fungi
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 2,539
- 4,672
Mahakama ya kikatiba nchini Uganda imefutilia mbali sheria hiyo ambayo ilisababisha mataifa ya Magharibi kuinyima Uganda msaada
Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda
Mahakama ya kikatiba nchini Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ambayo ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Kadhalika sheria hiyo ilizua gumzo sana sio tu Uganda bali kote duniani ambapo mataifa ya Magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.
Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja
Vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, tayari vilikuwa vimeharamishwa Uganda , lakini sheria hiyo mpya pia iliharamisha hatua zozote za kueneza mapenzi ya jinsia moja na wakati huu hata kuwajumuisha wanawake wasagaji kama sehemu ya wapenzi wa jinsia moja.
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
SOURCE: BBC
Wanaume wanaounga mkono mapenzi ya jinsia moja Uganda
Mahakama ya kikatiba nchini Uganda imefutilia mbali sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja ambayo ilisababisha mataifa ya magharibi kuinyima msaada.
Kadhalika sheria hiyo ilizua gumzo sana sio tu Uganda bali kote duniani ambapo mataifa ya Magharibi yalilazimika kuingilia kati.
Mahakama ilisema kuwa mswada huo kabla ya kuidhinishwa kuwa sheria ulipitishwa na wabunge ambao idadi yao haikutosha kupitisha mswada na kwa hivyo ni kinyume na sheria.
Baadhi ya waandamanaji waliounga mkono serikali kwa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja
Vitendo vya mapenzi ya jinsia moja, tayari vilikuwa vimeharamishwa Uganda , lakini sheria hiyo mpya pia iliharamisha hatua zozote za kueneza mapenzi ya jinsia moja na wakati huu hata kuwajumuisha wanawake wasagaji kama sehemu ya wapenzi wa jinsia moja.
Mataifa kadhaa ya Magharibi yamesitisha msaada kwa Uganda hasa baada ya sheria hiyo mpya kupitishwa.
Mashoga wapinga sheria Uganda
11 Machi, 2014 - Saa 14:00 GMT
Wanaharakati wa wapenzi wa jinsia moja, mawakili na wansiasa wamewasilisha kesi mahakamani nchini Uganda kupinga sheria mpya dhidi ya mapenzi ya jinsia moja nchini humo.
Wanaharakati hao, wanasema kuwa sheria hiyo inakiuka katiba ya Uganda na kuendeleza ubaguzi na kukandamiza uhuru wa kujieleza.
Sheria hiyo ilitiwa saini na Rais Yoweri Museveni mwezi jana na imelaaniwa vikali na jamii ya kimataifa.
Rais wa Marekani Barack Obama ameitaja sheria hiyo kama hatua ya ukandamizaji kwa waganda na nchi kadhaa tayari zimetishia kuinyima Uganda msaada.
Mwandishi wa BBC mjini Kampala anasema kuwa itachukua miezi kadhaa kabla ya kusikilizwa.
Marekani yaiwekea vikwazo Uganda
20 Juni, 2014 - Saa 07:12 GMT
Marekani imeiwekea Uganda vikwazo kwa kupitisha sheria zinazopinga mapenzi ya jinsi moja katika taifa hilo la Mashariki ya Afrika.
Afisa wa mahusiano anayesimamia maswala ya usalama katika ikulu ya whitehouse Caitlin Hayden anasema kupitia kwa barua kwa wanahabari kuwa sheria hiyo iliyopitishwa na bunge la Uganda mwezi Februari inakiuka haki za binadamu.
Vikwazo hivyo vitajumuishwa marufuku ya wanaharakati waliopigia debe sheria hiyo kupitishwa kutoingia Marekani.
Miradi itakayoathirika na marufuku hiyo ni pamoja na ushirikiano na polisi wa Uganda Wizara ya Afya.
Aidha msaada kwa miradi iliyoanzishwa kwa usaidizi wa marekani pia utapunguzwa mbali na kufutiliwa mbali kwa mazoezi ya kijeshi kati ya majeshi ya uganda na yale ya Marekani.
Sheria hiyo inaharamisha uhusiano baina ya watu wa jinsia moja na wale watakaopatikana wanaweza kuhukumiwa kifungo cha maisha jela.
Hii ndiyo hatua ya hivi karibuni iliyochukuliwa na Marekani katika ajenda yake ya kupinga sheria hiyo mpya nchini Uganda.
Juma lililopita Seneta mmoja kutoka Marekani ,Kirsten Gillibrand alilalmikia vikali uteuzi wa waziri wa maswala ya kigeni wa Uganda Sam Kutesa kuchaguliwa kuwa rais wa Umoja wa Mataifa kutokana na kuwa anatokea Uganda.
Watu 9000 walikuwa wametia sahihi pendekezo la kuitaka Umoja wa Mataifa kumng'oa kitini bw Kutesa aliyechaguliwa licha ya kampeini hiyo.
Wanaharakati wa wapenzi wa jinsia moja wameenda mahakamani wakitaka sheria hiyo iondolewe lakini inatarajiwa kupingwa kwani rais Yoweri Museveni aliupitisha maksudi kudhihirishia wafuasi wake kuwa yu huru kutokana na shinikizo kutoka kwa mataifa ya ughaibuni .
Punde baada ya kupitishia kwa sheria hiyo mpya benki kuu ya dunia iliahirisha utoaji wa mkopo wa dola milioni 90 ambazo zilikuwa zinapaswa kutumika kuimarisha sekta ya Afya nchini Uganda .
Mataifa mengi tu ikiwemo Denmark, Norway, Uholanzi na Sweden zote zimekatiza msaada kwa taifa hilo la Afrika Mashariki.
SOURCE: BBC

