Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Mabandiko mengine sio mabandiko ya kitoto!, ukijiona huelewi, we jipitie tuu!.
Angalizo la Alama ya Kuuliza "?".
Mimi mwenzenu jameni, nimewahi kuitwa mahali na kufikishwa mbele ya kamati fulani kwa kutuhumiwa nimesema statement fulani!, kumbe masikini mimi, sikutoa statement, niliuliza tuu!. Aliyenituhumu, hakuiona alama ya kuuliza, hivyo naomba kutoa angalizo la alama ya kuuliza?, bandiko hili sio la statement ni bandiko la swali.
Bandiko hili ni moja ya mabandiko yangu ya dhana dhanifu kuwa kuna uwezekano na huyu naye pia anadanganywa na amedanganyika!.
Leo nimeisikia tena dhana ya uhaini, ikitajwa mahali!, the voices behind inaniambia anadanganywa na amedanganyika!.
Hii issue ya uhaini nimewahi sio tuu kuizungumzia humu, bali nimeiandikia makala
Ijue Katiba ya JMT kwa Jicho la Mtunga Katiba: Watanzania Tusishabikie Uhaini. Hukuna Uhaini wa Kauli na Maneno, Uhaini ni Mipango na Matendo
Humo nilisema
Nimesema hili sio bandiko la watoto kwasababu natafuta the motives behind such lies ili kumjulisha mtu wetu inawezekana kuwa anadanganywa na watu wake, hivyo kama mtu ukidanganywa na watu wako unaowaaminia bila wewe kujua unadanganywa, ukidanganyika sio kosa lako wewe
unaodanganywa,; kwasababu hao wanaokudanganya ni watu wako unao waaminia, hivyo kudanganyika ni halali yako!, ila kosa ni la hao wanao kudanganya, na siku ukiujua ukweli kuwa ulikuwa unadanganywa, ndipo utaelewa kuwa ni kweli hapa duniani kuna watu na viatu, wengine ukiwaona machoni ni kama watu, lakini mioyoni ni mashetani wakubwa wamwaga damu za watu!.
Hii sio mara ya kwanza kwa hao watu kufanya vitendo na madudu ya ajabu ajabu kisha kudanganya mamlaka juu ku justify udhaoimu wao.
Enzi za Nyerere, alikataa na akawatundika msalabani baadhi yao na kuwafagia toka juu mpaka chini, ndio maana enzi za JPM, tulishauri TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
Nyerere aligoma kudanganywa, Mwinyi akadanganywa, Mkapa akadanganywa kwenye ubinafsishaji. Jakaya akadanganywa sana tuu kwenye rasilimali zetu. Mkapa na Kikwete Walidanganywa na Wakadanganyika!, Magufuli Anadanganywa!, Jee Atadanganyika?
JPM mwanzo aligoma kudanganywa na kudanganyika kwenye rasilimali zetu, akakaza, akabana na kukaba, tukauliza humu ataweza? Zita Act Retroactively? Tutavunja Mikataba Yote Iliyopo? Can we Stand? Do we have the Guts? kiukweli JPM alikuwa ni chuma, alikaza, vyuma vikabana, akabana akabana mwisho akaachia!
Mimi ni mtu wa mastori stori, kuna watu wanapenda mastori mastori na wana muda wa kusoma makitu marefu, na kuna wako wako busy hawana time na mastori, wao wanataka vitu short and clear. Wale wa mastori tuendelee, wale wa short and clear, just jump to the conclusion
Baadhi ya matukio ya ajabu ajabu kisha kuvalishwa uongo
Inawezekana yule Mzee wa watu (Mungu amuweke mahala pema peponi), kwa vile ni mstaafu wa jeshi, anawezekana anahesabika ndiye the strategist, hivyo kuhesabika ni mtu hatari he had to go!. Watekelezaji wakajua tukiharibu sura kwa acid hatatambulika tena!. Mwili umeokotwa Ununio Jumamosi asubuhi, ni polisi wameuchukua na kuu dump mortuary ya hospital ya Mwananyamala. Jumamosi mchana polisi haikutoa taarifa yoyote kuokota mwili wowote, bali Kamanda Musiime alitangaza Jeshi la Polisi kumtafuta huyo Mzee!. Jumamosi usiku ndio ndugu wanautambua mwili!.
Kufuatia kelele nyingi, CinC akatoa amri ya kufanyika uchunguzi wa kina!. Sasa ili kujikosha na kujisafisha, ikabidi itengenezwe script ya movie ya uhaini, ili ku justify kwa CinC why ameshughulikiwa!, wale mnao subiria taarifa ya uchunguzi wa tukio hilo, endeleeni kusubiria, kama ni wasiojulikana, taarifa itatolewa lakini kama ni 'wasiojulikana', tutasubiri sana kama taarifa ya tukio la pyu pyu za Tundu Lissu!.
Binadamu wote ni sawa, thamani ya uhai wa mtu na roho ya mtu, inalingana, huwezi kumtoa mtu uhai kivile, baada ya kelele za kitaifa na kimataifa, unaamua kutunga script ya uhaini!, na kweli jana CinC kakasirika kweli kweli!, yeye hajui kuwa ni script!.
Huu ni ushuhuda wangu jinsi PT wanavyo bambikia watu kesi mbaya, hawachelewi kubambikia watu uhaini!.
The bottom line ni polisi wetu wana bambika watu kesi mbaya hadi za mauaji!, hivyo hawezi kushindwa kubambika uhaini!.
Hivyo mtu ukihisiwa tuu wewe ni hatari kwa usalama wa the status quo, unabambikiwa kesi, unapotezwa, na sasa hadi uhaini unazungumzwa!.
Kwa vile mimi ni Tomaso, siamini kabisa dhana ya uhaini mpaka tuthibitishiwe!.
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali
Mabandiko mengine sio mabandiko ya kitoto!, ukijiona huelewi, we jipitie tuu!.
Angalizo la Alama ya Kuuliza "?".
Mimi mwenzenu jameni, nimewahi kuitwa mahali na kufikishwa mbele ya kamati fulani kwa kutuhumiwa nimesema statement fulani!, kumbe masikini mimi, sikutoa statement, niliuliza tuu!. Aliyenituhumu, hakuiona alama ya kuuliza, hivyo naomba kutoa angalizo la alama ya kuuliza?, bandiko hili sio la statement ni bandiko la swali.
Bandiko hili ni moja ya mabandiko yangu ya dhana dhanifu kuwa kuna uwezekano na huyu naye pia anadanganywa na amedanganyika!.
Leo nimeisikia tena dhana ya uhaini, ikitajwa mahali!, the voices behind inaniambia anadanganywa na amedanganyika!.
Hii issue ya uhaini nimewahi sio tuu kuizungumzia humu, bali nimeiandikia makala
Humo nilisema
Uhaini Tanzania..., My God!. Kuna Uwezekano Anadanganywa na Kadanganyika?. Mimi ni Tomaso, I Don't Believe This at All!. Sitatizwi na Uongo Wao, Natatizwa na The Motives Behind Such Lies!.Wanabodi,
Kufuatia tishio la matamshi yenye viashiria vya uhaini dhidi ya serikali ya JMT kwa baadhi ya watu, na watu hao kushikiliwa na vyombo vya dola, waneibuka watu, mashirika, wanaharakati kupigia kelele kuna kesi ya uhaini, na hadi baadhi ya taasisi za kimataifa kutaka kuingilia kati mambo yetu ya ndani!, hivyo kufuatia mwandishi wa makala hizi kuwa pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, naomba kuitumia makala ya leo, kuelimisha umma kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu kwa jicho la mtunga katiba.
Uhaini ni nini? Uhaini umetajwa kwenye sura ya Saba kifungu cha 39 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, yaani penal code kinasema Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano, kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais.
Kwa mujibu wa sheria tuliofundishwa darasani, uhaini ni vitendo na sio kauli ni uchochezi!. Kwa vile mpaka sasa hakuna mashitaka yoyote ya uhaini yaliyofunguliwa katika Mahakama yoyote, nawaombeni Watanzania wenzangu tusishabikie uzushi wa uhaini, hili sio jambo la kheri hata kidogo.
Vivyo hivyo kwenye jinai ya uhaini, sio kila matamshi ya uhaini ni uhaini, ili kuwepo kwa jinai ya uhaini, lazima kuwepo kwa zile sifa kuu mbili, actus reus na mens rea ya kupanga kufanya uhaini. Kitendo cha mtu ameghafilika tuu na hoja za Club House, akaanza kuhororoja kutoa matamshi ya kupindua serikali, haimaanishi ni uhaini wa kupindua kweli serikali, lakini matamshi hayo yanaweza kuwa ni matamshi ya uchochezi hivyo kusababisha watu wapange kweli kupindua serikali, lakini matamshi tuu kama matamshi bila ya kuwepo means rea ya kupindua serikali, watu hao watakuwa wamefanya kosa la sedition na sio treason.
Kitendo cha watu haswa wanaharakati kupiga kelele uhaini, kuiongopesha dunia na kufanya nchi yetu kuangaziwa vibaya kimataifa, wakati hadi ninapoandika hapa, hakuna kesi yoyote ya uhaini iliyofunguliwa popote, hivyo huku kushabikia na kushadadia uhaini sio jambo jema, ni kutaka kumchafulia bure huyu Mama wa watu ile sifa yake kuu ya kuliponya taifa!
Paskali
Nimesema hili sio bandiko la watoto kwasababu natafuta the motives behind such lies ili kumjulisha mtu wetu inawezekana kuwa anadanganywa na watu wake, hivyo kama mtu ukidanganywa na watu wako unaowaaminia bila wewe kujua unadanganywa, ukidanganyika sio kosa lako wewe
unaodanganywa,; kwasababu hao wanaokudanganya ni watu wako unao waaminia, hivyo kudanganyika ni halali yako!, ila kosa ni la hao wanao kudanganya, na siku ukiujua ukweli kuwa ulikuwa unadanganywa, ndipo utaelewa kuwa ni kweli hapa duniani kuna watu na viatu, wengine ukiwaona machoni ni kama watu, lakini mioyoni ni mashetani wakubwa wamwaga damu za watu!.
Hii sio mara ya kwanza kwa hao watu kufanya vitendo na madudu ya ajabu ajabu kisha kudanganya mamlaka juu ku justify udhaoimu wao.
Enzi za Nyerere, alikataa na akawatundika msalabani baadhi yao na kuwafagia toka juu mpaka chini, ndio maana enzi za JPM, tulishauri TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
Nyerere aligoma kudanganywa, Mwinyi akadanganywa, Mkapa akadanganywa kwenye ubinafsishaji. Jakaya akadanganywa sana tuu kwenye rasilimali zetu. Mkapa na Kikwete Walidanganywa na Wakadanganyika!, Magufuli Anadanganywa!, Jee Atadanganyika?
JPM mwanzo aligoma kudanganywa na kudanganyika kwenye rasilimali zetu, akakaza, akabana na kukaba, tukauliza humu ataweza? Zita Act Retroactively? Tutavunja Mikataba Yote Iliyopo? Can we Stand? Do we have the Guts? kiukweli JPM alikuwa ni chuma, alikaza, vyuma vikabana, akabana akabana mwisho akaachia!
Mimi ni mtu wa mastori stori, kuna watu wanapenda mastori mastori na wana muda wa kusoma makitu marefu, na kuna wako wako busy hawana time na mastori, wao wanataka vitu short and clear. Wale wa mastori tuendelee, wale wa short and clear, just jump to the conclusion
Baadhi ya matukio ya ajabu ajabu kisha kuvalishwa uongo
Huu uhaini unaoelezwa sasa, ni uhaini wa aina gani?!.Aliyekuwa DGIS, Iran Kombe alishughulikiwa kwasababu fulani!, wakadanganya ilikuwa ni kwa bahati mbaya tuu kwa kushukiwa kuwa ni jambazi!. Assassins wali m trail all the way from Dar Moshi just to accomplish the mission!.
Zile pyu pyu za Tundu Lissu was just a mission impossible kwasababu tuu Mungu alikuwa hajapanga, tukaelezwa ni watu wasiojulikana, sisi wa jicho la tatu tunajua sio wasiojulikana bali ni 'wasiojulikana', ndio maana Tundu Lissu mpaka leo hajachukuliwa maelezo, na kitendo cha kumrudishia evidence, ina maana failing la uchaguzi limefugwa!.
Wale wafabiasha wa 4 wa madini walioshughulikiwa na Zombe na Bageni, waliisha singiziwa ni majambazi!.
Ben Saanane, sisi wana jf wote tunajua sababu.
Kulitokea tukio Arusha, Ijumaa usiku, wakawakamata vijana 4 mmoja mmoja toka nyumbani kwake, huku ni wazima wa afya wanatembea wenyewe!, wakamataji wakajitambulisha ni polisi na kunyesha arrest warrant. Kesho yake Jumamosi ndugu zao wamewapelekea chakula kituo kikuu cha polisi, wote 4 walikuwa wazima na wakala. Jioni wanawaletea chakula cha usiku, wanaambiwa wamehamishwa kituo!. Jumapili asubuhi Jeshi la Polisi likaripoti kuokota miili 4 ya majambazi yaliyouliwa na watu wenye hasira "Mob justice" kwenda kuiangalia ile miili ni ya wale vijana wanne walikamatwa Ijumaa!.
Kwenye ule uhaini wa 1982, ring leader ni komandoo wa JWTZ, Martin Tamimu, alihesabika ni mtu hatari hivyo akashughulikiwa mapema!.
Watu wanaonekana ni watu hatari, wanashughuliwa kikamilifu!.
Inawezekana yule Mzee wa watu (Mungu amuweke mahala pema peponi), kwa vile ni mstaafu wa jeshi, anawezekana anahesabika ndiye the strategist, hivyo kuhesabika ni mtu hatari he had to go!. Watekelezaji wakajua tukiharibu sura kwa acid hatatambulika tena!. Mwili umeokotwa Ununio Jumamosi asubuhi, ni polisi wameuchukua na kuu dump mortuary ya hospital ya Mwananyamala. Jumamosi mchana polisi haikutoa taarifa yoyote kuokota mwili wowote, bali Kamanda Musiime alitangaza Jeshi la Polisi kumtafuta huyo Mzee!. Jumamosi usiku ndio ndugu wanautambua mwili!.
Kufuatia kelele nyingi, CinC akatoa amri ya kufanyika uchunguzi wa kina!. Sasa ili kujikosha na kujisafisha, ikabidi itengenezwe script ya movie ya uhaini, ili ku justify kwa CinC why ameshughulikiwa!, wale mnao subiria taarifa ya uchunguzi wa tukio hilo, endeleeni kusubiria, kama ni wasiojulikana, taarifa itatolewa lakini kama ni 'wasiojulikana', tutasubiri sana kama taarifa ya tukio la pyu pyu za Tundu Lissu!.
Binadamu wote ni sawa, thamani ya uhai wa mtu na roho ya mtu, inalingana, huwezi kumtoa mtu uhai kivile, baada ya kelele za kitaifa na kimataifa, unaamua kutunga script ya uhaini!, na kweli jana CinC kakasirika kweli kweli!, yeye hajui kuwa ni script!.
Huu ni ushuhuda wangu jinsi PT wanavyo bambikia watu kesi mbaya, hawachelewi kubambikia watu uhaini!.
ConclusionKijana wangu baada ya kuingia chuo kikuu nikamnunulia ka usafiri ka kutumia. Kijana ni like father like son, starehe, pombe na yale mambo yetu yale!.
Siku ya siku kazitwikwa za kutosha si kachukua room uswazi!, asubuhi anaamka akaikuta gari juu ya mawe, kila kinachofunguka kimesombwa!. Gari iligeuka kopo!. Akaja home kuripoti nikamshauri, kwanza akaripoti polisi, kisha aende kwenye used kuuliza kama mzigo umeishaingia sokoni.
Akaripoti polisi naomba nisikitaje kituo tukaanza kufuatana!. Kisha akaingia sokoni, akaukuta mzigo wote complete umeshushwa dukani.
Bei aliotajiwa ni karibu sawa na kununua gari nyingine!. Nikamshauri tununue vile vya msingi, tairi, starter, power windows, alternator, na vile vya ziada tutavimalizia tukioata pesa, ila abitolee advance ili visiuzwe!. Dogo akachukua fungu akaondoka.
Kule njiani akapata change of heart, akaamua akaripoti polisi.
Wakaondoka na mtego wa polisi mpaka duka la spear, akalipia vitu vikatolewa polisi wakavamia na kumdaka muuzaji!.
Muuzaji ni kijana tuu, akautwa mwenye duka, akadakwa, akaonyeshe waliomletea mzigo, wakadakwa jumla ni vijana 6! .
Dogo akasema yeye hataki kesi, anachotaka ni vifaa vyake tuu, gari yake irudi barabarani. Polisi wakamgomea, wakamwambia this is a polisi case!.
Akaambiwa ajiandae kuwakariri sura, ili kesi ikianza awatambue!. Walipoletwa dogo alitoka machozi jinsi walivyo vurugwa!.
Akapewa karatasi asaini maelezo yake, dogo akasaini bila kuyasoma !.
Kesi ilipoanza ndipo dogo akajua amesaini nini, wamepewa kesi ya armed robbery hukumu yake ni kifungo cha miaka 30!.
Wazazi wa hao vijana wakanitafuta, principal witness ni Kijana wangu!. Kiukweli dogo alikuwa ana feel very guilty, kwanini Ali ripoti wakati nimempatia fedha za kununua hivyo vifaa!. Ndipo nikagundua hawa watoto wetu sio tuu tuna share blood ya baba na mama, ni tunashere mpaka tabia, mimi ni spender mama yake ni stringy!, anasema eti aliona uchungu kulipia pesa kununua vifaa vyake vile vile vilivyo ibiwa!.
Wazazi wale walisema walioiba hivyo vifaa ni vibaka, hao wote waliokamatwa ni madali tuu, yule dogo wa dukani ameletewa tuu!.
Nikakubaliana nao japo gari la dogo limekuwa vandalised ni theft tuu na sio armed robbery!. Nikakubali kuwasaidia.
Hatua ya kwanza ni mimi kumpeleka dogo kituo cha polisi na kuripoti kwa Mkuu wa kituo kuwa dogo hakujua amesaini nini, hivyo akiyakana maelezo atalichafua Jeshi la Polisi.
Nikamuona mpepelezi nikamwambia kwa nini ameandika maelezo ya uongo?. Akijijibu kwa jeuri huo ndio utendaji wa jeshi la Polisi ili kuwakomesha vibaka unawapiga kesi za armed robbery!. Akasema na dogo akiyakataa maelezo yake mahamani, tunamuunganisha!.
Hatua ya pili nikaenda Mahakamani na kuzungumza na hakimu anayesikiliza, akasema wako kwenye committal procedures to establish prima facies. Mwenye mamlaka ya kufanya kitu ni DPP.
Nikaenda ofisini kwa DPP na kuonana na State Attorney wa hiyo kesi, Mungu bariki nikamkuta ni class mate wangu LL.B UDSM, akanieleza ukweli wa kila kitu na nini cha kufanya ni kupenyeza tuu rupia kila kona!.
Kwanza nilimuondosha dogo nchini, kisha nikawaeleza Wazazi wenzangu cha kufanya, ni nyoosha tuu mkono kushughulikia penye uzia, penyeza rupia.
The bottom line ni polisi wetu wana bambika watu kesi mbaya hadi za mauaji!, hivyo hawezi kushindwa kubambika uhaini!.
Hivyo mtu ukihisiwa tuu wewe ni hatari kwa usalama wa the status quo, unabambikiwa kesi, unapotezwa, na sasa hadi uhaini unazungumzwa!.
Kwa vile mimi ni Tomaso, siamini kabisa dhana ya uhaini mpaka tuthibitishiwe!.
Mungu Ibariki Tanzania
Paskali