Uhasama wa Tanzania bara na Zanzibar unazidi kukua na utaleta madhara makubwa kama yanayosemwa hayatashughulikiwa

Uhasama wa Tanzania bara na Zanzibar unazidi kukua na utaleta madhara makubwa kama yanayosemwa hayatashughulikiwa

Jinsi masuala ya muungano yanavyoshughulikiwa na kwa sasa, ni mtu kipofu wa akili tu ndio hataona kwamba kadiri siku zinavyopita mbegu za uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar inazidi kuota mizizi, majani ya chuki yakizidi kuchanua. Ni kiongozi mjinga tu asieweza kuona kwamba jinsi haya mambo ya muungano yanakoenda, yanaweza kusababisha mgongano (confrontation) mkubwa sana kati ya wakazi wa Zanzibar walioko bara na wakazi wa bara walioko Zanzibar.

Badala ya kujibu hoja zinazowekwa mezani, viongozi wameamua kwa makusudi kuwashambulia wale wanaozitoa, bila kuona kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kuchochea uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Kwa kumfurahisha nani?

Kama Tanzania bara wanaona kwamba kwao kero kubwa ya muungano ni kutokuwa na serikali ya Tanganyika, kwa nini hawasikilizwi? Wakati wa Nyerere huenda kulikuwa na sababu za msingi kuwa na serikali mbili, lakini ni wazi hilo halikubaliki kwa sasa, na huwezi kulilazimisha likaendelea kuwapo bila kuleta madhara.

Muungano tunaweza kulazimishwa uendelee kuwapo kwa kutumia nguvu ya dola, lakini haitazuia watu kuanza violence (kupigana) uhasama unaojitokea ukizidi kukua. Amini nawaambieni, huu muungano mnaodai uko imara unaweza kuvunjwa kwa nguvu na kuleta hali ya machafuko bara na visiwani. Watanzania bara walioko visiwani wataondolewa kule kwa nguvu, na wa-Zanzibar walikoko bara wataondolewa huku kwa nguvu, na hata kupoteza mali au uhai wao. Ndilo tunalosubiri? Au tunadhani haliwezi kutokea Tanzania, vitu kama hivyo vinatokea Rwanda tu?

Muungano ulifanyika zaidi ili Zanzibar kusiwe na counter-revolution ya Waarabu (wajomba) walipopinduliwa na kuchinjwa, na kwa Tanganyika kulinda usalama wake katika kuwa kitovu cha kupigania uhuru wa Afrika. Sasa hizi sababu sio hoja tena. Kama imefikia mahali Watanzania hawautaki muungano, basi ni bora uvunjwe kwa utaratibu na kuelewana, watu waulizwe je ungependa kubaki bara au kurudi visiwani, au ungependa kubaki visiwani au kurudi bara nk. Labda tuanze na "Referendum", wananchi ndio tuamue kidemokrasia kama tunataka au hatutaki muungano, sio serikali ituamulie kwa maslahi yake, au maslahi ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, au maslahi ya CCM.

Tusione aibu kukaa chini na kutafakari kuuvunja muungano, kama kuwa na serikali moja au tatu haiwezekani, kwa sababu mfumo wa muungano uliopo sasa hivi unazidi kukuza uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mwaka 1982 Senegal na Gambia waliungana na kuwa nchi moja ya Senegambia. Iliposhindikana, waliuvunja muungano, mwaka 1989. Juzi hapa Uingereza imejitoa kwenye muungano wa Ulaya. Kwa hiyo Tanzania haitakuwa ya kwanza kuvunja muungano. Muungano ni mkataba.
Upo sahihi..zile hofu za Waarabu na Ukomunisti hazipo tena!
Ni kweli Watsnganyika haturudhiki tena na jinsi Mambo yanavoenda! Ila Kuna watu wanajifanya hawaoni! Tunstaka Katiba ya Warioba!
 
Sheria iliyounda Senagambia, had provisions za kuuvunja. Ule ulikuwa ni mkataba, the same to UK kujitoa EU.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu ni Muungano wa dhima ya Muungano wa milele, zile Articles of the Union, sio mkataba, ni makubaliano ya milele, hakuna provision ya kuuvunja Muungano, tumeunganisha nchi mbili kwa kuchanganya udongo, na kuumwaga bara na Zanzibar, ili kuuvunja, lazima tuutafute ule udogo, tuupembue, punje za udongo wa Tanganyika, zirejeshwe Tanganyika na punje za Zanzibar zirejeshwe Zanzibar.

Kikemikali, muungano wetu ni compound na sio mixture!. Kikemikali, Ukichanganya vitu viwili na kuwa mixture, vitu hivyo vinakuwa havijaungana kikemikali, mfano kuchanhanya pombe na maji, kwa kutumia fractional distillation inawezekana kuitenganisha pombe na.maji. Vitu kama maji, H2Ounaweza kutenganisha hydrogen na oxygen, chumvi, unaweza hydrogen na.chlorine etc.

Lakini vitu viwili vinapoungana kwa chemical reaction, vitu viwili vile hufa na kuzaliwa kitu kipya kinachoitwa compound, huwezi tena kuvirejesha kwenye hali ya awali kama kuyeyusha sabuni ya unga kwenye maji, kunatokea chemical reaction, huwezi kutenganisha.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu, ume undergo chemical reaction kwa mataifa mawili Tanganyika na Zanzibar kuungana, kupoteza utaifa wake.na kuunda taifa jipya la Tanzania ambalo ni compound, halivunjiki tena!.

Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote.
P
Hoja hapa si kubaguana nadhani tuna exaggerate hili nyumba,gari na hata binadamu hufanyiwa ukarabati jinsi muda unavyokwenda ili kuviboresha na kuongezea uhai,jana leo na kesho ni vitu tofauti.Kupitia upya mifumo ie muungano kwa mahitaji ya sasa siyo kuupinga na kuleta ubaguzi tuache spinning.Tunaoshupaza shingo kuupitia upya ndiyo wavunja muungano kwa unafiki. wakemewe
 
Hakuna madhara yeyote, ni wazi Zanzibar hawataki huu muungano, tuwape kanchi kao walipe bill zao wenyewe, na wakitaka wamrudishe sultani sawa tuu, na wakitaka wajitangaze kabisa Islamic state under Sharia law, waende tuu na hata madeni tutawasamehe, huu sio muungano, kalikuwa kaproject ka mwalimu na Karume na fantasy zao za vita baridi za mabeberu na ukomunist
 
madhara yatakuwa makubwa kwa raia? raia gani? tueleweshe, serikali tatu Tanganyika watapata madhara gani, na zanzibar watapata madhara gani.
Serikali 3 zitasababisha hali ya changu ni changu pande zote kama Zanzibar wanavyofanya sasa hivi.
Matokeo yake, mfano tu, raia wa Zanzibar anayemiliki ardhi Tanganyika atanyang'anywa vinginevyo Zanzibar wakubali watanganyika kununua ardhi kwao.
Kwa ujumla kutakuwa na mtafaruku utakaosababisha watu kupoteza mali na hata muungano wenyewe kuvunjika.
Zanzibar watashindwa kuchangia serikali ya muungano (kipato chao kidogo), wafanyakazi waliopo bara kwa jina la serikali ya muungano watarudishwa kwao, wabunge wa kutoka Zanzibar watakosa fursa walizo nazo sasa na mengine mengi.
Raia wa Tanganyika waliopo Zanzibar watafukuzwa pia kwa sababu ya chuki ya kisiasa itakayojengeka.
 
Duh!, hakuna any provisions popote za kuuvunja muungano, huko kuuvunja kutaanzia wapi?.
Siku hizi tunahangaika sana na muungano huu.
Baada ya kukusoma juu ya hilo la kutokuwepo na 'provisions' za kuuvunja muungano; bila kujali niliyokwishajibu kuhusu jambo hilo, nimepata mfano sahihi wa kuunga hilo wazo la 'provisions'.

China ya Beijing (hivi hii ilitokatokaje kuwa Peking) na Hong Kong. Huo ndio mfano sahihi unaoendana na Tanganyika yetu na Zanzibar. Achana na habari za Zanzibar ilikuwa nchi huru kabla ya muungano.
Ile pwani iliyowahi kudaiwa na Sultan kuwa sehemu ya Zanzibar, ni sababu tosha ya Zanzibar kuwa 'an integral part of Tanganyika. Yeyote anayetafuta kuiondoa Zanzibar atakuwa anachezea usalama wa Tanganyika.
 
Mambo mengi yaliyofanyika wakati ww Nyerere yalikuwa ya kulazimisha, na alitumia uelewa duni wa wananchi kuyaimplement. Kwa bahati mbaya washauri wake wengi yeye ndio aligeuka mshauri wao. Hata hii katiba tunayoipigia kelele leo hii, ilitungwa rasmi kuendana na utashi wake. Kibaya zaidi alijua ubaya wa katiba hii, lakini hakutaka kuibadili maana aliogopa chama chake Cha ccm kitang'olewa madarakani.

Kwa hapa tulipofikia ccm lazima wajue kizazi kimebadilika, na yenyewe sio sehemu ya kizazi hiki. Ni vyema wakaruhusu rasimu ya Warioba itengeneze katiba yenye maoni halisi ya wananchi, na sio katiba ya kuifanya ccm isalie madarakani. Kinyume na hapo machafuko ama mapinduzi ya kijeshi lazima yatatokea hapa nchini Ili kupata mabadiliko ya kweli.
Mkuu, hatuhitaji kumtupia lawama mtu yeyote kwa sababu

Katiba hii hii mbovu, imetumika miaka mingi sasa na ilionekana ipo sawia kabisa kwa nyakati hizo ila kwa sasa haifai tena, naamini, hata ikiandikwa mpya leo, bado huko mbeleni haitaifaa tena kizazi kijacho kutokana na namna ya kizazi hiko

Na hata sasa, muungano wetu leo, unaonekana na matobo ni kutokana na majira na nyakati kupita, kwa kizazi tulichopo, ni vyema usukwe upya tena
 
Siku hizi tunahangaika sana na muungano huu.
Baada ya kukusoma juu ya hilo la kutokuwepo na 'provisions' za kuuvunja muungano; bila kujali niliyokwishajibu kuhusu jambo hilo, nimepata mfano sahihi wa kuunga hilo wazo la 'provisions'.

China ya Beijing (hivi hii ilitokatokaje kuwa Peking) na Hong Kong. Huo ndio mfano sahihi unaoendana na Tanganyika yetu na Zanzibar. Achana na habari za Zanzibar ilikuwa nchi huru kabla ya muungano.
Kwa kweli sijasoma ilikuwaje, wavunja miungano ni mabeberu, kama Japan na Taiwan, ni Mabeberu wa Marekani. China na Hong Kong ni mabeberu wa UK!.
Kwa vile zile Articles za Union, sio mkataba, ni agreement tuu, huko nyuma, niliwahi kuzifuatilia hadi UN, sikuziona!, Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?!. (Ufuatiliaji Muungano Sehemu ya I) na Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria (De Jure) Bali ni De Factor?!
P.
 
Kama serikali tatu haifai basi serikali moja, kama tunaupenda muungano kweli

Hakuna workable formula. Muunganio hauwezekaniki. Milioni 62 kwa milioni 1 unusu, the math ain't mathing.

Serikali moja maana yake Zanzibar ni mkoa. Zanzibar ishasema toka 1964, haitaki kuwa mkoa.

Serikali mbili ndo hizi, Muungano umeshikiliwa kwa mtutu wa bunduki. Nyerere na Dr. Shein walidhani wakimfunga Maalim Seif na kum house arrest Aboud Jumbe na kuwa shuti Mashehe wa Uamsho na kutishia kuwafukuza chamani G55 basi tatizo limekwisha, Hola! Hoja ya ubovu wa muungano bado inaita!

Serikali tatu ni gharama za kinyonyaji na kijinga, Tanganyika hatuwezi kukubali. Tukishakuwa na serikali ya Tanganyika ya kuendesha mambo yetu hiyo ya Zanzibar tunaihitaji ya nini ???? Kwa nini tubebe mzigo, Zanzibar wana nini cha mno cha kuungana nao ????? Ma stress ya serikali tatu ya nini ?????????

HAKUNA jawabu la Muungano. Hasara tupu. Sio kila Muungano una faida. UK walijitoa EU. Tuvunje Muungano, for heavens sake!
 
Jinsi walivyowengi huku bara siku kikinuka sidhani kama watapata pa kukaa huko visiwani.

Wanazaliana kwa wingi mno halafu Ardhi ya kuwatosha hawana.

Ardhi wanayoitegemea ni ya Tanganyika na bado wanaleta kiburi.
 
Raisi wa Tanganyika katoka Zanzibar lakini mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar, mambo ya ajabu kabisa
 
Serikali 3 ni kurudi nyuma na madhara yatakuwa makubwa kwa raia. Bora kwenda mbele kwenye serikali moja.
Madhara ya erikali moja ni baadhi ya wanasiasa kukosa vyeo na madaraka.
Umeeleza kitu kidogo sana mkuu unamaanisha serikali moja itasababisha viongozi kukosa vyeo?? Kaa chini fikiria upya.
 
Umeeleza kitu kidogo sana mkuu unamaanisha serikali moja itasababisha viongozi kukosa vyeo?? Kaa chini fikiria upya.
Ndiyo,
Hawatakuwepo Rais wa Zanzibar, makamu wa kwanza na wa pili, mawaziri wa Zanzibar, baraza la mawaziri la Tanzania nafasi zitagawanywa pande zote za muungano, wakuu wa taasisi zisizo za muungano watapungua baada ya kuunganishwa, ......
 
Ndiyo,
Hawatakuwepo Rais wa Zanzibar, makamu wa kwanza na wa pili, mawaziri wa Zanzibar, baraza la mawaziri la Tanzania nafasi zitagawanywa pande zote za muungano, wakuu wa taasisi zisizo za muungano watapungua baada ya kuunganishwa, ......
Hivyo ni vitu vidogo sana. Kikubwa zaidi nadhani kipo kwa wananchi.
 
Ndiyo,
Hawatakuwepo Rais wa Zanzibar, makamu wa kwanza na wa pili, mawaziri wa Zanzibar, baraza la mawaziri la Tanzania nafasi zitagawanywa pande zote za muungano, wakuu wa taasisi zisizo za muungano watapungua baada ya kuunganishwa, ......
Na kwenye uchaguzi watu wa bara hawatawapigia kura watu waliotokea Zanzibar maana Ubaguzi unaonekana dhahir hivi sasa !!

Kwahiyo siioni Zanzibar ikikubali kupoteza Utaifa wake. !

Waswahili Wanasemaga Akumulikaye mchana Usiku atakuchoma !
 
Wabara tulikuwa kama tunapuuza fulani hivi ila wazenji wenyewe tangu Zamani wanapambanis upande wao na wana umoja bila kujali itikadi,sasa huku bara kuna kama kufumbuliwa macho hivi,sasa huku bara wakiendelea hivi, wazenji watalia sana.

NB: WAZENJI WABAGUZI SANA LAZIMA TWENDE NAO JINO KWA JINO
 
Wabara tulikuwa kama tunapuuza fulani hivi ila wazenji wenyewe tangu Zamani wanapambanis upande wao na wana umoja bila kujali itikadi,sasa huku bara kuna kama kufumbuliwa macho hivi,sasa huku bara wakiendelea hivi, wazenji watalia sana.

NB: WAZENJI WABAGUZI SANA LAZIMA TWENDE NAO JINO KWA JINO
Ubaguzi huo !
 
Back
Top Bottom