Uganda: Waziri asema watu masikini hawatokwenda mbinguni

Uganda: Waziri asema watu masikini hawatokwenda mbinguni

Mtapenda

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2011
Posts
1,115
Reaction score
2,063
Waziri wa Uganda akinukuliwa

"Ikiwa hutumii akili alizokupa Mwenyezi Mungu, usimlaumu unaposalia kuwa maskini. Jitahidi kuushinda umaskini kwa sababu kuwa tajiri ni utukufu,"

Gazeti la New Vision la Uganda linamnukuu kiongozi mmoja mkuu nchini Uganda akisema kuwa

"maskini hawataenda mbinguni kwa sababu wanamtukana Mungu kwa njia ya maombolezo na shutuma kila siku".

Waziri wa Masuala ya ndani Kahinda Otafiire aliripotiwa kutoa maoni hayo katika hafla ya shule huko Kyenjojo, magharibi mwa Uganda, huku akiwaambia wanafunzi kuwa kufanya kazi kwa bidii ndio dawa ya umaskini.

Ukosefu wa ajira kwa vijana ni mkubwa nchini Uganda, ambayo ina moja ya idadi ya watu changa zaidi duniani ikiwa na 75% ya raia chini ya umri wa miaka 30.

Unazungumziaje hili ?

Je anapingana na biblia inayosema ni vigumu tajiri kwenda mbinguni kuliko ngamia kupenya kwenye tundu la sindano!?

Source: BBC Swahili Instagram

1653386776839.jpg
20220518_130006.jpg
 
Walioshiba hawawajui wenye njaa. Binaadam tunakufuru sana kupitia Mdomo.

Yeye ni nani hata atoe maelekezo ya kuingia Mbinguni.

Uganda kuanzia Rais wao mpaka viongozi wengine ni Majinga sana na unaweza kuthibitisha hili kupitia matamko yao.

Limtokalo mtu ni lile lilo Ndani yake = Moyoni Mwake & Akilini Mwake.
 
Ni vigumu tajiri kuingia mbinguni kama ngamia kupenya kwenye tundu la sindano. Kinyume chake ni rahisi kwa maskini kwenda mbinguni kama kula urojo tu
 
Walioshiba hawawajui wenye njaa. Binaadam tunakufuru sana kupitia Mdomo.

Yeye ni nani hata atoe maelekezo ya kuingia Mbinguni.

Uganda kuanzia Rais wao mpaka viongozi wengine ni Majinga sana na unaweza kuthibitisha hili kupitia matamko yao.

Limtokalo mtu ni lile lilo Ndani yake = Moyoni Mwake & Akilini Mwake.
Ata hivyo masikini wanachuki sanaa kwa matajiri... Pia wanalawama sanaa kwa mwenyezi Mungu...

Ukiangalia uongozi wa mwendazake ndio ungeona chuki za masikini kwa matajiri

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
 
Binadamu wa kiafrika wakipata cheo na pesa ni wa kuwaogopa sana. Viroporopo mno. Wanajiona wao ndio wao. wasengenyaji etc

Sasa hapo kakalia daraja la kuwavusha wenzie badala ya kuliweka sawa na kuwapa wenzie njia ya kuwavusha amebaki kakaa na kuanza kuwasakama
 
Binanadamu wa kiafrika wakipata cheo na pesa ni wa kuwaogopa sana. Viroporopo mno. Wanajiona wao ndio wao. wasengenyaji etc

Sasa hapo kakalia daraja la kuwavusha wenzie badala ya kuliweka sawa na kuwapa wenzie njia ya kuwavusha amebaki kakaa na kuanza kuwasakama
Wewe mtizameni hata Uso wake; Yaani umejaa kama Futari ya Magimbi Full Unene.
 
Ni vigumu tajiri kuingia mbinguni kama ngamia kupenya kwenye tundu la sindano. Kinyume chake ni rahisi kwa maskini kwenda mbinguni kama kula urojo tu
Umasikini ndo chanzo cha uovu wote
 
Back
Top Bottom