Uingereza kufuta kodi za bidhaa kutoka Nchi Maskini 65 Duniani

Uingereza kufuta kodi za bidhaa kutoka Nchi Maskini 65 Duniani

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Serikali ya Uingereza imeanzisha mpango unaolenga kufuta kodi ya bidhaa mbalimbali zinazoingia nchini humo kutoka nchi maskini 65 duniani. viatu, nguo na baadhi ya matunda yasiyo zalishwa nchini humo ni miongoni mwa bidhaa zitakazo nufaika na mpango huo.
photo_2022-08-16_15-20-28.jpg


Mpango huu unaotarajiwa kuanza rasmi January, 2023 utaongeza idadi ya bidhaa zinazo ruhusiwa kuingizwa nchini humo pasipo kudaiwa tozo na utahusisha asilimia 99 ya bidhaa zote kutoka Afrika.

Kitengo kinachohusika na biashara ya ndani nchini humo kimeelezea hatua hii kama sehemu ya kuongeza mshikamano, kuondoa umaskini na kupunguza utegemezi wa misada kwenye nchi za Afrika.

Aidha, mpango huu utakuwa na nguvu ya kuondoa ushiriki wa nchi wanufaika ikiwa zitajiingiza kwenye mambo yanayovunja haki za binadamu pamoja na kushindwa kutimiza matakwa yatakayowekwa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa.

Mfano wa matunda yatakayo ingia nchini humo pasipo kutozwa kodi ni matango ambayo huadimika sana wakati wa majira ya baridi.

Chanzo: BBC
 
Wamechelewa Sana. Kwa sasa hawana mbadala Ila tu kuruhusu Africa iendelee.
Wasirudie Tabia ya kuua viongozi shupavu wa Africa, washikamane nao kidiplomasia.
 
Serikali ya Uingereza imeanzisha mpango unaolenga kufuta kodi ya bidhaa mbalimbali zinazoingia nchini humo kutoka nchi maskini 65 duniani. viatu, nguo na baadhi ya matunda yasiyo zalishwa nchini humo ni miongoni mwa bidhaa zitakazo nufaika na mpango huo.View attachment 2325454

Mpango huu unaotarajiwa kuanza rasmi January, 2023 utaongeza idadi ya bidhaa zinazo ruhusiwa kuingizwa nchini humo pasipo kudaiwa tozo na utahusisha asilimia 99 ya bidhaa zote kutoka Afrika.

Kitengo kinachohusika na biashara ya ndani nchini humo kimeelezea hatua hii kama sehemu ya kuongeza mshikamano, kuondoa umaskini na kupunguza utegemezi wa misada kwenye nchi za Afrika.

Aidha, mpango huu utakuwa na nguvu ya kuondoa ushiriki wa nchi wanufaika ikiwa zitajiingiza kwenye mambo yanayovunja haki za binadamu pamoja na kushindwa kutimiza matakwa yatakayowekwa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa.

Mfano wa matunda yatakayo ingia nchini humo pasipo kutozwa kodi ni matango ambayo huadimika sana wakati wa majira ya baridi.

Chanzo: BBC
Wanajipendekeza tu baada ya kuona wamepoteza ushawishi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tanzania ana nini cha kuuza UK hata ile AGOA tumeshindwa kabisa kuitumia. Hiyo fursa waliyotoa UK haituhusu sisi.
 
Back
Top Bottom