Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

FAHAMU KUHUSU VIDONDA VYA TUMBO
( Abdominal Ulcers)

Hili limekuwa janga kubwa kwa watanzania walio wengi kibaya zaidi wengi wao hawajui suluisho sahihi liko wapi na kuishia kubaki sugu kwenye miili yao na kufikiri labda ni magonjwa ya maisha au kurithi. Hivo jamii kubwa mpaka leo hii hawajui suluisho hasa la VIDONDA vya tumbo ingawa ni hatari sana kwa afya.
Usisahau kuwa zaidi ya asilimia 75 magonjwa yote ya kiafya huanzia tumboni sasa ungana nami hapa uweze kujua ninichakufanya.

Vidonda vya tumbo maana yake nini........

Hii ni hali ya kuwa na vidonda au michubuko, majeraha ndani ya ule ukuta laini wa tumbo lako la chakula (membrane)

NINI HUSABABISHA VIDONDA HIVI
Imekuwa ikitafsiriwa na kila mtu kulingana na anavyodhania huko kwenye jamii zetu kuhusu tatizo hili sasa leo ningependa ujue hali halisi na chanzo hasa cha tatizo hili. Yako mambo mawili makubwa ambayo huleta vidonda vya tumbo.
1.Maambukizi ya bacteria aitwayo H.pylori pamoja na

2.Utumiaji madawa ya kupunguza maumivu (NSADs) kama panadol, ibuprofen, diclofenac sasa kama huwa unatumia dawa hizi halafu tayari ulikua na vidonda vya tumbo either ulikua unajijua au bado juwa wazi unaandaa mazingira ya hatari zaidi tumboni kwako kwa sababu dawa hizi zitazidi kuharibu mfumo wako wote wa digestive system (utumbo na ukuta wa tumbo la chakula) sasa je utajuaje kama wewe ni mmoja ya watu wenye tatizo hili ungana nami kujua ni zipi dalili za vidonda vya tumbo.

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
-Maumivu ya tumbo yanayo choma -hapa tumbo huwa linaunguza sana hasa katikati lakini pia karibu na kifua juu kabisa ya kitofu ikiambatana na kiungulia

-Tumbo kujaa gesi hili limekuwa tatizo la watu wengi sana kiasi kwamba watu huzani kuwa ni kawaida lakini kumbe siyo kweli pia huambatana na kusumbuka choo kubwa kuipata kwa shida

-Kutapika hapa waliofikia hatua mbaya hufikia kipindi mpaka kutapika damu sasa dalili hiyo ujue wazi kuwa vidonda vyako vimefikia mahala pabaya. Sasa wengi hufikiri labda vidonda vya tumbo siyo tatizo kubwa na hii ni kwasababu hawajui madhara hasa nini kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo

MADHARA
1.kutoboka utumbo mdogo kama uliwai kuona au kuambiwa mtu alipoteza uhai kwasabu ya tatizo hili basi ujue kuwa utumbo ulikwisha athiriwa pia na hii ni kwasababu ya acidi kutumika ndivyo sivyo ndani ya mwili baada ya kupata vidonda vya tumbo
-Kupungua uzito na hii ni kwasababu ya vyakula kushindwa kunyonywa ipasavyo ndani ya mwili ndio maana choo kubwa pia inakuwa nyeusi au ya giza ,wako watasema unamawazo au kuathirika kumbe shida ni Vidonda vya tumbo/digestive system health

-Ni rahisi kupata cansa ya utumbo kwasababu ya kuharibika kwa zile seli.

Suluisho

Imekuwa mazowea sasa watu kuskia maumivu hayo na kuendelea kunywa dawa za maumivu bilakujua kuwa wanazidi kuhatarisha zaidi kumbe ni bora hata ukatumia mboga za majani zote, na kuacha kutumia kahawa kwakua ina caffeine lakini pia machungwa na zabibu zina acidi nyingi hivo kama kupata unafuu zingatia hayo

Suluhisho la kudumu....

Kulingana na uhalisia wa haya madonda ya tumbo yanavyosumbua na watu kutafuta ufumbuzi kwa kubahatisha bahatisha tumekuandalia virutubisho ambavyo vingefaa kutumika kila siku ili kuakikisha unarudisha afya imara na kuepukana na haya madawa ya kikemikali pamoja na mitishamba kwani vyakula ndivyo nguzo sahihi kwa afya yako.

Mwenye kuitaji kuimarisha afya yake wasiliana nasi kwa namba 0788599960
FB_IMG_1542489043686.jpeg
FB_IMG_1541344563718.jpeg
FB_IMG_1542487418050.jpeg
IMG-20181104-WA0147.jpeg
 
Kwakweli nasumbuka sana wakuu

Pole sana ndugu,
Hebu jaribu hii tiba mbadala, kuna mtu ilishamsaidia halalamiki now.
Chemsha Supu ya kuku kienyeji, kwenye supu ongeza maziwa ya kutosha ili supu iwe rojorojo kwa maziwa, ongeza viazi mviringo kunogesha hiyo supu. Itumie asubuhi mchana na jioni, ila kama mambo ya kazi angalau asubuhi na jioni, kunywa bakuli moja tu kabla hujaendelea na milo mingine kawaida, rudia tiba hiyo kwa siku 3-5, then njoo na majibu hapa.
Ieleweke tiba inayoweza mfaa A si lazima imnufaishe B, hata hospital ipo hivyo.
 
Jaman wanajf naombeni msaada wa dawa ya vidonda vya tumbo,mana nimetumia dawa nyingi tu ila zinatuliza maumivu tu kwa mda fulan,So kwa yeyote yule anayefahamu dawa inayoweza kuponya kabsa naomba anisaidie plizz
 
asanteee kwa maelezo
mi nilipima kwa kipimo cha Endoscopy but sijajua sasa vimesababishwa na nini? na doctor hakunipa maelezo zaid,alinambia tu ninavidonda vya tumbo na nikapewa dawa tu za kutuliza maumivu
 
asanteee kwa maelezo
mi nilipima kwa kipimo cha Endoscopy but sijajua sasa vimesababishwa na nini? na doctor hakunipa maelezo zaid,alinambia tu ninavidonda vya tumbo na nikapewa dawa tu za kutuliza maumivu
Iko kipimo cha endoscopy bei gani mkuu
 
Back
Top Bottom