Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
WANACHAMA WA CHAMA KIPYA CHA SIASA WAMEKUJA KUHAKIKIWA NA MSAJILI WA VYAMA ARNAUTOGLO HALL 1993
Asubuhi na mapema tulikuwa tumeshafika Ukumbi wa Arnautoglo tumekuja kuhakikiwa kwa ajili ya chama chetu kipya cha siasa.
Ukumbi huu una historia kubwa sana katika siasa za kudai uhuru wa Tanganyika na katika historia ya Julius Nyerere.
Tarehe 17 April 1953 kwenye ukumbi huu ndipo Nyerere alikabidhiwa chama cha TAA baada ya ''kumshinda'' Abdul Sykes katika uchaguzi wa kugombea nafasi ya President wa TAA.
Wanachama kutoka sehemu tofauti za Dar-es-Salaam kuanzia Buguruni Kwa Mnyamani, Manzese Uzuri, Tandika, Temeke, Mbagala tumefika tumejikusanya nje ya ukumbi.
Maofisa wa Ofisi ya Msajili wamefika jua limepanda kidogo wametukuta tunawasubiri.
Niko pembeni na camera yangu naangalia yote yaliyoko pale.
Kwa mbali nikamuona Mzee Lumelezi anapita na shughuli zake.
Ukoo wa Lumelezi ni ukoo maarufu sana Dar-es-Salaam.
Mzee Lumelezi, Mzee Mavemba, Ally Sykes hawa wote mchezo mmoja na baba yangu na shule yao Al Jamiatul Islamiyya Muslim School Mwalimu Mkuu Sheikh Juma Mwindadi.
Nikamkimbilia kumwamkia.
Akaitikia salamu yangu lakini nikahisi kama vile anajiuliza hapa pana nini?
Sikusubiri aniulize nikamwambia, "Baba tumesajili chama cha siasa leo tunahakikiwa."
Siku hizo kuwa wewe si mwanachama wa CCM ilionekana kama usaliti vile.
Sasa mimi namtangazia hali ya hatari.
Niliona uso wa mzee wangu ukiporomoka kama vile kusema, "Mtoto ana kiranga huyu."
Mzee Lumelezi kainamisha kichwa chini hasemi kitu. Tukaagana.
Lakini Mzee Lumelezi si mjinga kayaona yote kwa macho yake. Kawaona waliotutangulia sisi na ndiyo wao na kashuhudia yote yaliyowafika.
Alikuwa kastaafu kazi Dar es Salaam City Council. Hawakupata chochote TANU ilichowaahidi.
Watoto wao wamesoma sana darasa la la 12 lakini kawaida wanamaliza darasa la saba ndiyo mwisho wao.
Alikuwa kwa ule ukimya wake ananiambia, "Tumeshindwa sisi mtaweza nyie?"
Maofisa wa Msajili wa Vyama Vya Siasa walikuwa hawajaona watu sampuli yetu.
Kwanza tuliokuwa pale umasikini wetu ulionekana dhahir haukujificha.
Nguo zetu zilitutangaza vizuri sina haja ya kusema mengine ila moja.
Sote wanachama tuliokuja kuhakikiwa tulikuwa Waislam watupu.
Nimekuwekeeni picha mfaidi kwani picha inasema maneno 1000 na picha inaonyesha kile jicho kiliona.
Maofisa wa Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa kutuangalia wakawa tayari wameshakasirika.
Nyuso zao wamezikunja hawana tabasamu.
Leo naangalia nyuma nacheka na nashangazwa na ule ujasiri wetu kuwa sisi masikini ya Mungu tunasajili chama kije kushindana na Chama cha Mapinduzi, chama tajiri kilichokuwa na kila kitu achilia mbali kuwa kina serikali.
Kisa cha Daud na Jalut.
Jalut anajivuna kwa nguvu zake na uwezo wake wa kumuua kila aliyethubutu kukabiliananae kwenye uwanja wa mapambano.
Daud alipokuwa anakwenda kumkabili Jalut aliomba dua Allah amthibitishie miguu yake ardhini amkabili Jalut.
Chama chetu kilinyimwa usajili.
Lakini huo haukuwa mwisho wetu.
Tuliyokuja kufanya si tu yalimstaajabisha Mzee Lumelezi bali hata sisi wenyewe.
Nimeweka na picha ya mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Ghandhi Hindu Mandal mwaka wa 1955.
Fananisha picha hii na picha yetu.
Asubuhi na mapema tulikuwa tumeshafika Ukumbi wa Arnautoglo tumekuja kuhakikiwa kwa ajili ya chama chetu kipya cha siasa.
Ukumbi huu una historia kubwa sana katika siasa za kudai uhuru wa Tanganyika na katika historia ya Julius Nyerere.
Tarehe 17 April 1953 kwenye ukumbi huu ndipo Nyerere alikabidhiwa chama cha TAA baada ya ''kumshinda'' Abdul Sykes katika uchaguzi wa kugombea nafasi ya President wa TAA.
Wanachama kutoka sehemu tofauti za Dar-es-Salaam kuanzia Buguruni Kwa Mnyamani, Manzese Uzuri, Tandika, Temeke, Mbagala tumefika tumejikusanya nje ya ukumbi.
Maofisa wa Ofisi ya Msajili wamefika jua limepanda kidogo wametukuta tunawasubiri.
Niko pembeni na camera yangu naangalia yote yaliyoko pale.
Kwa mbali nikamuona Mzee Lumelezi anapita na shughuli zake.
Ukoo wa Lumelezi ni ukoo maarufu sana Dar-es-Salaam.
Mzee Lumelezi, Mzee Mavemba, Ally Sykes hawa wote mchezo mmoja na baba yangu na shule yao Al Jamiatul Islamiyya Muslim School Mwalimu Mkuu Sheikh Juma Mwindadi.
Nikamkimbilia kumwamkia.
Akaitikia salamu yangu lakini nikahisi kama vile anajiuliza hapa pana nini?
Sikusubiri aniulize nikamwambia, "Baba tumesajili chama cha siasa leo tunahakikiwa."
Siku hizo kuwa wewe si mwanachama wa CCM ilionekana kama usaliti vile.
Sasa mimi namtangazia hali ya hatari.
Niliona uso wa mzee wangu ukiporomoka kama vile kusema, "Mtoto ana kiranga huyu."
Mzee Lumelezi kainamisha kichwa chini hasemi kitu. Tukaagana.
Lakini Mzee Lumelezi si mjinga kayaona yote kwa macho yake. Kawaona waliotutangulia sisi na ndiyo wao na kashuhudia yote yaliyowafika.
Alikuwa kastaafu kazi Dar es Salaam City Council. Hawakupata chochote TANU ilichowaahidi.
Watoto wao wamesoma sana darasa la la 12 lakini kawaida wanamaliza darasa la saba ndiyo mwisho wao.
Alikuwa kwa ule ukimya wake ananiambia, "Tumeshindwa sisi mtaweza nyie?"
Maofisa wa Msajili wa Vyama Vya Siasa walikuwa hawajaona watu sampuli yetu.
Kwanza tuliokuwa pale umasikini wetu ulionekana dhahir haukujificha.
Nguo zetu zilitutangaza vizuri sina haja ya kusema mengine ila moja.
Sote wanachama tuliokuja kuhakikiwa tulikuwa Waislam watupu.
Nimekuwekeeni picha mfaidi kwani picha inasema maneno 1000 na picha inaonyesha kile jicho kiliona.
Maofisa wa Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa kutuangalia wakawa tayari wameshakasirika.
Nyuso zao wamezikunja hawana tabasamu.
Leo naangalia nyuma nacheka na nashangazwa na ule ujasiri wetu kuwa sisi masikini ya Mungu tunasajili chama kije kushindana na Chama cha Mapinduzi, chama tajiri kilichokuwa na kila kitu achilia mbali kuwa kina serikali.
Kisa cha Daud na Jalut.
Jalut anajivuna kwa nguvu zake na uwezo wake wa kumuua kila aliyethubutu kukabiliananae kwenye uwanja wa mapambano.
Daud alipokuwa anakwenda kumkabili Jalut aliomba dua Allah amthibitishie miguu yake ardhini amkabili Jalut.
Chama chetu kilinyimwa usajili.
Lakini huo haukuwa mwisho wetu.
Tuliyokuja kufanya si tu yalimstaajabisha Mzee Lumelezi bali hata sisi wenyewe.
Nimeweka na picha ya mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Ghandhi Hindu Mandal mwaka wa 1955.
Fananisha picha hii na picha yetu.