Uhalifu wa mitandaoni tanzania basi tena!!!! 2024 /2025

Uhalifu wa mitandaoni tanzania basi tena!!!! 2024 /2025

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240
1_20241123_131725_0000.png



Serikali nchini Tanzania imeamua kuunda kikosi Kazi maalum cha kufuatilia makosa yote ya uhalifu mtandaoni, baada ya kufanyika mkutano wa wadau wa mawasiliano Jana novemba 22 mwaka 2024.

Mkutano ulifanyika makao makuu ya mawasiliano Tanzania (Tcra) , Dar es salaam ukihudhuriwa na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi mhandisi Hamad Masauni na Waziri wa habari mawasiliano na Teknolojia ya habari Jerry Silaa Pamoja na wadau wa mawasiliano na wawakilishi wa kampuni za simu.

2_20241123_131725_0001.png


Kikosi Kazi hicho kitahusisha wajumbe kutoka taasisi mbalimbali za serikali na wizara husika kuweza kushughulikia changamoto za uhalifu wa mitandaoni kwa ufanisi zaidi alisema mhandisi Masauni.


Makosa mbalimbali kama vile
• miamala mbalimbali ya kieletroniki
• wizi wa aina yoyote mtandaoni
• simu za utapeli au sms za utapeli nk.

3_20241123_131725_0002.png


Waziri Silaa naye alisisitiza " umuhimu wa ushirikiano wa karibu baina ya serikalini, kampuni za simu na sekta binafsi Pamoja na wadau mbalimbali katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu mtandaoni ambavyo vimeendelea kuwa tishio kwa usalama wa nchi.

Ukiona ujumbe wowote wa utapeli ripoti kupitia namba hii 15040.

4_20241123_131725_0003.png
 
Hawataweza zuia ila watapunguza matukio
 
View attachment 3159620


Serikali nchini Tanzania imeamua kuunda kikosi Kazi maalum cha kufuatilia makosa yote ya uhalifu mtandaoni, baada ya kufanyika mkutano wa wadau wa mawasiliano Jana novemba 22 mwaka 2024.

Mkutano ulifanyika makao makuu ya mawasiliano Tanzania (Tcra) , Dar es salaam ukihudhuriwa na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi mhandisi Hamad Masauni na Waziri wa habari mawasiliano na Teknolojia ya habari Jerry Silaa Pamoja na wadau wa mawasiliano na wawakilishi wa kampuni za simu.

View attachment 3159621

Kikosi Kazi hicho kitahusisha wajumbe kutoka taasisi mbalimbali za serikali na wizara husika kuweza kushughulikia changamoto za uhalifu wa mitandaoni kwa ufanisi zaidi alisema mhandisi Masauni.


Makosa mbalimbali kama vile
• miamala mbalimbali ya kieletroniki
• wizi wa aina yoyote mtandaoni
• simu za utapeli au sms za utapeli nk.

View attachment 3159622

Waziri Silaa naye alisisitiza " umuhimu wa ushirikiano wa karibu baina ya serikalini, kampuni za simu na sekta binafsi Pamoja na wadau mbalimbali katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu mtandaoni ambavyo vimeendelea kuwa tishio kwa usalama wa nchi.

Ukiona ujumbe wowote wa utapeli ripoti kupitia namba hii 15040.

View attachment 3159627
Tunajua uchaguzi unakuja hapo wanataka wakosoaji wa serikali dhalimu.

Kuhusu uharifu wanaufanya wao wenyewe

Mimi Mkulima wa Dumila napata wapi kuingilia mifumo ya TCRA?
 
Hicho kikao kilikuwa na mwakilishi wao, baada ya hapo na wao wanaenda kukaa kikao, hivyo mnapanga hivi na wao wanaweka mbinu hii, Mimi nilieko huku Isamvu- Mpimbwe huo uharifu naufanyaje! Ni nyie hao hao!
 
Back
Top Bottom