Ugomvi wangu na Ali Kiba ni "personal"

Ugomvi wangu na Ali Kiba ni "personal"

Hivi karibuni, kuna rafiki yangu mmoja alipewa invitation sehemu. Akanicheck nimpe kampani. Tukaenda wote.

Ilikuwa ni house party ya familia fulani ya kiarabu. Naweza kusema ni wale waarabu waliopinda na kunyongorota kabisa maana wanatafuna mirungi, gomba na kukata kilaji kama hawana akili nzuri.

Kitu kimoja ambacho kiliniboa ni playlist yao ambayo ilikuwa inasindikizia ile party. Walijaza nyimbo za Ali Kiba za kiarabu na Marekani kiasi.. Tatizo langu lilikuwa hapo kwa Ally.

Kuna binti ambaye alikuwa ndio anacontrol muziki tulikuwa close na tunapiga story sana vile ni mchangamfu. Uvumilivu uliponishinda, nikamwambia naomba hizo nyimbo za Kiba uzipotezee bhana. Akanishangaa!

Akasema wewe unataka zipi maana humu ndani kila mtu hampendi Diamond/WCB, wote ni team Kiba. Ikawa zamu yangu kushangaa!

Ikabidi tu nimwambie ukweli. Ugomvi wangu na Ali Kiba sio ushabiki wa u-team. Ni binafsi sana. Nikamsimulia kilichotokea kati yangu na msanii huyo takribani miaka 10 iliyopita.

Ni mapenzi. Alitembea na msichana wangu ambaye alikuwa shabiki wake namba moja. Kiukweli ule ushabiki wake hata mimi ulikuwa unanitia wivu sana ila sikujua kama zingefanyika jitihada za kutokea yaliyotokea. Nilirahisisha mno nikajisahau kuwa sote tupo ndani ya Jiji moja na chochote kinawezekana.

Ili ombi langu lifanyiwe kazi, nikamtania kidogo kwa kumsifia kuwa msichana mwenyewe alikuwa shombe shombe kama wewe japo umemzidi uzuri na akili kidogo. Tukacheka na nyimbo za Ali Kiba hazikupigwa tena mpaka tulipoondoka.

NB: Ali Kiba ni msanii mzuri na ana kipaji cha kweli. Sidhani kama kuna msanii anamfikia hasa kwa vocals. Sina tatizo nae kimuziki، ila siwezi kumshabikia kwa sababu nitakuwa natakatisha kile alichonifanyia miaka ile.

Kwa ujumla, nashauri wasanii na watu maarufu wawe na nidhamu. Mitaani kuna visasi vingi.
vip mtaalam bado upo na uyo manzi au 🤔🤔
 
Utamu kapewa mtu mwingine uchungu unakushika wewe daaah....
 
Interest,
Mwenye kisu kikubwa ndiye ula nyama siku hizi kila mtu ana mtu kilichobaki ni mwenye nguvu kumnyanganya asiye na nguvu. Halafu usimlaumu alikiba na kumchukia mlaumu demu wako kwa kutokuwa na msimamo tena mshukuru alikiba kwa kukufanya umjue demu wako ni mwanamke wa aina gani ungekuja kumuoa anngekuja kibosile akakugongea.
 
Mimi nikiwa na mahusiano na binti nikaona ana ndoto za kuwa video vixen na anakuwa inspired na akina tunda yani najiandaa kisaikolojia na kutoka ndukiii
Hakuwa hata na ndoto hizo. Basi tu nadhani mazingira yalimuexpose huko!
 
Yanii Hapa Ndipo Ulipozingua, Alikiba Hana Vocal Kama Unavomsifia, Alikiba Ni Mbana Pua Tu Kama Wabana Pua Wengine-- Hivi Unajua Vocal Wewe???

Bongo Wasanii Wenye Vocal Ni Kama Christian Bella Hivii Au Ukienda Nchi Jirani Apo Utakutana Na Sauti Soul

NB: Ali Kiba ni msanii mzuri na ana kipaji cha kweli. Sidhani kama kuna msanii anamfikia hasa kwa vocals. Sina tatizo nae kimuziki، ila siwezi kumshabikia kwa sababu nitakuwa natakatisha kile alichonifanyia miaka ile.




Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kweli duniani kila mtu ana lake moyoni siku mioyo ikifunuka patakua hapatoshi
 
Back
Top Bottom