Ugomvi wa ndugu 2,waliojariwa ofisi moja

Ugomvi wa ndugu 2,waliojariwa ofisi moja

fimboyaukwaju

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2020
Posts
2,977
Reaction score
3,798
Hawa ndugu wakiumu,waliozaliwa na mama mmoja ila baba tofauti,wote ni madereva na asili yao ni wahindi.Maisha yao wanayoishi ni kama waafrika kabisa,kwa kila kitu,kula,kuvaa,mademu ni kama wafanyavyo wabantu.Wameajiriwa na tajiri mmoja,sasa bosi wao akawaambia kuwa wajiandae kwa safari ya kenya na uganda maana ni madereva wake.Hao ndugu hawasemeshani kabisa na safari nzima hawaongei,bosi wao alikuwa anawashangaa sana,akiwauliza nyie mna ugomvi gani hawajibu.Huyo bosi wao ni rafiki yangu sasa na ndiye alikuwa akinipa huu mkasa na alikuwa anashangaa sana.Njia nzima hao ndugu ni kugombana na mpaka leo hii hao ndugu wana umri mkubwa hawaongei kabisa.Sijui ni kipi kikisababisha,wadau mshakutana na hali kama hii,ndugu hawaongei kwa takriban miaka zaidi ya 20
 
Pesa na madaraka !
IMG_0801.jpeg
 
wadau mshakutana na hali kama hii,ndugu hawaongei kwa takriban miaka zaidi ya 20
Kawaida sana

Nitakupa mkasa kidogo, mfano mna eneo la familia let say Eka 10 tu ikafika kipindi familia ikaamua liuzwe na kila mmoja kati ya wanafamilia apate mgao wa Eka 1, ikatokea ndugu mmoja kati yenu akapiga Eka 5 zote peke yake hivi huyo wewe utamchukuliaje? Ugomvi wowote wa ndugu unaouona jua kuna ndugu mmoja ana tatizo la kukandamiza ndugu wengine na kujifikiria yeye tu na sio vinginevyo
 
Ndugu umesema vizuri sana
Kawaida sana

Nitakupa mkasa kidogo, mfano mna eneo la familia let say Eka 10 tu ikafika kipindi familia ikaamua liuzwe na kila mmoja kati ya wanafamilia apate mgao wa Eka 1, ikatokea ndugu mmoja kati yenu akapiga Eka 5 zote peke yake hivi huyo wewe utamchukuliaje? Ugomvi wowote wa ndugu unaouona jua kuna ndugu mmoja ana tatizo la kukandamiza ndugu wengine na kujifikiria yeye tu na sio vinginevyo
 
Hawa ndugu wakiumu,waliozaliwa na mama mmoja ila baba tofauti,wote ni madereva na asili yao ni wahindi.Maisha yao wanayoishi ni kama waafrika kabisa,kwa kila kitu,kula,kuvaa,mademu ni kama wafanyavyo wabantu.Wameajiriwa na tajiri mmoja,sasa bosi wao akawaambia kuwa wajiandae kwa safari ya kenya na uganda maana ni madereva wake.Hao ndugu hawasemeshani kabisa na safari nzima hawaongei,bosi wao alikuwa anawashangaa sana,akiwauliza nyie mna ugomvi gani hawajibu.Huyo bosi wao ni rafiki yangu sasa na ndiye alikuwa akinipa huu mkasa na alikuwa anashangaa sana.Njia nzima hao ndugu ni kugombana na mpaka leo hii hao ndugu wana umri mkubwa hawaongei kabisa.Sijui ni kipi kikisababisha,wadau mshakutana na hali kama hii,ndugu hawaongei kwa takriban miaka zaidi ya 20
Ipo mkuu ni Dunia hii!
 
Itakuwa mmoja kati yao hasa mkubwa kiumri anammaindi mwenzie sababu baba yake kamgongea mama yake.
 
Hawa ndugu wakiumu,waliozaliwa na mama mmoja ila baba tofauti,wote ni madereva na asili yao ni wahindi.Maisha yao wanayoishi ni kama waafrika kabisa,kwa kila kitu,kula,kuvaa,mademu ni kama wafanyavyo wabantu.Wameajiriwa na tajiri mmoja,sasa bosi wao akawaambia kuwa wajiandae kwa safari ya kenya na uganda maana ni madereva wake.Hao ndugu hawasemeshani kabisa na safari nzima hawaongei,bosi wao alikuwa anawashangaa sana,akiwauliza nyie mna ugomvi gani hawajibu.Huyo bosi wao ni rafiki yangu sasa na ndiye alikuwa akinipa huu mkasa na alikuwa anashangaa sana.Njia nzima hao ndugu ni kugombana na mpaka leo hii hao ndugu wana umri mkubwa hawaongei kabisa.Sijui ni kipi kikisababisha,wadau mshakutana na hali kama hii,ndugu hawaongei kwa takriban miaka zaidi ya 20


Ushasema baba tofauti, hata kama mama ni mmoja, damu ni tofauti, inatokea sana hiyo
 
Back
Top Bottom