Ugali wa saiti

Umenikumbusha machimboni, aisee ni nomaa sana

Kuna siku kambini yalitengwa maharage upande wa pili likasongwa nguna, mpishi mikwara mingi afu kavua shati.

Mara tukaskia oya wanangu ebu chekini hii kitu, kucheki tukaona jamaa kaibua chura kutoka kwenye maharage akiwa amevimba baada ya kuchemkia kwa muda mrefu

Jamaa akasema sasa huyu tunamuweka hapa, akamuweka pembeni afu wazee wakashuka kuufinya kama kawa
 
Camp moshi vijijini watoto wa mama hawaelewagi hizi mamboView attachment 2024609
Camp ya kishua hii mpaka kuku inapikwa

Huko machimboni nyanda za kusini ni noma, yani nguna na maharage vinaipuliwa kwa pamoja

Halafu mboga ikiwa hivyo hivyo ya moto inatiwa pilipili kichaa za kutosha halafu maji ya kunywa yanawekwa hatua 50 kutoka eneo mnalolia msosi.

Siku ya kwanza nilipokula nilishindwa kuendana na kasi ya masela kulingana na msosi ulivyokuwa wa moto, jamaa mmoja akaniambia kabla ya kula huu ugali ulitakiwa ukafanye mazoezi ya kushika moto kwanza
 
De propera
 
Chura ni nyama tamu, kwanini hamkumla?
 
Urikuwa ritoto ramama muraa!
 
Duh umenikumbusha mwaka jana morogoro wakati tunajenga hospital ya halimashauri ya mvuha dadeki ulikua unasongwa ugali dagaa na pilipili ya mbilimbi iyo speed siisahau

Umenifanya nikumbuke zile hustle asee mungu mkubwa now afadhali nipo kwenye msitari wa ndoto zangu
 
Urikuwa ritoto ramama muraa!
Ngoja kwanza, uwaone hawa kwanza walau upate picha ya hao vibopa

Sasa hawa unao waona hapa kwa wale masela hawa bado ni ma beginner na wakikaa vibaya hata matonge matano wanaweza wasifikishe
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…