Uhusiano kati ya midori na vioja ndani ya nyumba

Uhusiano kati ya midori na vioja ndani ya nyumba

Movie zimekuharibu wewe na uyo jirani yako.
Kwa majukumu niliyonayo mkuu sina muda wa kutazama movie yoyote ile,amini hivyo kuwa jirani yangu alipatwa na maswaibu hayo maana hata niwe busy namna gani lazima nijue kuna shida gani kwa wapangaji,majirani na wazazi wangu wa pande zote ila sio movie.
 
Hayaja kukuta wewe bado mdogo kwa mambo ya elimu ya giza. Laiti yangelikukuta siku moja ungepata kuamini Tafuta Mdoli wowote uliopo nyumbani kwako kisha ushike na kusema maneno haya kila siku sema maneno haya ''wewe blodmeli nibadilishie kinyago hiki'' kwa siku 41 halafu njoo hapa ulete mrejsho wako usije kuikimbia nyumba unayoishi.
Mkuu; Naomba unifafanulie kwamba utataka huyo blodmeli akubadilishie kinyago hicho kuwa kitu gani? i.e. utataka kibadilishwe na kuwa e.g. mtu anayeongea, ndege atakaye imba usiku n.k.? au inakuwaje atabadili kama atakavyo yeye huyo Blodmeli? Tafadhali fafanua kidogo.
 
Nasema haiwezekani kifaa kitengenezwe kwa mbao au plastic useme eti ina shida?

Majini, Shetani na Binadamu ni Roho/Nafsi wakati hiyo midoli ni vifaa vinatengenezwa kwa material ya kawaida tu

Tulichokatazwa kwa Waislam na Wakristo ni KUABUDU au KUSUJUDIA HIZO SANAMU NA MIDOLI BADALA YA MUNGU PEKEE

Hivi vingine mnavyotuletea ni Uongo na Uzushi.
Ningekushauri unaonaje ukafanya utafiti aka kujaribu ili upate kuhakikisha kama ni kweli majini wanaweza kujigeuza midoli, nyoka mende, paka mweusi mbwa mweusi Nge na hata kujigeuza binadamu kwa imani yetu sisi Waislam tumefundishwa hivyo. Sijuwi wewe ni Mkristo au muislam? kw aimani yako wewe huamini shetani kujigeuza kuwa midoli ? Ndio maana kiongozi wetu wa waislam Mtume Muhammad rehema za Mungu ziwe juu yake pamoja na amani amekataza kuweka katika nyumba vinyago,midoli, picha ukutani na amsema kuw anyumba yenye vitu hivyo hawezi kuingia malaika wa rehema. Utakuw aunamuomba Mungu lakini malaika wanataka kuja kupokea maombi yako wanashindwa kuingia katika nyumba iliyomomo midoli,vinyago,na picha za ukutani ziwe picha za wanyama au picha za binadamu. Siwezi kukulazimisha uniamini kila mtu Mungu amempa akili yake ya kuweza kuitumia ukiamini sawa usipo amini pia sawa ninakuacha kama ulivyo. Lakini mimi ninaamini shetani anawezakujigeuza anavyotaka iwe kuingia katika midoli au nyoka au mende wakati wa usiku au nge au paka mweusi au mbwa mweusi au hata shetani anaweza kujigeuza kuwa ni binadamu na akakujia na kuzungumza na wewe na akaondoka zake, Na wewe pasipo na kumjuwa kama ni shetani aliyekuja kuzungumza na wewe kazi kwako.
 

Pengine Unamsikia tu Shetani Juu juu. Humfahamu Vizuri na Unasema ni Adui Yako.​

Pengine unamsikia tu shetani juu juu, humfahamu vizuri na unasema ni adui yako.

Unawezaje kupambana na adui usiyeijua nguvu yake?

Anafafanua kwa ufupi Mwl . Makungu m.s
0743781910

Kamwe Usimfananishe shetani na majini , mapepo , mizimu wachawi n.k. Ambao una uwezo wa kufanya nao vita kirahisi tu hata kwa kuweka mfupa wa nguruwe mlangoni na harufu ya bangi ndani ya chumba..

Unapotaka kufanya vita na adui ili umshinde kwanza elewa uwezo wake na mifumo yake inavyofanya kazi..

Umewahi kujiuliza kwann majini na mapepo yalikuwa yakimuona Yesu yanahangaika,yanapiga kelele, yanagalagala, yananywea na kukimbia lkn shetani alikaa na Yesu wakapiga story, wakajadili vifungu vya biblia na kubishana kwa hoja kwa siku 40 nyikani? ( Soma Vitabu vya injili).

Umewahi kujiuliza iliwezekanaje shetani aliyepigwa pmj na jeshi lake kule mbinguni akafukuzwa akatupwa duniani, lkn wana wa Mungu (wako wengi siyo Yesu tu-ntakufafanulia ktk andiko lijalo) walipokuwa wanakwenda kujihudhurisha mbele za Mungu mara kadhaa siku tofauti tofauti shetani pia alikuwa anajumuika pamoja nao katkat yao mbele za Mungu na wale wana wa Mungu wala hawakumfukuza na Mungu alipomuona wakajadiliana naye juu ya mustakabari wa wanadamu duniani. (Soma kitabu cha Ayubu) .

Na unajua mwisho wa siku Mungu alimwambia nini shetani juu ya Ayubu? Alimruhusu shetani amfanyie mambo / mapigo yote anayotaka lkn kasoro jambo moja tu "asiitoe roho yake".
Hii maana yake nini? Mungu akikaa pembeni , Shetani ana uwezo wa kutoa roho ya mtu.
Kwahiyo wale ambao hata wakiona watu wamekufa kinyama kwenye ajali wanakimbilia kusema " kazi ya Mungu haina makosa . Ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu" , Jiepusheni kumsingizia Mungu Kila kitu . Kazi nyingine ni kazi za shetani zina makosa...

Shetani ni adui yako mkubwa unayepambana naye kwahiyo unatakiwa kumfahamu vizuri.

Shetani Kabla hajaasi mbinguni na kuwa shetani Alikuwa ni malaika mkuu anayeitwa jina zuri lenye utukufu Lucifer ( Nyota ya asubuhi) .

Alikuwa na uwezo mkubwa Sana wa ajabu kuzidi malaika wengine wote aliopewa na Mungu mwenyewe mpk akajiona Kama yupo sawa na Mungu . Na ndiyo maana robo tatu ya malaika ilimuamini na ikaamua kuungana naye kupigana na Mungu. Wakiamini Lucifer atashinda .

Wanadamu wanaimba mpk sauti ya 4 . Lkn unaambiwa Lucifer Alikuwa anaimba sauti mpk sauti ya 12 peke yake..

Akinyanyua mabawa yake akiyashusha zinalia sauti za vinanda tupu.

Alikuwa ndiyo kiumbe wa karibu Sana na Mungu kuliko malaika wengine . Maana yake Ni kuwa alimuelewa na kuielewa mipango mingi ya Mungu.

Aikuwa ni Kama waziri mkuu ktk serikali ya mbinguni . Kwahiyo Alikuwa na mamlaka makubwa ktk kuiendesha ile serikali ..
Na tafsiri nyingine Ni kuwa alielewa Siri nyingi za serikali ya mbinguni..

Mungu ni roho , shetani ni roho na malaika ni roho ( hawana umbo maalumu lkn wana uwezo wa kujiweka na kujigeuza ktk umbo lolote ..
Na mwanadamu wa kwanza kabisa kuumbwa aliumbwa ktk umbo la mwanadamu lkn lenye roho ya uungu (nusu Mungu) ndani yake.. Ndiyo maana Alikuwa na uwezo wa kakaa nao na kuzungumza nao wanyama na miti na wakaelewana..

Najua hujanielewa vizuri hapo . Ngoja nikupe hii.
Mungu aliumba vitu vyote kwa kutamka neno tu na kwa kutumia umoja , yaani " na liwepo anga ,likawa". Lakini ilipofika muda wa kumuumba mwanadamu Mungu hakutumia neno tu na aliongea kwa nafsi ya wingi.

Yaani " na tumfanye mtu kwa mfano wetu " .
Unajua Alikuwa anawaambia wakina Nani ?
Na huo mfano ni wa sura au jinsia pekee?
Na unajua kwann shetani alichukia kuumbwa mwanadamu?

- kwanza uelewe mwanadamu aliumbwa ile siku ya 6 ya uumbaji baada ya Mungu kuwa kaumba vitu vyote vya msingi kabakiza vichache. Ilikuwa Siku 1 kabla ya kupumzika . Na shetani alichukia kuumbwa mwanadamu . Hii maana yake ni kuwa wakati mwanadamu anaumbwa tayari mbinguni kulikuwa na viumbe tyr vimeshaumbwa ( malaika) na shetani (Lucifer) ndiyo alikuwa malaika mkuu . Soma Mwanzo sura ya 2 ..

"Na tumfanye mtu kwa mfano wetu"..

-Mungu anasema "na tumfanye mtu kwa mfano wetu". Siyo sura pekee yake au jinsia bali ni mtu mwenye nusu uungu na uwezo ndani yake Kama walivyo wao kule mbinguni. Ndiyo maana shetani alichukia maana Mungu alihamishia mapenzi kwa mwanadamu kuliko kwa malaika.

Nimegusia jinsia hapo juu. Biblia haijawahi kusema Kama Mungu ana jinsia . Lkn biblia inaweka wazi kuwa wana wa Mungu wana jinsia .. Tukianzia na Yesu . Na wale wana wa Mungu walioshuka duniani nyakati za Nuhu na wakavutiwa na binti za wanadamu na wakawaoa wakazaa nao ,wakazaliwa watu wenye uwezo wa ajabu ,hodari na majitu (Giants) wanefili.. (soma Mwanzo 6:1> )... Japokuwa ktk jambo hili la kitheolojia kuna nadharia 2 zinapingana na Kila mmoja ameachwa aamini nadharia anayoitaka yeye.. Wapo wanaoamini wana wa Mungu walioshuka na kuzaa na wanadamu zama hizo walikuwa ni malaika toka mbinguni.. Na wapo wanaoamini wana wa Mungu hao walikuwa ni watoto wa uzao wa Sethi wacha Mungu wa Kipindi kile .. Biblia haijafafanua kwa uwazi tofauti ya wana wa Mungu waliotajwa ktk Ayubu na hawa waliotajwa nyakati za Nuhu.
Swali la kujiuliza na kujiongeza Ni kuwa " kwann baada ya wana wa Mungu hawa kuzaa na wanadamu walizaliwa binadamu wenye sifa na uwezo mkubwa tofauti na binadamu wa kawaida"?

Shetani anaijua vizuri biblia kuliko unavyoijua wewe . Ndiyo maana Alikuwa anabishana na Yesu kwa vifungu. Na anaitumia Kila siku ili apate njia za kukupoteza wewe kwa kutumia hiyo hiyo biblia.
Kwahiyo kama unadhani unaweza kumtisha shetani kwa kuishika biblia au rozali au msalaba bila kuwepo na roho ya Mungu pembeni yako unajidanganya.

- Huwa tunayatoa mapepo na majini ndani ya mtu na wakati mwingine yanajitaja Hadi majina ( makata,subiani,maimuna,n.k) . Lkn Ulishawahi kusikia tumemtoa shetani ndani ya mwili wa mtu na akajitaja na jina kuwa mm ni Lucifer?

Sisi watu wa Tanga na Zanzibar kuna wakati Huwa tunakutana na majini tunayaona live . Lkn nani aliishawahi kukutana na Lucifer?

- Mungu anamwambia Musa " hakuna mwanadamu atakayeniona akaishi" .
Pengine hii ni sababu ya pili iliyomfanya Musa afe mapema .. baada ya Musa kung'ang'ania Sana kutaka kumuona Mungu sura yake , Mungu alimziba Musa macho na alipopita akamuachia Musa akamuona kisogo na mgongo..

Shetani naye huiga Kila kitu kinachoendeshwa ktk ufalme wa Mungu . Kwahiyo huwezi kumuona Lucifer wewe na imani yako ndogo hiyo.

Shetani na malaika zake pamoja na kumuasi Mungu ,walipigwa kule mbinguni lakini hawakuuliwa. Zingatia neno " hawakuuliwa" . Wakatupwa duniani .
Tena Biblia inasema " Ole ole kwa wanadamu maana yule mshitaki wenu ametupwa kwenu " .. Na ukumbuke ana hasira za kupigwa.
- Mwanadamu alipomuasi Mungu Kipindi cha Nuhu akafutwa na gharika . Kipindi cha sodoma akafutwa na moto .. Lkn shetani hakuuliwa alitupwa kwetu .

Huyo ndiyo adui unayeshindana naye wewe.. Umjue jinsi alivyo . Sijui km unanielewa..

Shetani alipotupwa duniani hakuna sehemu Biblia inasema kuwa aliondolewa au kunyang'anywa zile nguvu zake na uwezo wake mkubwa aliokuwa nao mbinguni kuliko malaika wote .. Uwezo uliomfanya yeye ajione ni Kama Mungu .
Sasa fikiria huyo ndiyo kiumbe unashindana naye wewe ..

Ndugu yangu bila uwepo wa roho ya Mungu ndani yako na pembeni yako , utamchukia shetani tu lkn hutaweza hata kuligusa tu pindo la vazi lake . Tena siyo wewe utakayeshughulika naye ,ni Mungu mwenyewe.

Shetani anapenda ukuu, utukufu , na kuabudiwa km Mungu anavyoabudiwa.

Shetani Anapenda usafi , harufu nzuri za pafyumu, marashi ,udi , uvumba, manemane na marhamu . Kama vile tu Mungu anavyopenda . ( Soma torati ya Musa). Ndiyo maana majini yananukia kupita kiasi..

Anapenda damu na nyama kupita kiasi kuliko sadaka yoyote ile . Kama vile tu Mungu alivyokuwa anapenda Kabla ya kifo cha Yesu . ( Soma Agano la kale uone jinsi Mungu alivyokuwa anapenda damu na harufu nzuri ya nyama ya kuchoma km sadaka ) . Mungu aliacha ila shetani ameendeleza . Unajua kwann ? Damu huwa inaongeza nguvu na uwezo kwa viumbe vilivyo ktk ulimwengu wa roho. Kawaulize wachawi wanapotaka kuboost nguvu zao wanafanya nn..

Hakuna kiumbe kinachomfikia shetani kwa uzuri wa sura anapokuwa ktk umbile la kimwili.. unawakumbuka wale malaika walioenda kwa lutu kule sodoma na gomora jinsi walivyokuwa wanawavutia wale wajinga wa sodoma wenye ushetani ? Basi Lucifer kabla hajawa shetani ndiyo alikuwaga kiongozi wao kule mbinguni na hakuna malaika Aliyekuwa anamzidi kwa lolote.
Huwa tunafanya makosa Sana kumchora shetani na sura ya kutisha kiasi kwamba watoto wanakariri hivyo na inakuwa rahisi kuanguka ktk dhambi ya uzinzi maana wanakutana na sura nzuri nzuri tu bila kujua kuwa hao ndiyo vibaraka wa Shetani wapo kazini ..

Shetani anao uwezo wa kufanya miujiza ya kumponya mtu ( soma ufunuo atagundua mengi) ..
Ndiyo maana leo hii yapo baadhi ya makanisa yanayotilia mashaka ktk miujiza wanayofanya.
Kama unalijua neno la Mungu unawagundua kirahisi.

Shetani anao uwezo wa kumtoa mtu mapepo /majini. Pitia habari za beerizebuli ktk injili utagundua hilo..
kwahiyo usidanganywe na miujiza ya mtu , mpime huyo mtu kwanza.

Shetani anao uwezo wa kumpa mtu mafanikio . Na hilo linajionesha wazi kabisa ktk mahojiano yake na Yesu kule nyikani..
Kwahiyo usitamani mafanikio ya mtu bila kujua kayatoa wapi?

Shetani anao uwezo mkubwa wa ubunifu wa kisayansi na kiteknolojia. Na wanadamu wengi tunaingia kwny mitego ya shetani anayetumia akili nyingi kwa ujanja sana..
Ndani humo humo ya teknolojia nzuri tu kunakuwa na kajambo kadogo tu ka kishetani ndani yake.. Anachotaka ni kuona watu wanafanya kinyume na maagizo ya Mungu anavyotaka. Na kwa kuwa watu wengi hawasomi maandiko basi hawajui iwapasavyo kuenenda na wanapotea..

Tawala nyingi, mamlaka na falme za duniani zipo chini ya/ zinaendeshwa na shetani Lucifer. Rejea maagizo ya shetani kwa Yesu kule nyikani. Shetani huzishikilia tawala za dunia ili maamuzi yanayopitishwa na tawala hizo yawe ni ya kumkufuru Mungu na kumtukuza yeye. Ndiyo maana leo Kuna mambo km ya haki za ndoa za jinsia moja . Soma vizuri habari za mnyama ktk kitabu cha Ufunuo utaelewa.

Huyo ndiyo shetani Lucifer tunayedhani tunapambana naye direct kumbe tunapambana na vibaraka wake tu ..

ANGALIZO MUHIMU
Andiko hili halijaandikwa ili kumsifia shetani ,bali kuelezea ukweli halisi wa Shetani ( Lucifer) ili kukufanya ndugu mpendwa kujua nguvu ya adui unayepambana naye .
Ukiijua nguvu na uwezo na mbinu zake utajua jinsi ya kumkwepa/ kupambana naye..
Na usipambane na shetani bali mkwepe au muite Mungu apambane naye kwaajili yako.. Wewe Huna uwezo wa kupambana na Lucifer peke yako..

Makungu m.s
0743781910
 

JINSI SHETANI ANAVYOFUNGA MWILI:​

Na Mchungaji: Josephat Gwajima.
Shetani ana mbinu nyingi za kumfunga mtu, na ndio maana Biblia inasema 2Wakorintho 2:11 “Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.” Kwa maana hiyo imetupasa kujua mbinu anazotumia shetani, ili kuufunga mwili wa mwanadamu. Watu wengi wanasumbuliwa na vifungo vya mwilini, ikiwemo magonjwa mbalimbali hii ni kwasababu ya kutokujua siri hii, kuwa mwili ni udongo. Sasa tuone njia ambazo shetani hutumia kuufunga mwili, ambao kwa asili ni udongo, tofauti yake na udongo wa kawaida ni kwamba mwili uliwahi kushikwa na Mungu, pili mwili wa binadamu unauhai unao upata kutoka kwenye roho: njia kadhaa anazotumia shetani...

i) Kupanda na Kung’oa:
Mhubiri 12:7 “Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.” Kama tulivyoona toka mwanzo kuwa mwili ni udongo, na kwamaana hiyo, unavyoweza kuutendea udongo wa kawaida ndivyo hata mwili nao waweza kuutendewa vivyo hivyo katika ulimwengu wa roho. Kwenye udongo wa kawaida watu hupanda na kung’oa, kwahiyo na kwenye mwili ambao ni udongo kunaweza kupanda vitu mbalimbali.
Biblia inasema Mungu ni roho (Yohana 4:24), lakini pamoja na hilo kwamba ni roho aliweza kupanda bustani katika kitabu cha Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.” Ingawa Mungu alikuwa roho lakini aliweza kupanda bustani, na maandiko mengine kuonyesha BWANA aweza kupanda
(Zaburi 104:16; Hesabu 24:6). Kumbe roho zaweza kupanda na ndio maana katika Mathayo 15:13 “Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa.” Kumbe kuna mapando ambayo hayajapandwa na Mungu, na yanatakiwa yang’olewe. Hapa tunafundishwa kuwa kuna uwezekano wa mwili wa binadamu ambao ni udongo, kupandiwa vitu kama udongo wa kawaida.

Ayubu 4:8, Shetani ni mkulima analima maovu, na kupanda madhara. Mwili wa binadamu unaweza kupandiwa mmea au mti. Na ndio maana mtu anaweza kuwa safi rohoni na nafsini, lakini kumbe kwenye mwili wake amepandiwa vitu. Kwa namna hii shetani amefunga miili ya watu wengi sana bila ya wao kujua, ukifunguliwa macho ya rohoni ukaona utagundua kuwa watu wengi wamefungwa kwa jinsi hii. Na biblia inasema kwa muda nchi idumupo majira ya kupanda na kuvuna hayatakoma (Mwanzo 8:22), hivyo dunia imekaa katika kupanda na kuvuna.
Tunaweza kujifunza zaidi katika hili, kwenye Mambo ya walawi 19:19 “…usipande shamba lako mbegu za namna mbili pamoja;…” utajiuliza kwanini Mungu aliyasema haya kwenye torati, kimsingi torati asili yake ni ya rohoni Warumi 7:14 “…torati asili yake ni ya rohoni;…” sasa basi hayo Mungu aliagiza kuonyesha kuwa kuna uwezekana kwenye udongo kukapandwa pando la kiMungu au la shetani. Maana ya maneno haya ni kwamba pale ambapo Mungu amepanda shetani hatakiwi kupanda, Mfano, Ukiokoka Mungu anakupandia mbegu ya amani, upendo, furaha na afya. Hapo shetani hatakiwi kupanda mbegu yake, na hapo andiko la kila pando asilolipanda Mungu, litangolewa linapoleta maana.
Asili mia kubwa ya magonjwa yanayowapata watu, ni matokeo ya mapando ya rohoni. Mtu anaweza akawa anaonekana kwa nje amepooza kumbe kwenye mwili wake amepandiwa mti. Na pepo wamekaa kwenye mwili wake kama mti.
ii) Pepo anaweza kugeuka na kuwa:
Shetani na mapepo wachafu wote ni roho, na wanafanya kazi katika ulimwengu waroho. Na kwa hivyo kuna sifa ambazo wanazo zinazowatofautisha na wanadamu ojawapo ni uwezo wa kujibadilisha kwenye maumbo mbalimbali. Ukisoma kitabu cha 1wafalme 22:19-23 “…Akatokapepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo...” Tunaona huyu pepo, hakuwa pepo wa uongo lakini aliweza alijibadili na kuwa pepo wa uongo. Kumbe kimsingi shetani na mapepo yanaweza kujibadili na kuwa umbo wanalotaka.
Kama tulivyoona kuwa mwili wa binadamu ni udongo, na kwenye udongo waweza kuchoma vitu kama kisu, kunawanyama wanatambaa, mimea inaota na hatakuchimba shimo. Hivyo mapepo wao wapo katika ulimwengu wa roho kwahivyo wakiuangalia mwili wanaona ni udongo kabisa, sasa wanapotumwa na mchawi au mganga wa kienyeji, wanakuja na kujiuza na kuwa kitu kile walichotumwa kufanya. Mfano, waweza kumkuta mtu analalamika kuwa kuna vitu vinatembea kwenye mwili, kumbe ni pepo kajigeuza akawa mnyama atambaaye, mtu anawashwa mwili kumbe mmea wa upupu au mwili unachoma kumbe pepo kajigeuza na kuwa kisu. Shetani yupo na anatenda kazi ya kufunga miili kwa namna hiyo.
Pepo anaweza kujibadili na kisu cha kuchoma moyo, na matokeo yake utamwona mtu huyu anakuwa na uchungu au anakosa amani kila wakati. Jambo linaweza kuwa dogo tu lakini likamuumiza sana moyo, kumbe kuna pepo aliyejibadili na kuwa kisu. Kinachofanyika ni kwamba pepo ametumwa na kunuiziwa awe kisu, hivyo anabadilika na kuwa kisu kwenye moyo ili usione amani kwenye maisha. Na watu namna hii wasipopata msaada wa haraka hufikia kujiua.
iii) Kufunikwa uso:
Kama tulivyoona kuwa pepo aweza kujigeuza na kuwa. Njia hiyo shetani huitumia kufunika uso. Na ndio maana mtu anawezasema ana roho ya kukataliwa kumbe pepo amekuja usoni na kujigeuza kuwa sura nyingine kabisa. Na mpo mtu mwingine anapoongea naye yaani hisia tu zinakuja, kuwa anaongea na kitu kingine, kwa njia hiyo watu wanaanza kujitenga naye. Kumbe ni pepo aliyejigeuza na kuwa uso bandia.
Tabia ndiyo ambayo Yule pepo kwenye kitabu cha (1wafalme 22:19-23). Alivyofanya. Kumbe unaweza kumuona mtu anatukana matusi ya ajabu kumbe pepo kajigeuza kuwa kinywa chake usoni. Mapepo waweza kujigeuza maumbo mbalimbali, kama nyani, samba, paka hata bundi ilimradi kuharibu hatma ya mtu. Mnamkuta dada aolewi kumbe uso wake umefunikwa kwa sura ya simba, kila mwanaume anayetaka kumchumbia haoni sura nzuri bali anaona simba. Na ndio maana kuna baadhi ya wadada watumia muda mwingi kufanya kujipodoa lakini bado, kumbe wamefunikwa.

"KWA KUSUDI HILI MWANA WA ADAMU ALIDHIHILISHWA, ILI AZIVUNJE KAZI ZOTE ZA IBILISI"
 
Mkuu; Naomba unifafanulie kwamba utataka huyo blodmeli akubadilishie kinyago hicho kuwa kitu gani? i.e. utataka kibadilishwe na kuwa e.g. mtu anayeongea, ndege atakaye imba usiku n.k.? au inakuwaje atabadili kama atakavyo yeye huyo Blodmeli? Tafadhali fafanua kidogo.
utataka vile unavyo taka wewe kiwe active aka kinafanya kazi il unayotaka wewe. Anakuwa ni shetani upo nae ndani ya nyumba yako utakuwa unamtumia vile kama unavyotaka wewe anakuwa kama vile ni robot yako. Huyo shetani anakuwa kama huyu ROBOT SOFIA MDOLI.




 
Jf umesoma threads zote na ku-reply jf na majukwaa yake yote? Utapungukiwa na nini endapo hautajihusisha na uzi huu kama nyuzi zingine?
Mkuu unashindana na mtoto mdogo hebu ona hiyo picha yake kishandio uweze kuzngumza nae huyo kiakili bado mtoto mdogo sana kutokana jinsi anavyobisha mambo yapo wazi nimesha mwambia ajaribu kumuweka mdoli ndani ya nyumba yake kisha kuna maneno nimemfundisha ayaseme kwa siku 41 kisha atapata majibu yake kama kweli midoli aka vinyago vinaweza kujigeuza mashetani au uongo? Achana nae usibishane na mtoto mdogo na wewe utakuwa ni mtoto mdogo mwache abishe tu.
 
Habari wakuu
Kumekuwa na kawaida katika nyumba mbalimbali iwe masebuleni au vyumbani midori ikionekana imesheheni, baadhi hupamba midori katika meza na makabati, wengine huthubutu hata kuwa na midori vitandani au katika viti (sofa) ikiwa lengo ni kukufanya ujisikie raha fulani hivi unapoongea na ndugu, jamaa au marafiki pale unapomshikashika huyo mdori iwe kwa kumvuta sikio, ulimi ama mkia, na kila mtu huwa na upendeleo wa aina ya mdori kuwa nao ndani baadhi hupenda midori ya ndege mbalimbali mpaka bundi,na midori ya wanyama mpaka fisi.

KISA: Wiki iliyopita jirani yangu alipatwa na sintofahamu yenye ushabiihano na midori,ilifikia wakati akilala husikia kama vitu vinacheza cheza sebuleni,mara chakula kuliwa na asiyejulikana n.k.

Siku moja akaamua kuchungulia akiwa ametoka chumbani na kuiona midori ipo bize na kuruka ruka,alipojitokeza sebuleni midori yote ilirejea sehemu yake.

Alipoirudisha midori hiyo alikoinunua ndio ukawa mwisho wa tatizo.

Naomba kujuzwa kuna uhusiano gani kati ya midori na mauzauza hayo.
Huyo aliangalia muvi ya kutisha muda mfupi kabla hajaenda kulala
 
utataka vile unavyo taka wewe kiwe active aka kinafanya kazi il unayotaka wewe. Anakuwa ni shetani upo nae ndani ya nyumba yako utakuwa unamtumia vile kama unavyotaka wewe anakuwa kama vile ni robot yako. Huyo shetani anakuwa kama huyu ROBOT SOFIA MDOLI.




View attachment 2843807
Shukran Mkuu. Nimeelewa.
 
Nimemkumbuka timmy kwenye tamthilia ya passions 😁
Na Bibi yake Tabitha,,ITV Saa NNE na nusu Usiku,,jtatu Hadi alhamisi,,marudio jumamosi ya wiki zima kuanzia Saa nne asubuhi hadi saa saba mchana,,daahhh Wandafuli memorizii
 
Back
Top Bottom