Uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Somalia umevunjika rasmi

luangalila

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2014
Posts
6,346
Reaction score
6,928
Katika wakati usiotabirika urafiki wa kidiplomasia kati ya Kenya na Somalia umevunjika baada ya Kenya kumvurusha balozi wa Somalia nchi Kenya na kumuamuru balozi wa Kenya nchini Somalia kurudi nyumbani.

Chanzo kikubwa cha kuvunjika kwa uhusiano baina ya nchi hizi mbili ni mgogoro eneo la bahari Mashiriki Kaskazini mwa Kenya mpakani na Somalia (Kusini mwa Somalia) eneo hilo ambalo Somalia wanadai ni la kwao na Kenya kudai pia ni la kwao.

Hakika kwa kitendo hicho ni wazi wataalamu wa mambo wanasema huenda eneo hilo lina rasilimali nyeti ya mafuta

Lakini kwanini Kenya wamekuwa wepesi kufunja uhusiano kati na Somalia ilihali wanafahamu ya kuwa Al Shaabab ni maadui zao wakubwa na Somalia ndio makazi yao hawaoni kama kitendo hicho kitachochea vitendo vya mashumbulizi toka kwa magaidi ?

Wakenya pigeni kelele Serikali yenu iwe calm na pro active ktk ku resolve huo mgogoro kwa njia ya kidiplomasia mfano Tanzania iliingia ktk mgogoro wa mipaka na Malawi awamu ya bibi Joyce Banda lkn Tanzania hawakufukuza balozi zaidi zaidi iliongeza kasi ya mazungumzo baina ya viongozi wa nchi hizi mbili later walivyoona hawana maelewano wakatafuta mediator alikuwa Rais wa Mozambique thereafter things started to move smoothly
 
hivi kulikuwepo na uhusiano KWELI? kwa sababu hats kdf wapo kule kwa ridhaa ya Marekani na si Somalia.
 

Ahaaa haaa haaa
wanapenda kupora cha WATU. na sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kuwa wamezoea kwao kunyang'auana vitu. Kenya kila kitu hususan ARDHI ilisha nyang'auliwa na kina uhuru Kenyatta family na wengine.
 
hivi kulikuwepo na uhusiano KWELI? kwa sababu hats kdf wapo kule kwa ridhaa ya Marekani na si Somalia.
"Kdf wako kule kwa ridhaa ya Marekani" unamaanisha nini? Unadhani Marekani ndio waliotuamuru tuingie Somalia 2011? Unajua chanzo cha Kenya kuingia Somalia? Ama unadhani tullingia huko kwa sababu ya kufuata amri ya Marekani?
 
VITA SIO KITU KIZURI, HAPA KENYA INATENGENEZA ADUI WA PILI ANAYEITWA SOMALIA, NI VITA NGUMU SANA KWAKE KWA KUWA HATA HUYU ADUI ALSHABAB BADO HAJAMMUDU. ANGESULUHISHA MGOGORO HUU KIDIPLOMASIA ZAIDI ILI APATE SAPOTI YA KUPAMBANA NA ALSHABAB.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ya Somalia haipo bila KDF itakuwa overun by alshabybe within no time. Wenye wivu uwanja wa watokwa povu ni wenu...welcome.
 
"Kdf wako kule kwa ridhaa ya Marekani" unamaanisha nini? Unadhani Marekani ndio waliotuamuru tuingie Somalia 2011? Unajua chanzo cha Kenya kuingia Somalia? Ama unadhani tullingia huko kwa sababu ya kufuata amri ya Marekani?

Who is funding for the (kdf) existance in Somalia?
 
Write your reply...mturuki ako na mpango wa kuweka military base,somalia
 
"Kdf wako kule kwa ridhaa ya Marekani" unamaanisha nini? Unadhani Marekani ndio waliotuamuru tuingie Somalia 2011? Unajua chanzo cha Kenya kuingia Somalia? Ama unadhani tullingia huko kwa sababu ya kufuata amri ya Marekani?
Wakati KDF ilipokuwa inaingia Somalia U.K. na U.S. walipinga vikali maamuzi hayo ya Kenya. Achana na hawa watu na propaganda zao.
 
Wakati KDF ilipokuwa inaingia Somalia U.K. na U.S. walipinga vikali maamuzi hayo ya Kenya. Achana na hawa watu na propaganda zao.
Exactly. After Marekani walipinga vikali Kenya kuingia Somalia, Kibaki na kichwa yake ngumu aliamua kuingia Somalia kama mbaya mbaya. Marekani walishindwa kitu ya kufanya juu bado wanatutegemea and we are their closest ally in this region. Ilibidi Marekani wanyamazie hio stori. Baadaye wakacome up na condition ati Kenya ikijoin Amisom watatusupport lakini Kenya ikawaambia tutajoin tukimaliza mission yetu which was to capture Kismayu. Huyo ni Kibaki, Uhuru sijui kama ako na hizo balls.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…