Uhamiaji acheni siasa, mnafeli wapi?

Uhamiaji acheni siasa, mnafeli wapi?

Syston

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2017
Posts
243
Reaction score
351
Wadau, nimelileta hili maana limenivuruga akili haswa.

Ipo hivi: Niliingia tovuti ya Uhamiaji kwa ajili ya maombi ya passport ila mambo niliyokutana nayo huko yameniacha hoi na kunifanya niamini siasa siyo mchezo mzuri. Kero nilizoziona ni kama ifuatavyo:

1. Katika kujaza form kuna kipengele kimeniuliza dhumuni la safari na ninasafiri kwenda nchi gani. hapa najiuliza kila anayeomba passport ni lazima awe anasafiri au passport unatakiwa uwe nayo ili ikitokea unasafiri ndio unaomba Visa ya nchi husika.

2. Hiki ndo kituko zaidi, imagine kuna kipengele kinanielekeza uwezekano wa kuombwa uthibitisho wa tiketi ya kurudi, cheti cha kuzaliwa cha bibi.

Hivi mtu nina miaka 30 unaniambia kweli nilete cheti cha kuzaliwa cha bibi, nyie bibi zenu wana hivyo vyeti? Au ndiyo mwenye nguvu mpishe? Acheni kuweka siasa kwenye mambo yenye maslahi na maisha ya watu.

3. Ajabu ni kuwa utaratibu wa kuomba passport umewekwa uonekane ni lazima uwe unasafiri ndiyo uombe passport, lakini je, inapotokea mtu anatakiwa asafiri haraka iwezekanavyo kuna utaratibu wa uhamiaji kutoa passport haraka iwezekanavyo au ndo mtafuata taratibu zenu na kuharibu dili za watu?

4. Kwa sasa tuna vitambulisho vya taifa ambavyo kuvipata kuna mchakato mtu anapitia kama kuhakikiwa na uhamiaji wenyewe, amabapo wasio na vyeti vya kuzaliwa wamepeleka viapo na walipokidhi vigezo wakapatiwa NATIONAL ID, anapokuja mtu anataka passport jaribuni kurahisisha kwa huyu mwenye kitambulisho cha NIDA maana taratibu mnazotaka apitie tayari alizipitia wakati mnamthibitisha kuwa ni Mtanzania na mkampa go ahead kwenda NIDA kupata ID. Kiukweli uhamiaji nilijaribu kuona labda hata kun amahali inasema kwa Muombaji mwenywe kitambulisho cha taifa afuate hatua hizi, sikuona zaidi ya mahali tu mmeomba utambulisho wa taifa. Badilikeni muende na kasi ya technolojia sio kila siku mtu anarudia kufanya vitu vilevile, mbona tra, brela nk, hawana longolongo wanaomba tu namba ya NIDA basi mchezo umeisha.

There is no such a thing as a little freedom, either you are completely free or a total slave.
 
Uhamiaji pana matatizo kweli, lakini huwezi tu ukaomba pasi halafu usiwe na walau na matamanio ya kusafiri, achilia mbali kusafiri.

Kama huna cheti cha bibi sio kigezo cha wewe kukosa pasi, afisa wa pasi atakushauri cha kufanya.
 
Hivyo vyote sio lazima ili upate passport tuwe positive, kwa kinaowahusu wanajaza especially hiyo ya safari ili wapate haraka kama hausafiri pia utapata ila priority inakua wanasafiri na hiyo ya Bibi nadhan ni kama hauna cheti au affidavit ya Mzazi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Malalamiko dhidi ya uhamiaji ni mengi sana, ajabu ni kwamba mamlaka zinazohusika zinaweka pamba masikioni.

Passport yangu kubwa ya zamani inakwisha muda wake mwishoni mwa mwezi huu, ila kila nikiwaza urasimu wao wa kupata passport mpya najikuta nakata tamaa kabla hata sijauanza.

Ni kwanini wenye passport kubwa za zamani asingetakiwa kuleta kitambulisho cha NIDA tu kupata passport mpya?

Taarifa za wateja wenu za mwanzo hamnazo kwenye kanzidata?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
goodluck5, Yaani yangu haijaisha ni mpaka 2027 lakini ndio natakiwa epassport halafu unaambiwa kila kitu ujaze upya na uwe 150000 ndio upate nyingine,nimeamua kuwa kimya kwanza mana hali si hali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nakata tamaa kabla hata sijauanza.

Ni kwanini wenye passport kubwa za zamani asingetakiwa kuleta kitambulisho cha NIDA tu kupata passport mpya?

Taarifa za wateja wenu za mwanzo hamnazo kwenye kanzidata?

Sent using Jamii Forums mobile app
[/QUOTE]

Yaan hii waione UHAMIAJI TANZANIA

Nami nimewaza sana kuhusu hii kitu, taarifa za mtu husika zipo tayari kwenu bado mnataka mchakato upyaa! Nadhani hawa wenye passports za zamani wangepata ahueni kidogo, wawe na form tofauti!

Pili: Usumbufu njoo leo, njoo kesho passport inakaa miezi mitatu jamani unahangaikia jamani!?
 
Uhamiaji pana matatizo kweli, lakini huwezi tu ukaomba pasi halafu usiwe na walau na matamanio ya kusafiri, achilia mbali kusafiri.

Kama huna cheti cha bibi sio kigezo cha wewe kukosa pasi, afisa wa pasi atakushauri cha kufanya.
Hapa ishu sio ushauri, nachojiuliza hawa watunga hizi kanuni huwa wanakuwa wamevuta bangi au wako keroro, tatizo tunaiga mataifa yaliyoendelea bila kuangalia uwezo wetu. Fikiria kuhusu usajili wa laini kwa national ID lakini bado mtu anajitokeza anakuambia mwisho kusajili ni laini kadhaa, sasa unajiuliza nina national ID, nasajiri kwa finger print, laini yangu ikihusika na uharifu ntawajibika mwenyewe maana NIDA wana data zangu na ni rahisi hata kuwafuata ndugu, lakini bado mtu asiye na ubongo kapewa majukumu ya kufikiri.
 
Hivyo vyote sio lazima ili upate passport tuwe positive, kwa kinaowahusu wanajaza especially hiyo ya safari ili wapate haraka kama hausafiri pia utapata ila priority inakua wanasafiri na hiyo ya Bibi nadhan ni kama hauna cheti au affidavit ya Mzazi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Affidavit oath ya mzazi sasa hivi wana national ID ambayo walitakiwa kuwa na hiyo Affidavit ili wakamilishe mchakato kupata ID, simple maths A=B, A=C, automatically B=C, kwa nini mtu arudie mchakato kupata Affidavit ya mzazi wakati mzazi aliapa kupata NIDA ID, why wasiweke kipengere kama mzazi ana NIDA ID basi ijazwe tu namba maana wao na NIDA sin watoto wa nyumba moja.
 
Nimeshakuwin kisaikolojia
Ha ha haa, mjomba usipanic, i like Joking around, and uki come across me the first thing utasema nina dharau coz hicho ndo wengi huniambia but kiuhalisia i like playing the human mind. maybe umeniwin but i don't think so.
 
Na sisi tunaohitaji kubadilisha za zamani usumbufu ni uleule? basi itabidi kuanza mchakato mapema
 
Back
Top Bottom