiyo, migodi hii haizingatii kanuni za kutunza usalama na usafi wa mazingira.
Yamesemwa mengi kuhusu jinsi uwekezaji katika migodi ulivyoleta madhara kwa wananchi kiafya, cha kushangaza badala ya serikali kutafuta ufumbuzi ilikimbilia kukanusha yanayosemwa. Hatuelewi kwa nini serikali ihamue kuchukua hatua ambazo zinausaliti umma kwa kiasi hicho.

Japo sheria za mazingira na usafi zipo, serikali imeshindwa kuzitekeleza. Tatizo jingine ni kwamba japo sheria ya mazingira inazungumzia kufanyika tathmini ya madhara ya miradi kwenye mazingira, sheria hiyo haitoi fursa ya kufanyika kwa tathmini kwa njia huru/independent assessment, matharani inayoweza kufanya na asasi za kiraia

Sheria na sera tulizo nazo nchini kuhusu usafi na usalama wa mazingira, ni pamoja na; National Environmental Action Plan ( NEAP - 1994), National Environmental Policy (NEP- 1997), National Action Plan ( 1999/2004, Sheria ya machimbo ya mwaka 1998, Sheria ya mazingira ( Environmental Management Act 2004 ( EMA 2004), iliyoambatana na mkakati wa ukombozi wa mazingira wa mwaka 2004.
Ni dhahiri sheria hizo hazifuatwi na yamkini hazifahamiki miongoni mwa Watanzania walio wengi

Serikali kuu badala ya kuchukua hatua, inabaki kulalamika kuwa kuna uhaba mkubwa wa watendaji na vitendea kazi, uhaba mkubwa wa watumishi wa sekta ya afya, ujenzi holela usiozigatia mipango miji, biashara holela, ongezeko la watu mjini.

Kwa upande wa Halmashauri za Wilaya, tunaambiwa kuna maafisa afya na wasaidizi wao ambao hufanya kazi za ukaguzi wa mazingira katika Halmashauri za jiji, manispaa, miji, wilaya, kata na vijiji na wanapobaini chukizo huchukua hatua kwa kutumia sheria za afya. Katika Serikali za mitaa/vijiji kamati za afya zinapaswa hushiriki kupanga na kusimamia mipango ya usafi wa mazingira, kuelimisha jamii na kuandaa sheria ndogo ili kudhibiti uchafuzi wa mazingira. Bahati mbaya haya hayafanyiki hata kidogo.

Suala la uchafu mijini lina hata harufu ya ufisadi, matharani hapa Dar es Salaaam, kuna habari kuwa Kampuni ya MJENT(mali ya Mhe. Kingunge), imeiondoa kinyemela Kampuni ya SINCLON, iliyokuwa na tenda ya kuzoa taka. Sinclon imekwenda Mahakamani kuweka pingamizi dhidi ya hatua hiyo. Hii ni sababu mojawapo ya kufurika kwa taka katika maeneo ya jiji.


NINI KIFANYIKE KWA SASA
ninatoa wito kwamba yafuatayo yafanyike mara moja;
  • Watanzania wote tuchukue kila aina ya tahadhari ya kutuhepusha na madhara ya uchafu. Tunawaomba wananchi waongeze biidi katika kushiriki kikamilifu kutunza usafi wa maeneo wayoishi.

  • Serikali iwajibike moja kwa moja kutunza mzingira katika kila mtaa kupitia mtazamo wa awali wa Kinga kuliko tiba

  • Serikali itoe ushirikiano wa kutosha kwa taasisi mbalimbali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na wanaharakati, katika zoezi zima la kuhifadhi mazingira.

· Serikali itoe elimu ya Sheria za mazingira hadi ngazi za vijiji na vitongoji kwa wananchi na kuhakikisha sheria hizi zinafundishwa hata mashuleni kuanzia shule za msingi

  • Baraza la Mazingira la Taifa NEMC lichukue hatua thabiti za nguvu kukomesha balaa la uharibifu japo kwa kutumia sheria zilizopo.

  • Halmashauri za miji/serikali za mitaa zitumie ipasavyo sheria ndogo ndogo za kudhibiti vitendo vya uchafu, zinunue magari ya kutosha na kisasa ya kubebea taka, ziwapatie watendaji vitendea kazi bora ili kuleta ufanisi wa kazi na kuepuka magonjwa ya kuambukizwa, zihakikishe uwepo wa mapipa ya kuhifadhia taka katika vituo vya mabasi na maeneo ya hadhara.

Mungu ibariki Tanzania!
Ahsanteni kwa kutusikiliza,

George Leonard Kahangwa
KATIBU IDARA YA ITIKADI NA MAFUNZO
 
Charuka,
Ukimsoma vizuri huyu mh. Kahangwa utagundua kwamba anazungumza yale alosoma shuleni au yale wazungu wanayosisitiza. Yaani Uchafu wa mazingira yetu kauona baada ya kupewa kipimo na wazungu laa sivyo hakuona makosa kabisa kwani usafi wa mazingira huanza toka mji mnapokuwa planned.
Kama ujenzi wa nyumba vile, huwezi jenga nyumba pasipo chooo kisha ukaanza kuzungumzia baada ya kuambiwa na majirani kuhusu uchafu wa makimba yalozagaa barazani mwako...

Mkuu wangu sisi Wadanganyika siku zote hu deal na matatizo yanapotokea, hatuna utamaduni wa kufanya ukarabati kabla ya matatizo. Tazama hizo nyumba zetu zote ukaratabati haufanyiki hadi nyumba imeanza kuvuja na ajabu ni kwamba tutaziba tu yale matundu yanayovujisha. Usipoziba ufa Utajenga ukuta ni methari ambayo hatufahamu undani wake zaidi ya kuweka kiraka au kuziba tobo!

Ndio maana leo unaona tunabishana juu ya Dowans na IPTL ambazo ni katika kuziba matundu au kuweka kiraka cha umeme na ndio maana utetezi wote wa serikali na wananchi unahusu gharama za ununuzi wa mitambo mipya wakati kuna mingine mibovu na iliyochakaa ipo nchini..fikra za kuweka viraka viraka tu..
Ni kwa sababu kiraka hakiwekwi kama an emergency solution bali ni a short term solution..meaning kiraka kinakubalika na hugeuka kuwa fashion ya vazi zima.. Ndicho kilichotokea ktk sakata letu la Umeme, maji, afya, mazingira, kilimo, viwanda ni fujo tupu kwani vitu hivi vyote vinaenda pamoja..
 
Yote ni kweli. Lakini tatizo kubwa ni toka ngazi za juu kama viongozi kazi zao hawajui wajibu wala hawaoni haya hali kama uchafu ni kawaida kwao, mwananchi atajitahidi kadri ya uwezo wake lakini kama kiongozi hajali. Ndo inabidi uwe msafi kwako nje huna hila Waafrika tunataka viongozi wenye kujituma na kuchagua wafanyakazi wanaoweza kufanya kazi bila usimamizi, kujivunia kazi tukijilinganisha na wenzetu wa majuu kazi anaiheshimu hata kama ina mshahara mdogo lajini kama unaifanya kwa usanifu boss anagawa mshahara ziada.
Na yote ni maradhi ya Viongozi ufisadi, taka, foleni, umeme na rushwa chanzo ni Viongozi mpaka tutakapo pata viongozi wenye roho za kiBinaadam katika nafasi hizo. Wananchi tutaathiri kidogo sana hata kama tutajituma 100%, wanatudanganya lakini wadanganyika ni wachache kama si wengi.
 
Lakini, kwa nini tunakaa kukimbilia kulaumu Wanasiasa kwanza na si sisi wenyewe kuchukua jukumu la kujirekebisha kwanza?

Maana kila kitu sasa Mtanzania analaumu Serikali kuu, hata ile ya mtaani ameisahau.

Nilipita Ukonga siku moja, jirani na gereza, nikakuta kifusi cha takataka cha mita 8 kwa 8, kiko kando ya barabara. Nikajiuliza mkuu wa wilaya anapita hapa, mkuu wa gereza anapita hapa, wananchi wa kawaida wenye madaraka na wasio na madaraka wanapita hapa na kuuona huo uchafu. Sasa swali likaja, ni nani anayetupa hivo takataka? je kwa nini hawachimbi mashimo kutupa takataka na kuzichoma? nikajiuliza, hivi wanamsubiri nani aje kuwaondolea takataka hizo ambazo leo hii mvua ya vuli ikishuka ni Kipindupindu mtindo mmoja?
 
Rev.Kishoka,
Usinichekehse miye weee! yaani hatan wewe ulipita ukakiona ukakiacha kama wengine kisha unauliza jibu wakati mwenyewe unalo mkuu..duh! ama kweli nasikia raha tupu na vundo la Bongo!
Nitazidi kuuliza hao wananchi wataukusanya huo uchafu waulpeleke wapi?..Hivi kweli unategemea mtu wa kawaida achukue hata mkokoteni hadi tabaka Dampo, hana kazi nyingine jamani. Uchafu umeshakusanywa, umetupwa sehemu moja ni kazi ya Halmashauri ya mji kushughulikia kazi nyingine. Mimi hadi sasa hivi sikubaliani na usemi kwamba wananchi ni wachafu hata kidogo, pamoja na umaskini wao wanafagia nyumba zao za vumbi na wengi sana wanajitahidi hata kupanda michongoma na kuweka bustani katika maeneo yao..Lakini tazma amaeneo yote yanayomilikiwa na hizo halmashauri ni mashauri kweli!..
 

Mkandara,

Watu waliniona kichaa nikiokota chupa tupu za maji na kuzitupa kwenye mapipa! Siku moja pale Billicanas nje jamaa walikuwa wakipata maji yao Kilimanjaro wakaanza kuzitupa chupa, nikainama kuzikusanya nikaziweka kwenye mfuko nikaweka kwenye pipa, jamaa wakaza kuniangalia kama nimechanganyikiwa!
 
Mch Kishoka et al,

Hii mada ni tete sana.

Nashauri tuangalie mapendekezo ya Jenerali Ulimwengu hapa....yeye anasema chanzo cha matatizo yetu ni kuporomoka kwa maadili kuanzia kwenye ngazi ya familia. Mimi nakubaliana naye kwa 100%. Nashauri mikakati ya kutafuta suluhisho ianzie kwenye ngazi ya familia....soma na wewe utoe mchango wako...


 

spot on, spot on.

Katika vijiwe vyote hapa US, kila mtu anasema maboksi nayopiga hapa US yanalipa vizuri mbongo. Ukiwauliza yanalipa vipi, kila mtu anakupa dili za wizi. Tena wengine wanaosema hivyo ni members hapa JF ambao kila siku wanawasemea mbovu mafisadi. Sijawahi kukaa na mbongo na akanipa maneno ya kufanya juhudi za kubadilisha maisha ya mbongo angalau mmoja.

Hivyo inanifanya mimi kuamini kuwa tunalalamika kwa sababu hatupo kwenye nafasi, na tukipata nafasi basi tutafanya kama waliopo madarakani.
 

Nyani Ngabu umenifurahisha sana kwa kumuita Invisivbe H.N.I.C. Kusema kweli Miafrika ndivyo tulivyo is very troubling rhetoric, kwa sababu it is a naked truth. It is something which we always prove honkies that this is who we are.
Sijawahi kusikia sehemu yoyote mwizi akisifiwa, au serikali kukiri kuwa hatuwezi kuwashughulikia wahalifu. WTF. Eti na sisi tunajiita nchi. Ni kama tungekuwa better under whitemans rule, kuliko sasa ambapo hata suala la umeme ni issue. May be Dar es salaam is the only city (big village) in the world ambapo umeme unakatika. Na wezi na majambazi wanatamba kuliko wasio wezi na majambazi.\Ndivyo tulivyo
 
Yebo Yebo,
Kuna ukweli ktk maelezo ya Jenerali lakini hatuwezi kurekebisha malezi ya mtu mwingine hata kidogo na bahati mbaya hao hao ndio huja na kuwa viongozi wetu. Ukichunguza kwa makini hoja ya Ulimwengu haina solution kwa mlalahoi zaidi ya kukubali matokeo ama kuomba Mungu wazazi hawa wenye tamaa watakuja badilika, jambo ambalo haliwezekani.. Kwa hiyo tujiandae kwa vizazi vyetu kuwa katika wakati mgumu zaidi.
Kusema kweli kulingana na historia ya nchi yetu, viongozi wetu wote walitoka familia maskini, kwani baada ya ASzimioa la Arusha, familia nyingi tajiri walitupwa chini kiutawala, hivyo ni wachache sana waliokulia katika maisha ya fridge Open. Kisha basi viongozi wote hawa walipigwa msasa wa Ujamaa Kigamboni wakawa waumini wa imani hiyo ya malezi.

Binafsi naamini kabisa WaTanzania tumepitia malezi hayo ya Ujamaa na pengine kosa kubwa lililofanyika ni kuwa strictly ktk imani ya Ujamaa. Kama vile mzazi unapokuwa mkali sana kwa mwanao kuhusiana na zinaa au anasa za dunia, sasa siku akija funguliwa na kuona yanayotokea nje huingia kwa pupa na kasi ya ajabu. Mfano mdogo na mzuri ni Wasomali wanapoingia nchi hizi.

Kwa uhakika Tanzania tulipitia kipindi kigumu sana cha Ujamaa, Tanzania ilikuwa nyumba ya gate kali sasa tulipokuja kuingia Ubepari, mtumeee haramu zote zilikuwa halali, ndio haya tunayoyaona leo. Lakini cha ajabu na kile kinacho nisukuma mimi kuamini kwamba NDIVYO TULIVYO, nazitazama nchi kama Kenya, Zimbabwe, Zambia. wao walikuwa Mabepari toka enzi lakini leo hii hawana tofauti na sisi tena wao ndio wameathirika zaidi, leo hii Kenya wanachimba visima vya maji mijini, wanavaa mitumba na kadhalika...Kenya ambayo tulikuwa tukiisikia tu kikifananishwa na London. Zimbawe ndio usiseme kabisa yaani duh!

Kwa hiyo, kweli malezi yanachangia makuzi ya mtoto sana tu lakini sidhani kama kuna malezi bora kwa mtoto zaidi kuzingatia Utamaduni wa wahusika na mazingira wanayoishi. Wahindi, Wachina na hata hao Wazungu malezi yao wote wanafuata tamaduni zao zaidi ya kuchukua malezi ya kuiga..Mtoto wa kihindi ni lazima ajifunze kwanza tamaduni za Kihindi kuanzia lugha, chakula, mavazi, heshima, mawasiliano na kadhalika..All of them have their own culture hata kama kuna wageni toka nje, wao hawasahau culture zao. Wazungu na Wachina wote ni katika mfumo huo huo..

Ukirudi kwa MIAFRIKA na hasa nchi za kusini mwa Jangwa (maskini kuliko zote) sisi sote tumeziacha culture zetu..Mkerewe mimi sitaki hata kusikia wala kuzungumza kikerewe, kumwamkua kaka ama dada yangu shikamoo ati ni utumwa, kwa sababu tu mzungu kasema hivyo.

Hata Nyerere alipokuja na Ujamaa ulikuwa wa kuchonga zaidi ya kufuata culture zetu. Mpango wa kuitana Ndugu badala ya Mheshimiwa, kuanzisha vijiji vya Ujamaa ulowachanganya watu wa makabila kuondoa Ukabila pasipo kufahamu kwamba kiswahili lugha iliyokubalika haina historia ya Utamaduni nyuma yake. hatukuwa na mwongozo wa Utamaduni nyuma ya makundi yote haya ila siasa za Ujamaa ambao hata Wachina waliufuata lakini bado walitukuza culture zao. Leo hii kila mtu hapendi kuzungumza kiswahili maanake sii lugha yake, ni sawa na mtoto alozaliwa Marekani umwambie yeye ni Mtanzania atakubishia hadi kesho!

Kwa hiyo hitimisho langu ni pale tulipopoteza Utamaduni wetu, makabila yote yanafanya vizuri nchini ni yale yaliyolinda tamaduni zao ndani ya Ujamaa. Unaona Wahaya, Wachagga na Wanyakyusa hadi kesho wanalinda tamaduni zao za kiasili na wanalindana sana ukilinganisha na Wasukuma au wanyamwezi ambao bado wanatukuza kiasi tamaduni zao lakini mikoa yao imevamiwa na wageni kiasi kwamba tamaduni hizo hazionekani.. watoto wao wanakua pasipo kuziona, kupitia malezi yenye kutukuza tamaduni hizo na matokeo yake ndio unayaona..
Mkuu niamini tazama nchi zote maskini, watu wake hawana utamaduni wao kabisa na huwezi jenga values kwa kutumia siasa ama sheria za bunge pasipo kutukuza tamaduni zinazo identify jamii hiyo.. Utamaduni ndio chanzo cha mawasiliano, mshikamano na hata kuaminiana...Ni katika tamaduni hizo ndipo kipimo cha malezi bora huweza pimwa.
 

Mkandara:

Mi sioni kuwa utamaduni ndio suala linalozuia maendeleo. Na sikubaliana kabisa kusema kuwa wachagga, wanyakyusa na wahaya wanafanya vizuri kwa sababu wameshikiria utamaduni wao.

Maendeleo ya jamii yanategemea injini za maendeleo. Wanyakyusa, wachagga na wahaya wanatoka katika maeneo yanayolima kahawa. Hivyo kilimo cha kahawa ni injini za maendeleo kwa jamii hizi. Na pesa za kahawa zilitumika kusomesha watoto (diversitifaction) na kufanya mambo mengine yamezisaidia jamii zao.

Kama kushikilia utamaduni ni chanzo cha maendeleo basi waMasaai, waHazdar wangekuwa wa kwanza kuendelea.

Na kuonyesha kuwa kahawa ni injini ya maendeleo, pale Nyerere alipoanzisha mamlaka za mazao na serikali kuchukua mapato makubwa ya mazao ya biashara, wachagga, wahaya na wanyakyusa waliathrika sana. Vijana wengi wa kichagga waliishia darasa la saba na kupata ajira kwenye kazi za kusafisha viatu.

Wasukuma wana injini za maendeleo katika maeneo yao. Lakini kwa bahati mbaya zinashikiliwa na serikali. Serikali kuu iwaachie wasukuma machimbo ya dhahabu na baadaye tuangalie watafanyia nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…