Ugonjwa huu umenimalizia tikiti nifanye nini kuepuka nao

Ugonjwa huu umenimalizia tikiti nifanye nini kuepuka nao

Pole sana mkuu, huo ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu aitwaye kwa jina la kienyeji "dondoa".

Mdudu huyo hutoboa matunda yakiwa machanga na ana sumu ambapo akishatoboa hukojolea hiyo sumu na kusababisha tunda lioze kwenye sehemu iliyotobolewa au kuozesha tunda zima.

Kama halikuoza lote, litaoza sehemu iliyotobolewa na hiyo sehemu husinyaa na sehemu zingine huendelea kukua hivyo tunda huwa na mkunjo flani.

Wadudu hawa huishi kwenye miti hususani mikuyu, miembe nk.

Wadudu hawa ni waharibifu sana kwenye matunda hivyo dawa za sumu kali na zenye harufu huwakimbiza shambani mfano Selecrone ni dawa mojawapo unapaka kwenye pamba au vipande vya godoro na kusimika shambani kila mahali.

Pia kuna mitego ya kuwanasa ambayo hutundikwa at least mitego 6 kwa ekari moja na kila mtego ni shs 5000.

Hiyo mitego ipo kama chocolate inawa attract hao wadudu wanapoingia tu hukutana na sumu na kufa hapo hapo.

Wauzaji wa hiyo mitego nawafahamu waliopo Arusha.


Pole sana mkuu
Mkuu uko vizuri

Naomba ufafanuzi kwenye hili

Mimi nimeanza kilimo cha nyanya ila ile sehemu nayotaka kupandikiza miche kuna miti ya mikorosho miwili, Je inaweza kuleta shida yoyote ya magonjwa au wadudu kwa nyanya zangu?

Ahsante.
 
Mkuu uko vizuri

Naomba ufafanuzi kwenye hili

Mimi nimeanza kilimo cha nyanya ila ile sehemu nayotaka kupandikiza miche kuna miti ya mikorosho miwili, Je inaweza kuleta shida yoyote ya magonjwa au wadudu kwa nyanya zangu?

Ahsante.
Asante na karibu sana mkuu. Kwa miche ya nyanya sidhani kama kuna shida sana unless kingekuwa kipindi cha msimu wa baridi ndo miche ingeweza kudhurika.

Ila hakikisha kivuli cyo kizito sana hadi kupelekea uwepo wa giza. Kivuli kikiwa kikubwa na mwanga ukawa hauifikii miche husababisha miche kuwa marefu na yenye udhaifu.

Ili kuua wadudu kama funza na fungus, nyunyuzia miche yako dawa za sumu.
 
Kuna dawa inaitwa Guguset ukipata inakausha kila jani isipokuwa miti
mkuu nashkuru sana,,km hutojali ntakuchek pm niwe nakupa updates mana mm sio mzoefu kwnye hii tasnia so naenda kwa msaada wa materials na maelekezo ya wadau nisije kosea step
 
View attachment 656254
Hivyo ndivyo tikiti inavyokuwa
Huu si ugonjwa wala wadudu ni ukosefu wa Calcium katika tunda kitaalam tunauita BLOSSOM END ROT. Weka mbolea za CAN mara tu maua au matunda yanapoanza kutoka na baada ya hapo hakikisha unakuwa na ratiba maalum ya kumwagilia isiyobadilika badilika hadi wiki moja ya mwisho kabla ya kuvuna uache kumwagilia.
 
Je ukichunguza huweza kuona tobo?
je baada ya kuanza kuoza huoza lote au vinginevyo?
kwa msaada zaidi tembelea hapa CHALAJI COMPANY LIMITED: UFAHAMU UGONJWA WA KUOZA VITAKO(BLOSSOM END ROT) KWA MATIKITI NA NYANYA.
Huu ni ugonjwa gani mkuu? na dawa gani nitumie? umetokea kwenye baadhi ya miche ambayo ina wik 4 ss
89d7a4205a64ae08444a28774b131aab.jpg
 
Back
Top Bottom