Ugonjwa wa Acid Reflux uwe janga la kitaifa

Ugonjwa wa Acid Reflux uwe janga la kitaifa

Kuna ugonjwa mwingine una itwa GASTRITIS.

Ebwana eeeh ni balaaa upo kama vidonda vya tumbo ila nahisi huu ni balaa zaidi ya hivyo vidonda vya tumbo.

Mwenyezi Mungu atusaidie tuu.
 
Mimi ninapambana nacho zaidi ya 5 years now
Pole sana kiongozi, ulifanikiwa kupata matibabu au bado tatizo linakusumbua?

Mimi nafahamu dawa za mimea, ukipenda naweza kukuandalia.

Kiujumla Kwa yoyote mwenye tatizo la PEPTIC ULCERS, GERD, GASTRITIS dawa zake nazifahamu.

Naweza kumuandalia atakaependa. Utalipia tu 10,000Tshs kwa kuwa nitatumia muda na fedha kuandaa dawa hizo.

Aghalabu hiyo dawa utakayolipia 10,000Tshs huwa inatosheleza kwa matibabu mpaka kupona, mara chache kuhitajika dozi ya pili isipokuwa kwa tatizo lenye athari za muda mrefu.

Nakutakia afya njema.
 
Ewaaaaaaa saaafi sana, Nina mwaka maybe wa nane au kumi napambana nayo but Mungu anasaidia. Nimeweza kufanya yafuatato:
1. Nakula mapema sana kati ya saa nane na saa kumi Jioni, kwahio Nina Milo miwili tu breakfast na late lunch, baaasi!

2. Usiku nakunywa juice fresh ya parachichi na embe lililoiva sana, ukipata ambalo halijaiva imekula kwako

3. Nakula papai, hii inaisaidia saaana sanna Kwa upande wangu Mimi huyu ni mkombozi, hata Sasa nimetoka kula papai
4. Nakunywa maji ya kutosha usiku
5. Nikiona nimeharibu ratiba yangu either nikiwa Safarini au pengine nikiwa sherehe au kampani na jamaa mkala late kidogo BASI kwenye Bag langu la PC sikosi Magnesium (hizi natafuna mnooooo, juzi nimenunua magnesium nzuri sana, ikabidi ninunue za buku nne, Hadi muuzaji akashangaa.

Matokeo yake
1. Nalala bila kupata heartburn
2. Sipaliwi Tena usingizini
3. Sikoromi Tena usiku
4. Napata choo bila kutumia nguvu

Changamoto
1. Kuna siku kama Leo nimekula mapema zaidi, saa nane kasoro, muda huu nimekula papai na juice, yaani night itakua ndefu kuanzia saa Tisa hivi......

Hii ndio niliyofanya lakini pia ukipata TANGO ni nzuri kama utalila bila kuweka vitu vingine, yaani ule tango kama TANGO, haya ni Kwa upande wangu
Piga Tikiti Mzee utakuja nishukuru
 
Hello Wana JF, great thinker.

Ndugu zanguni naomba tu serikali ya Namhuri ya Muungano wa Tanzania wautambue huu ugonjwa wa Acid reflux kama janga la kitaifa kwani huu ugonjwa ukikushika huwezi kufanya Kazi kabisa kwani kifua kinabana.

Hauwezi kutembea haraka, viungo karibia vyote huwa vinachoka sana, unaweza kufikiri una tatizo la moyo au pumu.

Yaani we acha tuu, naomba madaktari wetu kupitia hili jukwaa wawe wanatoa somo kuhusu huu ugonjwa Kabla ya mgonjwa hajaanza kukimbilia Muhimbili au India na vipimo vingi vya Moyo kumbe tatizo ni acid reflux.

Asante sana waheshimiwa madaktari, waliowahi kuugua huu ugonjwa na wakapona na wanaoendelea kupambana nao waje na mawazo yao please.

Serikali haiwezi kutatua hili tatizo kwasababu ni utamaduni mbaya ndiyo chanzo. Sasa mtu anakula saa moja kabla ya kwenda kulala ni lazima atakuwa na acid maana acid kazi yake kubwa ni kuyeyusha chakula sasa lazima utapata acid. Kama hauli vyakula vyenye alkaline utapata acid

Haya ni matatizo lakini kwa wengi ni utamaduni wa kula ndiyo chanzo
 
Ni miaka mitatu napambana nayo mkuu , usiombe ikukamate boss , utaona kijijini kwenu kuchungu
Pole sana kiongozi, pamoja na kuzingatia mtindo wa maisha rafiki kama baadhi ya wadau walivyochangia, unaweza pia kutumia vitu hivi ni vizuri sana kwa tatizo la ACID REFLUX/KIUNGULIA:

i) Manjano - Unatumia unga wake kijiko kimoja cha chai mara mbili kwa siku kwenye chai au maji ya vuguvugu.

Ukiweza kupata pilipili manga ni bora zaidi unanyunyizia kidogo sana (0.4g), inasaidia manjano kuweza kufyonzwa na mwili kwa ufanisi zaidi.

N.B : Kama unatumia dawa nyingine yoyote ni vizuri kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia na (i) hapo juu.

ii) Kabichi - Unaisaga na kuitumia kama juisi, glasi moja (~ 100ml) asubuhi kabla ya kula chochote.
Kama ni tatizo ni kubwa sana unaweza kutumia kabla ya chakula cha mchana pia.

Manjano na Kabichi pia hutumika kwa tatizo la vidonda vya tumbo na gastritis.

Nakutakia matibabu mema.
 
Tumekosa taarifa sahihi ,kuna unajua kiingereza naomba utazame hii video nimetoa YouTube. Huyu anaitwa DK Berg ni marekani anaongelea jinsi ya kutibu acid reflux na sio ku-manage symptoms,I hope itawasaidia wengi. Pia soma na comments za ushuhuda wa watu waliopona kupitia kwake (YouTube comments).

Hii imeeleweka sana nahitaji kujaribu pia naona kwenye comment watu wanatoa ushuhuda mzuri juu ya matumizi ya apple cider vinegar pamoja na Bataine hcl hapa ndo nilipoachwa. msaada kwa tanzania nazipataje hizi material
 
Back
Top Bottom