johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
TRA imebaki jina tuHarafu sasa hivi wengi hata mambo ya kodi hawayajui kazi kushinda vichochoroni kukamata risiti...
Tatizo Watu hudhani Kazi ya kukusanya Kodi TRA ni fursa ya kutajirika lakini wanasahau kuwa kutoza ushuru ni sehemu ya Ibada ilu Jamii iweze kustawiKuna kale kajamaa kafupiii kalikuaga kamishna hapo TRA kakatumbuliwa sasahivi knahangaika na madaladala ya mwendokasi kalikua kanaoneaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa, kanahamisha tu watu ilimradi tu kutenganisha wake na waume zao etc etc , kimsingi TRA kuna shida sana hasa inapokuja suala la mtumishi kutotoa kitu kidogo kwa wakubwa zake na lile la rushwa ya NGONO ndio kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
Hiyo ishu sio TRA pekee sehemu nyingi zinazojaza watu pana mambo ya ajabu ajabu sana...wanamaindiana huko utadhani pana kitu cha maana wanapata kumbe kawaida tuu..TRA imebaki jina tu
Staff wanarogana kama hawana akili nzuri
Ukienda kwa Mwamposya utawakuta Mapolisi na Watoza ushuru ndio wanaongoza kwa kutolewa mapepo
TRA hawapendani kabisa
RIP Tarimo
Uhamisho si jambo baya kwenye utumishi, ni kawaida mfanyakazi kuhamishwa kutoka kituo kimoja Kwenda kingine ili kuimarisha utendaji na kuleta ufanisi. Tatizo kubwa ni kuwa wafanyakazi tunahamishwa bila kulipwa stahiki zetu.Yah..haijakaa SAwa hiyo
Sasa mtumishi anapoambiwa atafute fedha zake ahame kana kwamba alijihamisha mwenyewe, je hii ni haki ?. Je Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan anajua kuwa kuna uonevu wa namna hii TRA ? Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Khasim Majaliwa analijua hili, Mkuu wa Utumishi, na Waziri wa Fedha wanalijua hili ? Nakumbuka serikali ilishatoa agizo kuwa mtumishi akihamishwa lazima apewe stahiki zake kwanza ndipo ahame sasahii ya kujigharimia imetoka wapi na kutishana kwenda TAMISEMI ?Mbona mnamsimanga sana wakati madai yake ni genuine.
Mambo sio marahisi hivyo bro ?Umejaribu kwenda kumuona immediate boss wako na boss wa kule unapohamishiwa kwa ajili ya malalamiko?
Mimi sifanyi kazi mamlaka ya zakayo lakin kuwalaumu katika kukusanya kodi ni tu unapungukiwa na ujuzi wa sheria wanazotumia kufanya kazi zao.Tatizo hata nyinyi mfumo wenu wa utendaji wa kazi pia umejaa dhuluma kubwa.Huwa mnatutesa sana sisi tunaohangaika huku Jua kali. Umeona sasa madhara ya kudhulumiwa yanavyouma. Pole sana lakini liwe pia fundisho, haya maumivu unayoyapitia ndiyo sisi wa jua kali tunayaishi siku zote kupitia nyinyi wafanyakazi wa TRA.
Boss, Halmashauri, Tamisemi na kufananako, wanaitwa kwenye vikao Dar au Dom kutokea chaka huko, wanajigharamia wakiahidiwa kulipwa, wengine wanamaliza miaka 2 hawalipwi, achilia mbali kukopwa mshahara wa kwanza na wa pili wa kuanzia kazi kwa kigezo cha Cheque Number.Mambo sio marahisi hivyo bro ?
Huyo Siyo chawa!Ukiona unaonewa ACHA KAZI
Mfanyabiashara akitunza kumbukumbu vizuri analipa Kodi kidogo sanaMimi sifanyi kazi mamlaka ya zakayo lakin kuwalaumu katika kukusanya kodi ni tu unapungukiwa na ujuzi wa sheria wanazotumia kufanya kazi zao.
Kodi ni muhim kwa maemdeleo na ustawi wa nchi lakin adui mkubwa wa ulipaji huo ni watunga sheria au sera.
Kiuhalisia wakusanya kodi wakinyoosha rula jumuia yote ya wafanyabiashara ingekuwa na vilio kama vya msiba wa waliokula sumu kwenye shughuli. Aina ya rushwa zao ni scratch my back I scratch yours. Looser ni fuko kuu.
Nadhan umeshajua tatizo lilipo. Nadhan umeshamjua wa kupiga jiwe kwa kombeo!
Acha wafu mzikaneMheshimiwa Kamishna Mkuu wa TRA, nachukua fursa hii kukuomba uingilie kati uonevu unaofanywa na wasaidizi wako kwenye uhamisho unaoendelea sasa.
Nimefanya kazi TRA miaka mingi lakini hali iliyojitokeza sasa si ya kufumbia macho.
Uhamisho si jambo baya kwenye utumishi, ni kawaida mfanyakazi kuhamishwa kutoka kituo kimoja Kwenda kingine ili kuimarisha utendaji na kuleta ufanisi. Tatizo kubwa ni kuwa wafanyakazi tunahamishwa bila kulipwa stahiki zetu.
Mkuu wa Rasilimali aliyepo hapo anatulazimisha Kwenda kwenye vituo vipya bila kulipwa anasema kama huna hela za kuhama nenda kakope Benki au mahali popote ili mradi uende unakotakiwa Kwenda. Na anatishia kuwa usipokwenda utaona kitakachokukuta ikiwa ni Pamoja na kuhamishiwa TAMISEMI.
Inaonekana kuw TAMISEMI ndio sehemu ya kupeleka watu wasiotakiwa.
Nina uhakika wewe Kamishna Mkuu hulijui hili kwa kuwa tunakufahamu kuwa wewe ni mtu wa haki na hupendi wafanyakazi wateseke.
Kwa mujibu wa utumishi, mfanyakazi anapohamishwa Kwenda kituo kipya cha kazi anatakiwa alipwe kama ifuatavyo:
1. Usafiri
Mfanyakazi anatakiwa apewe usafiri Kwenda kwenye kituo kipya cha kazi, yeye na mke au mume na Watoto wasiozidi 4 walio tegemezi kwa mfanyakazi. Kiutumishi, usafiri au nauli vinatakiwa kulipwa na kituo anachoondoka (kuhama) kabla mtumisji ahajaondoka Kwenda kwenye kituo kipya.
2. Fedha ya kufungashia mizigo (Disturbance allowance)
Hii ni aslimia 10 ya mshahara ghafi wa mwaka wa mfanyakazi, na inatakiwa ilipwe wiki mbili kabla ya mtumishi kuondoka kituo cha zamani.
3. Fedha za kujikimu
Mtumishi anapofika kwenye kituo kipya anatakiwa kulipwa fedha za kujikimu, kwa mujibu wa kanuni za utumishi
4. kusafirishiwa mizigo
Mtumishi anapohamishwa anatakiwa kusafirishiwa mizigo kwa mujibu wa stahiki zake.
Sasa Mheshimiwa Kamishna Mkuu, mtumishi anapoambiwa atafute fedha zake ahame kana kwamba alijihamisha mwenyewe, je hii ni haki ?.
Je Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan anajua kuwa kuna uonevu wa namna hii TRA ? Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Khasim Majaliwa analijua hili, Mkuu wa Utumishi, na Waziri wa Fedha wanalijua hili ?
Au hawa maafisa wanatarajia tukapokee rushwa kwenye vituo vipya ? wanatarajia tukaibe ? Au wanakusudia nini kama sio kutukomoa.
Mheshimiwa Kamishna Mkuu najua hili liko kwenye uwezo wako, tafadhali fuatilia mwenyewe, waulize hata hao waliohamishwa, utaona hayo mauzamauza yanayofanywa na wasaidizi wako. Kuanzia Makamishna, Wakurugenzi husika na maafisa wao lao ni moja. Wanataka wewe uonekane mbaya kwa wafanyakazi wakati sisi tunajua sio hivyo.
Viongozi hawa sijui wamepataje nafasi hizi ambazo hawazimudu kabisa ?. Uongozi ni Pamoja na kutetea haki za wafanyakazi, jambo ambalo wasaidizi wako hawalifanyi.
Kuanzia idara ya Rasilimaliwatu, kuna huyu Renada ambaye ana majibu ya Manzese utafikiri hajasoma kabisa. Halafu n akule fedha pia ukumulike.
Mimi nimehamishiwa mikoa ya kusini, nina miezi miwili sijalipwa, wengine Mwezi mmoja, wengine wiki mbili watu tunaishi mahotelini. Jamani hii ni kinyume na haki za binadamu.
Nakuomba Mheshimiwa ufuatilie tupate malipo yetu na hawa dhulumati wapewe haki yao ya uonezi.
Nakuomba usianze kutafuta nani kaandika, angalia u ukweli uliopo.
Nimetumia njia hii kwa kuwa kuna ugumu mkubwa sana kukufikia, na victimisation lazima itokee kama nigekuja mwenyewe au hata kukutumia barua
Asante
Johnson
Hivi masamaki ndo yule alikuwa na nyumba za kisasa zaidi ya mia Daressalamm?Tatizo Watu hudhani Kazi ya kukusanya Kodi TRA ni fursa ya kutajirika lakini wanasahau kuwa kutoza ushuru ni sehemu ya Ibada ilu Jamii iweze kustawi
Sijawahi kumuona Kamishna wa TRA aliyekuwa na maisha mazuri baada ya kustaafu kuanzia enzi za akina Ndyetabula, Rutaitina, ST Masawe, Kapera, Kezilahabi, Sanare, Silla, Kitilya, Masamaki nk....nk
Rushwa hupofusha macho kwa mujibu wa Biblia