Uingereza: Waziri Mkuu Johnson aomba radhi kwa sherehe ya unywaji pombe

Uingereza: Waziri Mkuu Johnson aomba radhi kwa sherehe ya unywaji pombe

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson ameomba radhi kwa kushiriki katika sherehe ya kunywa pombe iliyofanyika katika bustani ya ofisi yake wakati nchi hiyo ilipokuwa chini ya vizuizi vikali vya watu kujumuika.

Hata hivyo, kiongozi huyo amepuuza miito ya upinzani ya kumtaka ajiuzulu, iliyomtaja kama mtu asiyeona aibu.


Johnson amesema aliuchukulia mkusanyiko huo wa watumishi wa ofisi yake kuwa wa kikazi, na kuongeza kuwa hivi sasa anajutia tukio hilo.

Johnson alikuwa akijibu maswali ya wabunge mchana wa leo mjini London, baada ya kusalia kimya kufuatia ufichuzi wa sherehe hiyo inayouweka mashakani uongozi wake.

Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha Labour Keir Starmer amepuuza hatua hiyo ya Johnson ya kuomba msamaha, akisema imechelewa na haina maana, baada ya miezi ya udanganyifu na ulaghai.
 
Kassim Hapa Home Amekausha Kimya Hata Alipotajwa
 
Kusalimika hii issue ni majaaliwa, waingereza watakomaa nae hadi ajiuzuru. Mbaya zaidi na ndani ya chama chake wapo wanaotaka ajiuzuru
 
Maana yake nini?
Maana yake ni kwamba pombe haijawahi kumwacha mtu yeyote salama.

^I don't use those things^~ Donald Trump.

^Meu pai foi uma grande lição para mim. Ele era alcoólatra e sofreu horrivelmente como resultado. Eu não quero seguir o exemplo dele^~Cristiano Ronaldo.
(My father was a great lesson to me. He was a helpless alcoholic, and suffered horribly as a result. I don't want to follow his example)
 
Back
Top Bottom