Ugonjwa wa Kuwashwa Mwili Umeenea: Naomba Msaada Wenu

Ugonjwa wa Kuwashwa Mwili Umeenea: Naomba Msaada Wenu

Manjovial

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2015
Posts
590
Reaction score
1,125
Habari,

Yapata mwezi sasa nimekuwa nikikumbwa na tatizo la kuwashwa mwili kama nimemwagiwa upupu, hasa mida ya saa tatu usiku ambapo mambo yanakuwa mabaya zaidi na najikuna vibaya mno. Mwanzo, mtoto wangu mmoja alianza na hali hii, kisha ikaenea kwa watoto wote. Walipokuwa wanashindwa kulala sababu ya kujikuna, sikuwa naelewa kama walikuwa wanapitia kipindi kigumu kiasi hiki.

Baada ya kupewa tiba ya siku 14, watoto walipona, lakini mmoja ameanza tena kupata vipele vibaya mikononi na miguuni. Nachanganyikiwa kuelewa ni ugonjwa gani huu. Na si sisi tu, inaonekana kama umeenea kimya kimya. Leo nikiwa kwenye duka la dawa, nilikutana na mtu mwingine aliyekuwa akiomba dawa itakayomsaidia yeye na familia yake, ambao pia wanapitia hali kama yangu. Pia, dada yangu ambaye yupo Shinyanga naye analalamika hivyo hivyo kuwa wamepatwa na ugonjwa huu wa kuwashwa mwili.

Wakuu, kuna yeyote anayepitia changamoto kama hii? Mimi nipo Ruvuma na si msimu wa joto. Cha ajabu ni kuwa hata walio katika hali ya hewa ya joto wanalalamika kama mimi. Hii ni nini? Wataalam wa mambo wanasema ni maambukizi ya fungus kwenye damu, ingawa sijui kama nilisikia vizuri au nilikuwa busy na gitaa.

MSAADA HATA WA MAWAZO UTASAIDIA. Nilipewa Ethromaisini lakini bado nakesha nikijikuna. Mpaka sasa nimejaribu dozi kadhaa bila mafanikio, kuna unafuu kidogo lakini tatizo linarejea palepale.
 
Ni ishu ya kawaida tu mkuu sio ya kuogopa Mpaka kukupa stress jaribu kuizingatia matandiko, nguo na usafi Kwa ujumla.. Pia cheki maji pengine Yana shida.. Onana na watalaam akupe dawa
 
Habari,

Yapata mwezi sasa nimekuwa nikikumbwa na tatizo la kuwashwa mwili kama nimemwagiwa upupu, hasa mida ya saa tatu usiku ambapo mambo yanakuwa mabaya zaidi na najikuna vibaya mno. Mwanzo, mtoto wangu mmoja alianza na hali hii, kisha ikaenea kwa watoto wote. Walipokuwa wanashindwa kulala sababu ya kujikuna, sikuwa naelewa kama walikuwa wanapitia kipindi kigumu kiasi hiki.

Baada ya kupewa tiba ya siku 14, watoto walipona, lakini mmoja ameanza tena kupata vipele vibaya mikononi na miguuni. Nachanganyikiwa kuelewa ni ugonjwa gani huu. Na si sisi tu, inaonekana kama umeenea kimya kimya. Leo nikiwa kwenye duka la dawa, nilikutana na mtu mwingine aliyekuwa akiomba dawa itakayomsaidia yeye na familia yake, ambao pia wanapitia hali kama yangu. Pia, dada yangu ambaye yupo Shinyanga naye analalamika hivyo hivyo kuwa wamepatwa na ugonjwa huu wa kuwashwa mwili.

Wakuu, kuna yeyote anayepitia changamoto kama hii? Mimi nipo Ruvuma na si msimu wa joto. Cha ajabu ni kuwa hata walio katika hali ya hewa ya joto wanalalamika kama mimi. Hii ni nini? Wataalam wa mambo wanasema ni maambukizi ya fungus kwenye damu, ingawa sijui kama nilisikia vizuri au nilikuwa busy na gitaa.

MSAADA HATA WA MAWAZO UTASAIDIA. Nilipewa Ethromaisini lakini bado nakesha nikijikuna. Mpaka sasa nimejaribu dozi kadhaa bila mafanikio, kuna unafuu kidogo lakini tatizo linarejea palepale.
Umetembelewa na walozi! Au ndo nyie mnaopinga hakuna ulozi!
 
Duh juzikati nilipatwa na shida hii. Nikaacha vitu vyote vipya nilivyotumia wiki hiyo chakula sabuni na mafuta ya kujipaka. Bahati mbaya nilisahau mafuta ya nywele. Nikaendelea kujipaka mwili unawasha na vipele na usoni nakuwa ka Mzee USO unajikunja. Duh kumbe shida mafuta ya flani niliyokuwa najipaka usoni. Nikitumia temosl sabuni nashangaa Sasa shida imepungua kabisa.
Hebu badili vitu vipya ambavyo hukua ukitumia mwanzo
 
Umetembelewa na walozi! Au ndo nyie mnaopinga hakuna ulozi!
Mkuu nimepitia hapa jukwaani nimeona kuna mtu aliwahi lalamika na hali hii hivi hivi ...mimi sio mshirikina na siamin katika hilo sijalogwa aisee ni ugonjwa kama magonjwa mengine usiombe yakupate
 
Nilikula kitimoto mkoa fulani
Niliumwa huo ugonjwa
NIliwashwa kama chizi
Dawa nilochomwa sindano
Muwasho ukakata hapo hapo
Mapele in 3 days yaliisha.....

Hao ni parasites kuna chakula hakiko sawa au hakipikwi vizuri
 
Habari,

Yapata mwezi sasa nimekuwa nikikumbwa na tatizo la kuwashwa mwili kama nimemwagiwa upupu, hasa mida ya saa tatu usiku ambapo mambo yanakuwa mabaya zaidi na najikuna vibaya mno. Mwanzo, mtoto wangu mmoja alianza na hali hii, kisha ikaenea kwa watoto wote. Walipokuwa wanashindwa kulala sababu ya kujikuna, sikuwa naelewa kama walikuwa wanapitia kipindi kigumu kiasi hiki.

Baada ya kupewa tiba ya siku 14, watoto walipona, lakini mmoja ameanza tena kupata vipele vibaya mikononi na miguuni. Nachanganyikiwa kuelewa ni ugonjwa gani huu. Na si sisi tu, inaonekana kama umeenea kimya kimya. Leo nikiwa kwenye duka la dawa, nilikutana na mtu mwingine aliyekuwa akiomba dawa itakayomsaidia yeye na familia yake, ambao pia wanapitia hali kama yangu. Pia, dada yangu ambaye yupo Shinyanga naye analalamika hivyo hivyo kuwa wamepatwa na ugonjwa huu wa kuwashwa mwili.

Wakuu, kuna yeyote anayepitia changamoto kama hii? Mimi nipo Ruvuma na si msimu wa joto. Cha ajabu ni kuwa hata walio katika hali ya hewa ya joto wanalalamika kama mimi. Hii ni nini? Wataalam wa mambo wanasema ni maambukizi ya fungus kwenye damu, ingawa sijui kama nilisikia vizuri au nilikuwa busy na gitaa.

MSAADA HATA WA MAWAZO UTASAIDIA. Nilipewa Ethromaisini lakini bado nakesha nikijikuna. Mpaka sasa nimejaribu dozi kadhaa bila mafanikio, kuna unafuu kidogo lakini tatizo linarejea palepale.

Nenda kapime isije kuwa damu inachanganyana na nyongo.
 
Nenda kapime isije kuwa damu inachanganyana na nyongo.
Nmecheka aisee walisema ni mchafuko wa damu..hasa hawa watu wa pharmacy walisema ss hivi wanapata case nyingi za aina hiyo ..kiswahili tunasema ni kaupepo flan hivi kamepita
 
Nilikula kitimoto mkoa fulani
Niliumwa huo ugonjwa
NIliwashwa kama chizi
Dawa nilochomwa sindano
Muwasho ukakata hapo hapo
Mapele in 3 days yaliisha.....

Hao ni parasites kuna chakula hakiko sawa au hakipikwi vizuri
bado ukila kitimoto unawashwa?
 
Nmecheka aisee walisema ni mchafuko wa damu..hasa hawa watu wa pharmacy walisema ss hivi wanapata case nyingi za aina hiyo ..kiswahili tunasema ni kaupepo flan hivi kamepita
Umecheka nini sasa? Hujasoma kuwa anaumwa na tunajaribu kumwambia sababu ambazo zinaweza kuwa ugonjwa?
 
Back
Top Bottom