Uganda: Watakaonunua chapati tano kukamatwa

Uganda: Watakaonunua chapati tano kukamatwa

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2014
Posts
4,298
Reaction score
7,612
Ukistaajabu ya Musa utashanga ya mengi katika hali ya kushangaza polisi kwenye wilaya ya Moroto kaskazini mwa Uganda wametangaza kukamata mtu yoyote atakayekutwa akinunua chapati zaidi ya tano kwa mara moja.

Chanzo cha kamata kamata hiyo ni kutokana wakazi wengi wa wilayani humo kutumika kupeleka chakula kwa baadhi ya wezi wa mifugo kwenye wilaya hiyo na kuwaficha majumbani mwao.

Akizungumza na wanahabari msemaji wa jeshi la polisi wilayani humo Micheal Longole, amesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya wizi wilayani humo.

“Kwanzia sasa tutakamata na kumhoji mtu yoyote atakaye nunua chapati zaidi ya tano kwa lengo la kujua ni kwa nini ana nunua kiasi hicho cha chapati, tumepata taarifa kuwa watu wengi wananunua na kupeleka kwa waharifu waliojificha maporini” amesema Longole.
 
Yaani serikali au Polisi wameshindwa wamakuja na mbinu za kijinga ndio hapo mzungu anamcheka Muafrika kwa kuona hajaendelea kwa kifupi ni Ushamba .Kamata wizi wa mifugo wapeleke katika uwanja wa mpira wa Moroto waite wanakijiji wote wale wizi wainamishe wapige risasi za mkundu uone kama atatokea mwizi tena hapo Moroto lazima saa nyingine utoe sharia ngumu hiyo sheria ya chapati ni Ujinga mno.Hata mafisadi kwa hapa bongo shria kama hii ya kupiga marisasi ingekuwa safi sana pamoja na wizi mbele ya Hadhara.
 
Tunashangaa ya Uganda wakati sisi tuliongeza kodi kwenye mafuta ya taa ili wezi wasichakachue mpaka kesho mafuta ya taa bei inatofautiana kidogo na petrol ukiuliza miaka yote hiyo pesa iliyopatikana bure tuu imefanya nini jibu hupati ndio wanaleta tozo na mataka taka mengine ya kulipia jengo kwa njia ya Luku..
 
Ukistaajabu ya Musa utashanga ya mengi katika hali ya kushangaza polisi kwenye wilaya ya Moroto kaskazini mwa Uganda wametangaza kukamata mtu yoyote atakayekutwa akinunua chapati zaidi ya tano kwa mara moja.

Chanzo cha kamata kamata hiyo ni kutokana wakazi wengi wa wilayani humo kutumika kupeleka chakula kwa baadhi ya wezi wa mifugo kwenye wilaya hiyo na kuwaficha majumbani mwao.

Akizungumza na wanahabari msemaji wa jeshi la polisi wilayani humo Micheal Longole, amesema wamefikia hatua hiyo kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya wizi wilayani humo.

“Kwanzia sasa tutakamata na kumhoji mtu yoyote atakaye nunua chapati zaidi ya tano kwa lengo la kujua ni kwa nini ana nunua kiasi hicho cha chapati, tumepata taarifa kuwa watu wengi wananunua na kupeleka kwa waharifu waliojificha maporini” amesema Longole.
Wabane Unga, Je wakipika kwao??????????????
 
Tunashangaa ya Uganda wakati sisi tuliongeza kodi kwenye mafuta ya taa ili wezi wasichakachue mpaka kesho mafuta ya taa bei inatofautiana kidogo na petrol ukiuliza miaka yote hiyo pesa iliyopatikana bure tuu imefanya nini jibu hupati ndio wanaleta tozo na mataka taka mengine ya kulipia jengo kwa njia ya Luku..
Mbombo ngafu

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
Tunashangaa ya Uganda wakati sisi tuliongeza kodi kwenye mafuta ya taa ili wezi wasichakachue mpaka kesho mafuta ya taa bei inatofautiana kidogo na petrol ukiuliza miaka yote hiyo pesa iliyopatikana bure tuu imefanya nini jibu hupati ndio wanaleta tozo na mataka taka mengine ya kulipia jengo kwa njia ya Luku..
Wee jamaa wewe. Ebu agizia chochote hapo dukani kwa mnaijeria Gauteng ntapitia kulipia.
 
Uwezo wao wa kufikiri ndio umegotea hapo sasa wafanye nini🙄
 
Majirani wanamambo ya ajabu sana...

Chanjo lazima wao, lock down wao... mpaka chapati tano ni kosa...
 
Ukinunua unga wa ngano na kupika chapati 20 nyumbani kwako poa tu.
 
Shauri yao watakosa pisi za Afghanistan bora wale mbili tu
 
Huku Tozo huko Chapati tano, dah, ngozi nyeusi wacha iendelee kutawaliwa tu.
 
Sasa ni kwanini msifanyenmsako huko maporini badala ya kufanya msako kwenye maduka ya chapati?
 
Back
Top Bottom