Uhasama wa Tanzania bara na Zanzibar unazidi kukua na utaleta madhara makubwa kama yanayosemwa hayatashughulikiwa

Uhasama wa Tanzania bara na Zanzibar unazidi kukua na utaleta madhara makubwa kama yanayosemwa hayatashughulikiwa

Jinsi masuala ya muungano yanavyoshughulikiwa na kwa sasa, ni mtu kipofu wa akili tu ndio hataona kwamba kadiri siku zinavyopita mbegu za uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar inazidi kuota mizizi, majani ya chuki yakizidi kuchanua. Ni kiongozi mjinga tu asieweza kuona kwamba jinsi haya mambo ya muungano yanakoenda, yanaweza kusababisha mgongano (confrontation) mkubwa sana kati ya wakazi wa Zanzibar walioko bara na wakazi wa bara walioko Zanzibar.

Badala ya kujibu hoja zinazowekwa mezani, viongozi wameamua kwa makusudi kuwashambulia wale wanaozitoa, bila kuona kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kuchochea uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Kwa kumfurahisha nani?

Kama Tanzania bara wanaona kwamba kwao kero kubwa ya muungano ni kutokuwa na serikali ya Tanganyika, kwa nini hawasikilizwi? Wakati wa Nyerere huenda kulikuwa na sababu za msingi kuwa na serikali mbili, lakini ni wazi hilo halikubaliki kwa sasa, na huwezi kulilazimisha likaendelea kuwapo bila kuleta madhara.

Muungano tunaweza kulazimishwa uendelee kuwapo kwa kutumia nguvu ya dola, lakini haitazuia watu kuanza violence (kupigana) uhasama unaojitokea ukizidi kukua. Amini nawaambieni, huu muungano mnaodai uko imara unaweza kuvunjwa kwa nguvu na kuleta hali ya machafuko bara na visiwani. Watanzania bara walioko visiwani wataondolewa kule kwa nguvu, na wa-Zanzibar walikoko bara wataondolewa huku kwa nguvu, na hata kupoteza mali au uhai wao. Ndilo tunalosubiri? Au tunadhani haliwezi kutokea Tanzania, vitu kama hivyo vinatokea Rwanda tu?

Muungano ulifanyika zaidi ili Zanzibar kusiwe na counter-revolution ya Waarabu (wajomba) walipopinduliwa na kuchinjwa, na kwa Tanganyika kulinda usalama wake katika kuwa kitovu cha kupigania uhuru wa Afrika. Sasa hizi sababu sio hoja tena. Kama imefikia mahali Watanzania hawautaki muungano, basi ni bora uvunjwe kwa utaratibu na kuelewana, watu waulizwe je ungependa kubaki bara au kurudi visiwani, au ungependa kubaki visiwani au kurudi bara nk. Labda tuanze na "Referendum", wananchi ndio tuamue kidemokrasia kama tunataka au hatutaki muungano, sio serikali ituamulie kwa maslahi yake, au maslahi ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, au maslahi ya CCM.

Tusione aibu kukaa chini na kutafakari kuuvunja muungano, kama kuwa na serikali moja au tatu haiwezekani, kwa sababu mfumo wa muungano uliopo sasa hivi unazidi kukuza uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mwaka 1982 Senegal na Gambia waliungana na kuwa nchi moja ya Senegambia. Iliposhindikana, waliuvunja muungano, mwaka 1989. Juzi hapa Uingereza imejitoa kwenye muungano wa Ulaya. Kwa hiyo Tanzania haitakuwa ya kwanza kuvunja muungano. Muungano ni mkataba.
Kwani huu muungano ukifa shida ipo wapi? Kwanini tulazimishane kuungana wakati muungano umegeuka KERO badala ya neema? Sijawahi kuona muungano wa kiquma kama huu tangu nizaliwe.
 
Sie wengine zanziber ni sawa na kisiwa cha mafia ukerewe au kome, hizi kelele zinachagizwa na wanasiasa wa hovyo kama lissu na jussa,

Nyerere aliuliza mpemba na mdigo na mjaluo yupi ndugu zaidi? Wapo wapemba wananunua mchele na hatuna shida nao, wapo dadapoa kutoka shinyanga wako unguja, kuna wamasai wapo fukwe za tumbatu wakisaka vibabu vya kiitaliano.
kwan kati ya mmasai wa tz na mmasai wa kenya vs mmakonde yupi ndugu zaid ? ccmu inajaa wajinga siku hz

hoja za Lissu zipo wazi kwann mtanganyika hanaonekana raia daraj la pili kule zenji ?

ukute wewe ni mtanganyika ila ccmu wamekujaza ujinga
 
HATUTAKI SERIKALI ya Tanganyikana. Tunataka nchi ya Tanganyika.

Hatutaki serikali tatu. Serikali tatu zinakupa Marais watatu, mabunge watatu, wabunge mia tisa, Majaji Wakuu Watatu, Makamu wa Rais watatu, Waziri Wakuu watatu.

HAKUNA formulation ya Muungano wa watu milioni 62 na watu milioni moja unusu halafu ikawa fair. Mkubwa atanyonywa na vilio havitaisha.

Huwezi kuunganisha shamba lako na mashamba ya Muhammed Dewji halafu muanze kugawana mavuno na mamlaka ya uendeshaji na amana za mikopo na nafasi za wakulima. Wewe unamwongezea thamani gani ?

Tuuvunje Muungano, for the love of God!
kwa anayofanya Sa100 , tuvunje tu muungano
 
Nadhani hujaelewa hili somo, kwa nini tumefikia hapa tulipo, na tumefikia hapa tulipo leo na sio huko nyuma. Nataka nikueleze jambo moja very serious, ujue kuna mengi sana nyuma ya pazia. Makubwa ni matatu;
  1. Zanzibar kuna potential kubwa ya mafuta, na yakipatikana Zanzibar itakuwa kama Kuwait; kimapato, ukitumia GDP, the richest country in the world. Tangu ijulikane kuwa Zanzibar ina uwezekano mkubwa wa kuwa na mafuta, suala la nishati (mafuta na gesi) kuwa katika muungamo likawa ni kero ya muungano kwa upande wa Zanzibar, jambo la kuondolewa
  2. Zanzibar ni kisiwa cha kimkakati (strategic island) kiuchumi. Kuna mataifa kama Oman, UAR, Saudi Arabia nk, wako tayari kuingia makubaliano nao ili kiwe katika himaya zao na kuwaahidi Zanzibar mabilioni ya dola, kwamba wakikubali wataishi kama wako peoponi tayari na hakutakuwa na Mzaznibar masikini au asiye na nyumba ya kifahari, matibabu bire kwa wote, na kila mkazi atajengewa nyumba ya kisasa nk. Zanzibar hawawezi kuingia makubaliano kama hayo wakiwa sehemu ya Tanzania, na wakilazimisha basi itabidi JWTZ wachukulie ni uvamizi.
  3. Zanzibar ni kisiwa cha kimkakati (strategic island) kijeshi. Kuna mataifa kama USA, China, Russia nk, wako tayari kuingia makubaliano nao ili kiwe kituo chao cha kijeshi, na kuwaahidi Zanzibar mabilioni ya dola. Tanzania (bara) hawako tayari kuruhusu hili, kwa gharama yeyote ya kulinda muungano, hata kama ni kuwalea huku wanakukojolea kila siku.
Kwa hiyo basi, hizo ndio sababu za msingi zinafanya Zanzibar waone muungano kwa sasa unawazuia kuingia peponi, kulingana na ahadi wanazopewa kama wakiuvunja. Wanafanya kila njia ili kuwakera Tanzania bara kwa visababu vingi vidogovidogo lakini haya ndio mambo yaliyoko nyuma ya pazia.

Hawatasema sababu za kutaka kuvunja muungano, na haya mengine unayosikia ni kelele tu. Na aliethubutu kujaribu hili la kuiondoa Zanzibar katika muungano alikuwa ni Aboud Jumbe, ndio maana akaishia kutengwa kama mtu mwenye ukoma. In fact, ilitakiwa afungwe kwa uhaini. Aliyevujisha taarifa za kile Aboud Jumbe alitaka kufanya alikuwa ni Maalim Seif Sharif, hadi akazawadiwa Uwaziri Kiongozi. Lakini waliambiwa wazi, mtu mwingine yeyote akithubutu, JWTZ itaingia, na wakumbuke hatutahitaji kuweka boots on the ground in Zanzibar wakifanya uasi. Tunaweza kuwapiga tukiwa Bagamoyo.

Sasa, theory nyingine ya kutisha iliyopo ni kwamba hata Raisi Samia huenda anatumika kama kichocheo cha kuvunja muungano, akitumia nafasi yake kuwaudhi watu wa bara ili wafikie hatua kusema hawataki tena muungano. Watu wana theorize kwamba anafanya makusudi kuingia mikataba kama ya bandari, kuleta Wa-Zanzibar waajiriwe bara nk, kwa lengo la kuchochea hasira upande wa bara, hasira ambayo mwisho wake ni kuvunja muungano.

Angalia kwamba theory ya Raisi Samia kutumika kama kichocheo cha kuvunja muungano inakuwa na logic fulani kwa jinsi alivyong'ang'ania mkataba wa bandari. Ilikuwa ni kama ugomvi wa watu wa bara na Samia, na hakujali kuendelea kuwaudhi watu, hata viongozi wa dini, na wazee wa busara, kwa sababu hilo ndio lilikuwa lengo; wakasirike, waseme sasa muungano basi. Katika hali ya kawaida ya siasa, zile kelele zilipaswa kumfanya aseme basi tunaacha tumewasikia wananchi. Lakini akakaza uzi tu, japo upinzani wa juu sana aliokabiliana nao. Theory ni kwamba kulikuwa na sababu ya yeye kushika ule msimamo, na hiyo sababu haikuwa ya kiuchumi.

Na kuna vitu vingine vingi vinavyohusu kuwafungulia waarabu fursa upande wa bara, pamoja na mambo ya mbuga za wanyama nk. Haya yote yalionekana kuwa ni strategy, kwamba hata kama muungano utavunjika, uwepo wa hawa waarabu upande wa bara, waarabu wanaoonwa kuwa wajomba wa Samia na watu wa Zanzibar, kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar. Na hata kuna watu wanasema haya mambo yanafanyika kwa coordination ya Zanzibar na Uarabuni.

Kuna mengi sana nyuma ya pazia. Suala ni kwamba, ni thory tu au yana ukweli ndani yake? Nilitaka kupost hili jambo kama thread inayojitegemea, lakini wewe sasa ndio umefanya niliseme. Haya ni baadhi ya mambo Nyerere alijua, na akawa na msimamo muungano usivunjwe kwa gharama yeyote ile. Hofu yake ilikuwa ni ya kuisalama. Lakini suala la Samia kuwa Raisi wa Tanzania limepeleka hili jambo katika level nyingine kabisa.
sorry umeandika pumba mkuu

kwahiyo unauza nchi ya Tz ili kuizuia Zenj isipige hatua ? je mapato yao huwa mnaletewa huku bara ?

fanya research achana na hizo story za vijiweni
 
Muungano uboreshwe hapo tunaongea lugha moja. Na ndiyo maana kuna Wizara inayoshughulikia kero za Muungano chini ya Makamu wa Rais. Halafu kuna Tume ya Fedha ya pamoja ndani ya Wizara ya Fedha ya JMT.

Wakati East Africa Community inazidi kupata mvuto kwa nchi kujiunga kutoka zile 3 za asili (Kenya, Tanzania na Uganda) hadi kuwa na nyongeza za Rwanda, DRC, Burundi na South Sudan, huku Tanzania wanaharakati uchwara wanataka kuvuruga muungano uliotulia??

Mpaka Somali na Ethiopia wako kwenye mchakato wa kuingia EAC. Eti sisi tunaona ZNZ ni mzigo kisa hawalipi umeme auHamidu Shaka ni DC wa Ifakara.

Dunia nzima itatucheka. Mfumo wa Serikali 3 waonekana uko vulnerable kuvunja muungano ndiyo maana haushabikiwi sana.

Watu wanaogopa kilichotokea kwa Gorbachev alipobaki hana ardhi anayotawala

Senegal na Gambia walikuwa na Muungano wakaita Senegambia ila walidumu kwa muda mfupi
ila Lumumba imejaza watu wajinga sana , mbona uliyoyaandika hayajibu maswali ya Lissu , siku tukiungana EAC kila raia atakuwa huru kwenda nchi jiran kumiliki lolote pia uhuru wa kuabudu kitu ambacho watanganyika wanakidai kwa Zanzibar

kwann mzenji anamiliki ardhi huku ila sisi hatuwez kwenda kumiliki ardhi kule kwao ?

kwann mzenji anaeza kuwa kiongoz huku bara hata uenyekiti wa kijiji ila si mtanganyika kuwa kiongoz kule zenji ?

kwann wao wana uhuru wa kuabudu huku bara ila sisi wakristo hatuna uhuru wa kufungua sehem za kuabudu kule zenj ?

Zenji ni eneo la kuongeza kura kwa ccmu kipind cha uchaguz

UKIWA MJINGA UNAKUWA MTAJI WA CCMU
 
Serikali 3 zitasababisha hali ya changu ni changu pande zote kama Zanzibar wanavyofanya sasa hivi.
Matokeo yake, mfano tu, raia wa Zanzibar anayemiliki ardhi Tanganyika atanyang'anywa vinginevyo Zanzibar wakubali watanganyika kununua ardhi kwao.
Kwa ujumla kutakuwa na mtafaruku utakaosababisha watu kupoteza mali na hata muungano wenyewe kuvunjika.
Zanzibar watashindwa kuchangia serikali ya muungano (kipato chao kidogo), wafanyakazi waliopo bara kwa jina la serikali ya muungano watarudishwa kwao, wabunge wa kutoka Zanzibar watakosa fursa walizo nazo sasa na mengine mengi.
Raia wa Tanganyika waliopo Zanzibar watafukuzwa pia kwa sababu ya chuki ya kisiasa itakayojengeka.
ni bora tuvunje muungano kuliko kuendelea kuwapa ccmu pa kujazia kura za uchaguz kwa kodi zetu zinazoenda wapet peti wazenji
 
Ubaguzi huo !
kunizuia mimi mtz mwenzio kumiliki ardhi huko kwenu huo sio ubaguz ila mimi kukutaka urudi kwenu nami nimiliki ardhi yangu huu ndo ubaguz si ndio ?

JINO KWA JINO MPK AKILI ZIWAKAE
 
Bro Umezungumza kama dikteta hujatoa suluhisho nini kifanyike kutatua KERO ambazo ndio msingi wa hoja za muungano na mara nyini wanasiasa zaidi ni maslahi sio ufumbuzi wa kudumu kwa nini iwe chako chetu na chetu chetu?
kweny huu muungano kipele ni Zanzibar , maana hawapo kwenye muungano ila ccmu ya Tanganyika inalazimisha huu muungano sababu ni kichaka chao cha kura kipindi cha uchaguzi
 
Hivi kwanini huu muungano usizamwishwe baharini na hawa wala UROJO warudi kwao na vibwengwe vyao!
Halafu tumewachoka Saaaaaaaaaaaaana!
 
Tuseme wazi, wanasubiri wasikie watu wamechinjwa kutokana na chuki za Ubara na Uzanzibar. Na ndani ya moyo wangu naona wazi hili litaanza Zanzibar, na huku bara watu wataanza kulipa kisasi. Zanzibar wameshaanza kuwaita watu wa bara kule majina ya kudhalilisha na kubagua, na hili limejitokeza sana katika kipindi hiki cha Raisi Samia
Watu wa bara ndio watu gani!? Sema waTanganyika na waZanzibar
 
Sheria iliyounda Senagambia, had provisions za kuuvunja. Ule ulikuwa ni mkataba, the same to UK kujitoa EU.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu ni Muungano wa dhima ya Muungano wa milele, zile Articles of the Union, sio mkataba, ni makubaliano ya milele, hakuna provision ya kuuvunja Muungano, tumeunganisha nchi mbili kwa kuchanganya udongo, na kuumwaga bara na Zanzibar, ili kuuvunja, lazima tuutafute ule udogo, tuupembue, punje za udongo wa Tanganyika, zirejeshwe Tanganyika na punje za Zanzibar zirejeshwe Zanzibar.

Kikemikali, muungano wetu ni compound na sio mixture!. Kikemikali, Ukichanganya vitu viwili na kuwa mixture, vitu hivyo vinakuwa havijaungana kikemikali, mfano kuchanhanya pombe na maji, kwa kutumia fractional distillation inawezekana kuitenganisha pombe na.maji. Vitu kama maji, H2Ounaweza kutenganisha hydrogen na oxygen, chumvi, unaweza hydrogen na.chlorine etc.

Lakini vitu viwili vinapoungana kwa chemical reaction, vitu viwili vile hufa na kuzaliwa kitu kipya kinachoitwa compound, huwezi tena kuvirejesha kwenye hali ya awali kama kuyeyusha sabuni ya unga kwenye maji, kunatokea chemical reaction, huwezi kutenganisha.

Huu Muungano wetu adimu na adhimu, ume undergo chemical reaction kwa mataifa mawili Tanganyika na Zanzibar kuungana, kupoteza utaifa wake.na kuunda taifa jipya la Tanzania ambalo ni compound, halivunjiki tena!.

Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote.
P
Pascal acha kuhadaa watu kwa mifano isiyo na ulinganifu. Hayo ya kuchanganya udongo ni mbwembwe za fikra kiimani ktk siasa kama zilivyo kauli mbinu ktk kuendea jambo fulani kisiasa.

Wapo watu waliounganisha undugu wa hiari kwa kuchanja damu na kuzichanganya ktk miili yao lakini bado undugu ulivunjika na maisha yaliendelea kama ilivyo ktk ndoa wanavyoapa kuwa kitu kimoja lakini bado inavunjika.

pascal acha kupotosha ukweli usemwe na kujadiliwa ili maauzi sahihi yafanyike kwa kuwa na tija ya kitaifa lakini pia kuepusha uhasama utakaokuja kutokea.
 
ila Lumumba imejaza watu wajinga sana , mbona uliyoyaandika hayajibu maswali ya Lissu , siku tukiungana EAC kila raia atakuwa huru kwenda nchi jiran kumiliki lolote pia uhuru wa kuabudu kitu ambacho watanganyika wanakidai kwa Zanzibar

kwann mzenji anamiliki ardhi huku ila sisi hatuwez kwenda kumiliki ardhi kule kwao ?

kwann mzenji anaeza kuwa kiongoz huku bara hata uenyekiti wa kijiji ila si mtanganyika kuwa kiongoz kule zenji ?

kwann wao wana uhuru wa kuabudu huku bara ila sisi wakristo hatuna uhuru wa kufungua sehem za kuabudu kule zenj ?

Zenji ni eneo la kuongeza kura kwa ccmu kipind cha uchaguz

UKIWA MJINGA UNAKUWA MTAJI WA CCMU
Watanzania tuko 61 Million na ardhi yetu ina 945,000 Sqaure kilometres za ukubwa.

Zanzibar wako 1.2 Million na ukubwa wa 2,460 Square kilometres.

Ni aibu leo watu 61 Million kuanza kugombea ki-ardhi kidogo namna hiyo wakati huku kumejaa mapori makubwa ya kutisha.

Hizo fursa za kazi unazozitaka ZNZ ziko wapi? Kama elimu yako na uwezo wako hauwezi kukupatia ajira hapa Bara penye uchumi wa GDP ya USD 85 Billion ndiyo ukabamane na GDP ya ZNZ ambayo USD 3.75??

Tunahitaji kubadilisha mtazamo tu. Tatizo letu kubwa ni umaskini. Zanzibar ingekuwa tajiri kama Qatar, mengi ya yanayosemwa wala isingekuwa issue. Kama sikosei, Area Commissioners from Zanzibar au positions nyingine zimepewa Watu wa upande mwingine wa Mwungano toka enzi za Mwalimu.

Na hizi feelings zikipewa nafasi, zinaweza hata kuleta issues kati ya movements za watu mikoani. Kuna watu, suddenly, watadai wakuu wa mikoa, wilaya, watoke katika mkoa huo huo.

Mikoa kama ya Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro, Arusha ina mchango mkubwa kiuchumi kuliko mikoa mingine kama Tabora, Singida, Kigoma, Mtwara. What if hao wenye uchumi mkubwa wakaona wanannyonywa au kutawaliwa na watu wa mikoa maskini?
 
Watanzania tuko 61 Million na ardhi yetu ina 945,000 Sqaure kilometres za ukubwa.

Zanzibar wako 1.2 Million na ukubwa wa 2,460 Square kilometres.

Ni aibu leo watu 61 Million kuanza kugombea ki-ardhi kidogo namna hiyo wakati huku kumejaa mapori makubwa ya kutisha.

Hizo fursa za kazi unazozitaka ZNZ ziko wapi? Kama elimu yako na uwezo wako hauwezi kukupatia ajira hapa Bara penye uchumi wa GDP ya USD 85 Billion ndiyo ukabamane na GDP ya ZNZ ambayo USD 3.75??

Tunahitaji kubadilisha mtazamo tu. Tatizo letu kubwa ni umaskini. Zanzibar ingekuwa tajiri kama Qatar, mengi ya yanayosemwa wala isingekuwa issue. Kama sikosei, Area Commissioners from Zanzibar au positions nyingine zimepewa Watu wa upande mwingine wa Mwungano toka enzi za Mwalimu.

Na hizi feelings zikipewa nafasi, zinaweza hata kuleta issues kati ya movements za watu mikoani. Kuna watu, suddenly, watadai wakuu wa mikoa, wilaya, watoke katika mkoa huo huo.

Mikoa kama ya Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro, Arusha ina mchango mkubwa kiuchumi kuliko mikoa mingine kama Tabora, Singida, Kigoma, Mtwara. What if hao wenye uchumi mkubwa wakaona wanannyonywa au kutawaliwa na watu wa mikoa maskini?
Ndugu nahisi kama hoja za changamoto za Muungano huu haujazopitia vizuri na kung'amua chanzo chake.

Hoja za kudai ardhi, nafasi za uongozi na fursa kadhaa zinazungumzwa na watu wa bara kwa kuwa wananchi wa wanzanzibar na viongozi wao tena wakiwemo wa ccm wanapaza sauti ya kudai wawe na mamlaka kamili, lakini pia wakidai kuwa Tanzania bara inainyonya zanzibar, rejea hata jinsi Rais wa Zanzibar alivyowahi kuivimbia serikali ya Muungano juu ya deni la umeme. Kwa ufupi wanzanzibar wamechoka na Muungano huu na tunavyoendelea kulazimisha ndivyo wanavyotaka na makubwa zaidi. Ndiyo maana sasa ifike kikomo kuwe mjadala huru juu ya namna bora ya kuwa na Muungano huu ama turejed ktk kuchakata katiba mpya au mazungumzo makhushu na ya kina juu ya Muungano yafanyike
 
Ndugu nahisi kama hoja za changamoto za Muungano huu haujazopitia vizuri na kung'amua chanzo chake.

Hoja za kudai ardhi, nafasi za uongozi na fursa kadhaa zinazungumzwa na watu wa bara kwa kuwa wananchi wa wanzanzibar na viongozi wao tena wakiwemo wa ccm wanapaza sauti ya kudai wawe na mamlaka kamili, lakini pia wakidai kuwa Tanzania bara inainyonya zanzibar, rejea hata jinsi Rais wa Zanzibar alivyowahi kuivimbia serikali ya Muungano juu ya deni la umeme. Kwa ufupi wanzanzibar wamechoka na Muungano huu na tunavyoendelea kulazimisha ndivyo wanavyotaka na makubwa zaidi. Ndiyo maana sasa ifike kikomo kuwe mjadala huru juu ya namna bora ya kuwa na Muungano huu ama turejed ktk kuchakata katiba mpya au mazungumzo makhushu na ya kina juu ya Muungano yafanyike
Bado hivyo vitu ni peanut sana kuliko strategic position tuliyonayo. Kuwaacha ZNZ wawe available kwa mshirika mwingine kama Alshabab ni risk kwa nchi yetu.

Hizo gharama za umeme sijui na mgawo wa fedha inazopewa ZNZ ndizo opportunity cost ya Muungano.

Duniani kote hakuna watu wanaopenda Muungano iwe Russia, USA au Sudan.

Leo ZNZ ikijitoa na tukaiacha, itakuja mikoa yenye uchumi mkubwa kama Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na Arusha. Watadai wananyonywa na mikoa ya Singida, Lindi na Mtwara hivyo wanadai kujitenga.

Watakuja Kagera watakuambia wao ni watu wa Uganda wanataka warudi kule kwa kuwa Nyerere aliwaleta kwa lazima.

Hizi hoja hazina mashiko zaidi ya kuwapa umaarufu wanasiasa.

Nimezaliwa miaka 4 kabla ya Muungano na sasa ni mstaafu, sioni faida yeyote tutakayoipata tukiwa bila ZNZ.

Na hao ZNZ wasijifanganye kuwa watapiga hatua kuwa kama DUBAI eti kwa sababu ni kisiwa. Mbona Comoros, Seychelles na Mauritius bado haziko kama Dubai au Qatar.

Kwenye geopolitics sehemu ambayo iko strategic kupata biashara ni Eritrea na Djibouti.

Ni nani apeleke meli zake Zanzibar Port na aache kuleta Dar Port ambako kuna ndiko kuna mizigo inapaswa kufika nankutawanyika kwenda nchi 8 zinazotuzunguka?
 
N
Bado hivyo vitu ni peanut sana kuliko strategic position tuliyonayo. Kuwaacha ZNZ wawe available kwa mshirika mwingine kama Alshabab ni risk kwa nchi yetu.

Hizo gharama za umeme sijui na mgawo wa fedha inazopewa ZNZ ndizo opportunity cost ya Muungano.

Duniani kote hakuna watu wanaopenda Muungano iwe Russia, USA au Sudan.

Leo ZNZ ikijitoa na tukaiacha, itakuja mikoa yenye uchumi mkubwa kama Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na Arusha. Watadai wananyonywa na mikoa ya Singida, Lindi na Mtwara hivyo wanadai kujitenga.

Watakuja Kagera watakuambia wao ni watu wa Uganda wanataka warudi kule kwa kuwa Nyerere aliwaleta kwa lazima.

Hizi hoja hazina mashiko zaidi ya kuwapa umaarufu wanasiasa.

Nimezaliwa miaka 4 kabla ya Muungano na sasa ni mstaafu, sioni faida yeyote tutakayoipata tukiwa bila ZNZ.

Na hao ZNZ wasijifanganye kuwa watapiga hatua kuwa kama DUBAI eti kwa sababu ni kisiwa. Mbona Comoros, Seychelles na Mauritius bado haziko kama Dubai au Qatar.

Kwenye geopolitics sehemu ambayo iko strategic kupata biashara ni Eritrea na Djibouti.

Ni nani apeleke meli zake Zanzibar Port na aache kuleta Dar Port ambako kuna ndiko kuna mizigo inapaswa kufika nankutawanyika kwenda nchi 8 zinazotuzunguka
 
Bado hivyo vitu ni peanut sana kuliko strategic position tuliyonayo. Kuwaacha ZNZ wawe available kwa mshirika mwingine kama Alshabab ni risk kwa nchi yetu.

Hizo gharama za umeme sijui na mgawo wa fedha inazopewa ZNZ ndizo opportunity cost ya Muungano.

Duniani kote hakuna watu wanaopenda Muungano iwe Russia, USA au Sudan.

Leo ZNZ ikijitoa na tukaiacha, itakuja mikoa yenye uchumi mkubwa kama Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro na Arusha. Watadai wananyonywa na mikoa ya Singida, Lindi na Mtwara hivyo wanadai kujitenga.

Watakuja Kagera watakuambia wao ni watu wa Uganda wanataka warudi kule kwa kuwa Nyerere aliwaleta kwa lazima.

Hizi hoja hazina mashiko zaidi ya kuwapa umaarufu wanasiasa.

Nimezaliwa miaka 4 kabla ya Muungano na sasa ni mstaafu, sioni faida yeyote tutakayoipata tukiwa bila ZNZ.

Na hao ZNZ wasijifanganye kuwa watapiga hatua kuwa kama DUBAI eti kwa sababu ni kisiwa. Mbona Comoros, Seychelles na Mauritius bado haziko kama Dubai au Qatar.

Kwenye geopolitics sehemu ambayo iko strategic kupata biashara ni Eritrea na Djibouti.

Ni nani apeleke meli zake Zanzibar Port na aache kuleta Dar Port ambako kuna ndiko kuna mizigo inapaswa kufika nankutawanyika kwenda nchi 8 zinazotuzunguka?
Hizi hisia ni za zamani sana kwamba Zanzibar ikiachwa itaangukia kwa alshababi. Tukubali kuwa Dunia imesonga mbele na siyo kama zamani. Umetoa mfano mzuri kuwa vipo visiwa vya usheli na comoro ambvyo vipo jirani na vipo salama kwamba havina hao maadui je woga huo kwetu unatoka wapi. Lakini pia ujue hauwezi endelea kukaa na mtu asiyekutaka ukadhani utamtawala milele siku ya kutoka ni vita kama Urusi na ukraine je ndivyo unataka itokee

Ama kuleta hii mifano ya mikoa yenye uchumi kujitenga bado unatembelea kivuli cha Nyerere ambacho kwa wakati ule ilikuwa sahihi lakini pia uelewe Zanzibar tayari ni nchi iliyo na Rais, tamaduni, na mambo mengi ya ki mamlaka kama nchi, hivyo mfano huo hauwezi kuwa halisi kwa mikoa ya bara kujitenga.
 
kunizuia mimi mtz mwenzio kumiliki ardhi huko kwenu huo sio ubaguz ila mimi kukutaka urudi kwenu nami nimiliki ardhi yangu huu ndo ubaguz si ndio ?

JINO KWA JINO MPK AKILI ZIWAKAE
Duh 🙄 !
 
Back
Top Bottom