Uhusiano Na Hizbu-ccm Vs Cuf Nani Mkweli?

Uhusiano Na Hizbu-ccm Vs Cuf Nani Mkweli?

Si unaona hii habari Kibunango?
Especially pale nilipo highlight?

Sakata la mwafaka Zanzibar

2008-05-18 11:44:05
Na Simon Mhina


Chama cha Wananchi (CUF), kimesema kauli ya Rais Jakaya Kikwete ya kukitaka chama hicho kurejea kwenye meza ya mazungumzo na CCM, wanaichukulia kama porojo, vinginevyo ayatoe kimaandishi.

Kadhalika, Chama hicho kimesisitiza kuwa hakitakubali kamwe kukaa meza moja tena na Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuf Makamba kuzungumzia Mwafaka.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni Bw. Hamad Rashid Mohamed, alisema habari za Rais kuwaomba CUF warejee kwenye mazungumzo wamezisikia kwenye Redio na magazeti, hivyo hawajazitilia maanani.

Alisema hivi sasa CUF imeshachoka `kutapeliwa` kisiasa na CCM hivyo hawakubali maneno yoyote yasipopelekwa kwao kwa maandishi.

Alisema akiwa Mkuu wa Nchi, inashangaza kuona anatoa maagizo mazito yanayogusa ustawi wa Taifa, kupitia mlango wa nyuma.

Alisema Rais alikuwa na uwezo wa kuwasiliana nao moja kwa moja, badala ya kutoa maagizo hayo wakati anazungumza na Waziri anayeshughulikia mambo ya kimataifa wa Serikali ya Ufaransa aliyemtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

``Anavyosema CUF na CCM tukutane, wakati anazungumza na mfaransa huyo, alikuwa anamtuma aje atuambie au vipi?``alihoji.

Bw. Mohamed alisema kwa kiasi kikubwa CUF wanamheshimu mno Rais Kikwete na hawakusudii kupuuza wala kudharau mawazo yake.

Alisema ni kweli Rais akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu, anao wajibu wa kuhangaika ili kuhakikisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakuwa ya amani.

``Tunamheshimu Rais Kikwete, lakini anapotoa maagizo makubwa kama hayo katika vyombo vya habari, kwa kweli tunabaki tunashangaa, maana hata majibu tunashindwa kutoa,``alisema.

Alisema angalau wakishapata waraka wa maandishi kutoka kwa Rais Kikwete wanaweza kujibu.

Hata hivyo, Bw. Mohamed alisisitiza kwamba mazungumzo hayo katika kiwango cha Makatibu wakuu, yameshapita.

Alisema Makatibu wakuu, wa CUF na CCM wamekaa mezani na kuchukua muda mrefu wa miezi 14, hivyo kikao chao hakiwezi tena kuwa na jipya.

Alisema japokuwa wakipata taarifa ya maandishi kutoka kwa Rais wataijadili, lakini ni wazi kwamba CUF haitakubali tena mazungumzo ya makatibu wakuu wa vyama hivyo.

``Iwapo atatuandikia, barua yake tutaitafakari vema, iwapo tu itataja watu wengine wakukutana na kuzungumza lakini si Seif na Makamba,``alisema Bw. Mohamed.

Alisema CUF kinaamini kwamba maelekezo atakayoyatoa Rais sasa ni Bw. Seif kukutana na Rais Karume.

Kuhusu madai ya CUF kuhusika na wananchi wa Pemba wanaotaka kisiwa hicho kijitenge, Bw. Mohamed alisema wananchi wote wana haki ya kutoa maoni yao.

Alisema eneo la Pemba pia kuna wanachama wa vyama vingine, kwa hiyo anaamini kati ya wananchi hao waliopeleka barua Umoja wa Mataifa kutoa madai hayo, wamo pia wanachama wa CCM.

Hata hivyo, kiongozi huyo alimshangaa Kada wa CCM Bw. Hiza Tambwe aliyekaririwa akisema wapemba hao ni wahaini, na wanapewa msukumo na CUF.

``Nataka umuulize Tambwe hivi wale wabunge 55 waliotaka iundwe Serikali ya Tanganyika walikuwa wa Chama gaini? Walikamatwa na kufikishwa Mahakamani?``alihoji.

Alisema kama kuna mtu ambaye ameigawa Zanzibar hadi hivi sasa ni Rais Aman Karume, ambaye ameunda Serikali ya upande mmoja.

Bw. Mohamed alisema hata katika ajenda namba tatu ya mazungumzo, wajumbe wote walikubaliana kwamba Karume ameigawa Zanzibar.

Alisema madai ya Tambwe kusema CUF ni chama cha vurugu, sio ya kujenga na wala maneno hayo hayana faida kwa CCM zaidi ya kuleta utengano.

``Kwanza hatujui hayo yalikuwa maneno ya CCM au ya Tambwe Hiza, sisi tumekaa na CCM meza moja kwa miezi 14, kwanini walijadiliana nasi mambo muhimu kama sisi ni magaidi?``alihoji.

Alisisitiza kwamba CUF kimeandikishwa kwa mujibu wa sheria, na hakijapata onyo lolote toka kwa Msajili wa vyama vya siasa kutokana na kukiuka misingi na kanuni za vyama vingi.

Aliionya CCM kwamba Tambwe atawafikisha pabaya kutokana na maneno yake yakufufua shari.


``Huku wanadai turejee kwenye meza ya mazungumzo, huku wanasema sisi ni magaidi, sasa tushike lipi?``alihoji.
  • SOURCE: Nipashe

Haya sasa na hao waliodaiwa kuwa wahaini kuna CCM ndani?
Wanaoelewa watoe ufafanuzi..
 
siasa za zanzibar ni kama drama hivi.
watoto wa Karume (baba), kwanza wote ni waarabu nusu. kwa maana hiyo licha ya kuwa kuna uwezekano wa kuwa wao wanauhusiano na hizbu moja kwa moja, baadhi ya watoto hao (atleast mmoja kwa ushahidi kamili nnao) amelikana jina la karume na kutumia sir name yake jina la ukoo (wa kiarabu) wa mama yake. ...
mtoto huyo amelelewa Oman, ambapo ni sehemu mama yake alikokimbilia baada ya karume kufa. mtoto huyo ni Mpemba (mama yake), na yeye sijui, lakini jamaa zake wa karibu wa upande wa mama wote ni wapemba na CUF na hilo halina mjadala.

mtoto wa karume mwengine, aliolewa na Mpemba (mwenye asili ya uarabu, ambaye haina doubt ni CUF), na baada ya kuachana nae sasa ameolewa na Mpemba mwengine mwenye cheo kikubwa tu kwenye uongozi wa CUF,Zanzibar.

sasa hizi kesi za kuwa CUF ni chama cha waarabu, au wanataka wawarudishe waarabu, hazina msingi ukizingatia kuwa watoto wa mpinduzi wa zanzibar wao wenyewe ni nusu waarabu na wanauhusiano usio pingamizi na CUF
 
hizbu ni chama kilichokuwa kinahusishwa na usultani. chama hichi kilikuwa na wanachama wa kila rangi, ambao labda wote walikuwa wanapenda nchi iendelee kuongoza na sultan (mornachy).
watu hawa wapo wenye asili ya kiarabu, asili ya kiafrika na asili ya kishirazi.

sio kila mweupe ni hizbu na sila mweusi ni ASP vile vile.

hii fitna ya kuhusishwa hizbu na watu weupe ni dhana mpya, ambayo wazee wa zamani wanaipinga kwa kuwa sio fact yenyewe
 
Kibunango ni lazima mkae chini mkubaliane kuidropu hii issue la sivyo itaongeza uchochezi tuu!
Sasa wewe una vithibitisho kuwa ccm hawana uhusiano na hizbu?

Unamshauri nani Kibunango mwenzetu huyo hasikii haoni kama ni maji ya Bendera ya kijani alikuntwa zaidi ya share walopewa wenzake.
 
mahazibu si waarabu tu mahizibu kwa mkukusudia ZNP ni wale ambao wanajiita wazalendo wa zanzibar au maalwatwan wao wanaamini kuwa wao ndio wenye haki ya zanzibar na ASP wengi wao ni watwana wakuja na si wenye asili ya Zanzibar na ndio maana watu wanasema CUF ni mahizbu kwa kuwa wao wanasimamia sera zao mfano tokea kuundwa CUF kuna wazanzibari na wazanzibara kwa maana wale wazalendo wa zanzibar na wale wageni.

Nimekuelewa Mheshimiwa. Kwa maana hiyo ndiyo maana wafuasi wa CUF ndio hung'ang'ania sana kuwa wao ndio WAZANZIBARI na kuwabeza wenzao wasio CUF-hata kama ikiwa mababu zao ndio walioshirikiana na Masarahangi wa Hassan Bin Ali kujenga vitu kama msikiti wa kale kule Kizimkazi- Uzanzibari umeanishwa vizuri katika Sheria ya Mzanzibari kama ilivyopitishwa na Baraza la Wawakilishi. Kinyume cha hivyo "definitions" nyengine zote zinalenga katika dhana ya UHIZBU.
 
Unamshauri nani Kibunango mwenzetu huyo hasikii haoni kama ni maji ya Bendera ya kijani alikuntwa zaidi ya share walopewa wenzake.
Jmushi na Bikirembwe,
Jaribuni kukumbuka hii issue ya hizbu ambayo ilikuwa imekufa kifo cha taratibu kwa kadiri ya uukuaji wa SMZ imerudishwa na nani?
 
Jmushi na Bikirembwe,
Jaribuni kukumbuka hii issue ya hizbu ambayo ilikuwa imekufa kifo cha taratibu kwa kadiri ya uukuaji wa SMZ imerudishwa na nani?

CUF wameirudisha kwasababu wamegundua hiyo ndiyo mojawapo ya silaha ambayo CCM wanaweza kuitumia ili wasibanwe!

Soma makala zinaonyesha kuwa CUF wanadai kuwa CCM inawa brand wao as "Terrorists"
 
CUF watakiwa kujiandaa

na Saada Said, Zanzibar



KATIKA kile kinachoonekana kama kujibu mapigo, Chama cha Wananchi (CUF) kimewataka vijana wafuasi na wanachama wa chama hicho, kujiandaa kwa mapambano.
Kiongozi mmoja wa juu wa CUF, alisema wakati akihutubia mkutano wa hadhara mwishoni mwa wiki huko Pemba kuwa, wakati wa mapambano ya kudai haki umefika na kuwataka vijana wote kuwa tayari kufuata maelekezo na maagizo ya viongozi wao yanayotolewa.
Akihutubia mamia ya wanachama wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Nyarugusu, Jimbo la Fuoni, Naibu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma, Salim Bimani, alisema wakati umefika kwa Wazanzibari kudai haki yao bila kusubiri.
Alisema hatua ya kusubiri kuletewa haki ndani ya kisahani cha chai imepitwa na wakati, kutokana na waafidhina wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hususan wale wa Zanzibar, kushikilia misimamo ya kihistoria na kukataa makubaliano ya mwafaka ambayo yangeweza kwa kiasi kikubwa kupunguza joto la kisiasa visiwani humu.
“Hakuna kukata tamaa, ule wakati wa kusubiri uletewe haki yako kwenye kisahani cha chai umekwisha, hatuwezi kupata haki yetu mpaka tupambane… sasa ni wakati wa mapambano, tutadai haki yetu mpaka ipatikane, hakuna kusita,” alisisitiza Bimani huku akishangiliwa na idadi kubwa ya vijana waliohudhuria mkutano huo.
Kauli hiyo ya CUF inakuja siku chache tu baada ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kueleza kuwa wapo tayari kuwalinda viongozi wao kwa namna yoyote ile dhidi ya vitisho kutoka kwa viongozi wa CUF.
Bimani aliwaeleza vijana hao kuwa, matukio ya hivi karibuni yamethibitisha usemi wa zamani kuwa haki haiwezi kupatikana hivi hivi kwa kukaa, bali hupatikana iwapo watu watajitolea kuidai na kuitetea kwa nguvu zote.
Kutokana na hali hiyo, Bimani aliwataka vijana wa chama hicho kuwa tayari na kusikiliza maagizo ya viongozi wao wakati ukifika wa kuidai haki hiyo na kusisitiza kuwa safari hii hakutakuwa na kukata tamaa katika hilo.
“Sasa lazima tutoke jasho, na tutasimamia haki yetu hadi tone la mwisho la damu, lakini hatuwezi kukaa hivi hivi tu, tumeshafanyiwa mengi, tumeshadhalilishwa, tumeshabakiwa ndugu na mama zetu, tumeshafungwa, tumeonewa vya kutosha, lipo lililokuwa bado hatujafanyiwa?” alisema na kuhoji Bimani.
Alisema hivi sasa CUF haiwezi kuiachia CCM ikatamba huku akitumia methali za Kiswahili kwamba nguruwe hawezi kuachiwa shamba la muhogo kwa kuwa atalimaliza.
Naibu Mkurugenzi huyo alisema CUF imejifunza mengi kuhusu siasa za Afrika, hasa kupitia uchaguzi uliomalizika hivi karibuni nchini Kenya, ambako mamia ya Wakenya walipoteza maisha na wengine kukimbia makazi yao, hivyo elimu hiyo itasaidia pia katika uchaguzi ujao wa 2010 ambapo vijana watakabidhiwa madaraka yote ya usimamizi wa uchaguzi.
“Uchaguzi wa 2010 utaongozwa na vijana na akina mama, maana tumeshaona kwa nchi jirani mambo yanavyovurugwa, kwa hivyo sasa ni wakati wa kujitayarisha na sisi,” alisema huku vijana wakisimama kama ishara ya kuunga mkono kauli hiyo.
Pamoja na mambo yaliyotokea Kenya, Bimani alisema pia kuwa uchaguzi wa Zimbabwe nao umewapa funzo kubwa kutokana na mizengwe iliyojitokeza.
“Siasa za Afrika mnazisikia, tukimaliza uchaguzi wa Zimbabwe tunakuja uchaguzi wa Zanzibar, Tsvangirai hakuwa na mtu… yule kapigwa kama pweza kama tulivyopigwa sisi, kwa hivyo na sisi sasa hatuna mtu zaidi wa wenyewe wananchi,” alisema Bimani.
Awali, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Juma Duni Haji, alisema CUF haipo tayari kufanywa matofari ya kuparamiwa na wezi kwa ajili ya kuchungulia ndani ya nyuma na kuiba, kwani hivi sasa wameshaamka.
Alisema CUF pia haikubali kufanyika vurugu katika kutafuta suluhu ya mpasuko wa kisiasa visiwani Zanzibar, na wataendelea kutafuta njia sahihi kutokana na CCM kutokuwa tayari kwa suala hilo.
“Mtu akitafunwa na nyoka mara moja tu, basi hata ukuti ukimgusa huruka… sisi hatuwaamini tena,” alisema.
Duni, ambaye anakaimu nafasi ya Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad aliye nje ya nchi, alisema haoni sababu yoyote ya kurudi katika meza ya mazungumzo kama alivyoagiza Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akizungumza na mabalozi, kwa kuwa CCM haina dhamira ya kweli ya kuondosha tofauti visiwani Zanzibar.
Aliwataka wanachama wa chama hicho pamoja na Watanzania kumpuuza Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda cha CCM, Tambwe Hiza, kwani alishawahi kusema kuwa kiapo alichokula wakati anajiunga CUF ndicho kilichomdhuru.
“Tambwe kiapo chake ndicho kilichomdhuru maana wakati anajiunga kwetu alikula kiapo akasema hivi; ‘mimi nikirudi CCM basi nikalale na mama yangu’. Sasa unaona kiapo hicho? Madhara yake ndiyo hayo ya kuropokwa, leo hata hajijui anasema nini masikini,” alisema Duni.
Wakati chama hicho kikiwataka wanachama wao kujitayarisha kwa lolote, wabunge na wawakilishi wa CUF wameamua kukutana kisiwani Pemba kwa lengo la kutathimini hali ya kisiasa visiwani hapa, hasa katika kipindi hiki ambapo joto la kisiasa limepanda baada ya vyombo vya usalama kuwakamata watu saba kati ya 12 waliowasilisha barua yao Umoja wa Mataifa kutaka Kisiwa cha Pemba kijitenge.
Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohammed aliliambia Tanzania Daima kwamba kikao hicho kilichofanyika jana, kiliwakutanisha viongozi hao, ili kutafakari hali ya mambo inavyokwenda, hasa katika kipindi hiki ambapo mambo kadhaa yameanza kujitokeza ambayo hayana mwelekeo mzuri katika nchi. Akithibitisha kufanyika kwa kikao kimoja katika Ukumbi wa Ofisi ya CUF Wilaya ya Ole, chini ya uenyekiti wa Khalifa Suleiman Khalifa (Gando), Hamad alisema kuwa wajumbe waligawiwa waraka wa mazungumzo ya mwafaka kati ya CCM na CUF. Katika hatua nyingine, Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume alirejea jana kutoka katika ziara yake nchini Marekani na kushindwa kuzungumza na waandshi wa habari, huku maofisa wa Ikulu wakiahidi kuitisha mkutano wa waandishi leo Ikulu.
 
Politicians bwana matatizo matupu.. Ningekuwa mimi Kikwete ningeweka ndani viongozi wote wanaoshinikiza agenda hii toka CCM, CCM vijana na hao CUF wanaojaribu kuleta vurugu zisizokuwa na msingi...

Na hizi lugha za Hizbu na sijui waarabu ni lazima zikome mapema kwani hao Washiraz ambao ni part ya ASP ni watu gani?...Haya matatizo ya rangi ndio yaliyompa sababu na kiburi Dikteta Karume kutoa ruksa ndoa za nguvu kwa sababu hali kama hii ya utenganisho ilikuwepo toka upande wa pili (waarabu) sasa hivi weusi tunaanza kuitumia kama walivyokuwa waarabu wenyewe..

Ni ajabu kubwa weusi tulivyokuwa na laana maanake leo South Afrika ambao kwa miaka mingi walikuwa wakilia na Apartheid leo hii wao weusi ndio vinara wa kutenga watu wengine tena wana chuki kubwa kuliko hata Kaburu...
Ujinga mtupu..
 
Jmushi na Bikirembwe,
Jaribuni kukumbuka hii issue ya hizbu ambayo ilikuwa imekufa kifo cha taratibu kwa kadiri ya uukuaji wa SMZ imerudishwa na nani?

Kibunango, kwa kumbukumbu za karibuni tu aliyeikumbusha ni babu yenu Kingunge katika mahojiano yake ambayo alimkandia na Warioba. Alisema kuwa CUF asili yao ni ZNP( hawa ndio Hizbu, kama ulikuwa hujui) ambao wana utamaduni wa kukataa kushindwa.

Na kama kuianzisha hiyo ni propaganda ya CCM na SMZ kitambo sasa ila CUF juzi ndio wamejibu mapigo tu.
 
Back
Top Bottom