Ujanja mpya umeibuka wa kutapeli wanawake hela kwa kutumia dating page za Instagram

Ujanja mpya umeibuka wa kutapeli wanawake hela kwa kutumia dating page za Instagram

Habari wadau.

Ukweli wabongo ni Watu wanaojua sana kucheza na fursa.

Wamegundua wanawake wengi sana wanatafuta wachumba wa kuwaoa. Hivyo wajanja wameanzisha page instagram za kuunganishiwa mwenza kwa malipo kiasi kazaa. Na page hizo zinakiwa zinatoa ushauri wa mambo ya mahusiano ili kuvutia followers wajae.

Mbinu wanayofanya.

Kwanza Kwenye page zao wanapost details za mwanaume mwenye kazi nzuri akijifanya anatafuta mchumba wa kike wa kuoa.

Huyo mwanaume anakuwa ni fictional character tu hayupo kiuhalisia. Ila kunakuwa na wanaume kazaa wanaojuana na mwenye dating page kwa ajili ya kujifanya wao ndio huyo mwanaume hewa aliyepostiwa.

Wadada wengi walio single wakiona sifa za huyo mwanaume anaetafuta mchumba wanaenda inbox wakiomba wanganishwe nae. Huko inbox wanaambiwa kuunganishwa ni lazima watoe hela 20,000 ama 30,000 kuonesha wapo serious.

Wakishalipa hizo hela wadada hao wanapewa namba ya mwanaume ambaye ameshapangwa tayari na mwenye dating page. Kwamba wazuge zuge hawa wadada kwa kuwachatisha tu. Na kuwatumia picha hata za uongo. Ili wadada waone hela waliyolipia imefanya kazi. Ila baada ya siku kazaa jamaa akate mawasiliano ama anajifanya amesafiri.

Hivyo wanakuwa wanapiga hela za wadada wanaotafuta wachumba kila siku.

Unakuta per day wenye hizo page wanatengeneza hadi laki 5 kwa urahisi tu.

Nimelijua hilo baada ya kupewa story na boda boda mmoja Ambae ni mmojawapo ya hao wanaume wanaotumika kuwachatisha wanawake waliolipishwa fedha huko instagram kwenye page za kuunganishiwa wachumba.

Unakuta mdada meneja wa bank ana masters ila anachatishwa na muhuni tu dalali wa vyumba anaejua kiingereza. Dada anajiona amepata mume anasubiria kuonana nae. Huku kashaliwa elfu 30 yake na mwenye page
Bora hiyo, ipo hii ya wazungu, wachina kuwaibia wadada wanaofanya kazi bank taarifa za siri za kibenki, yaani anakuja bank na kutoa/kuweka hela na unakuta ana mpunga mrefu bank, mara ya kwanza ya pili etc, baada ya hapo mdada anajiona kapata, then siku ya siku mzungu anamuomba wakutane wakalane hotel, unakuta ni muda wa kazi akitoka waonane (kinacholengwa hapo ni laptop/simu zenye taarifa za bank anayofanyia kazi), basi wanaenda hotel nzuri tu nyota tano. Wakifika mzungu hatoi kitambulisho na mdada kwa sababu anajiona kapata mzungu nasi anasema mume wangu hahahah, wanaenda chumbani baada mida kama saa tano au sita au midnight Mzungu anatoka anasema kapata dharula mke wake kampigia au kisingizio chochote anatoka hotelini na credentials za mdada zoteeee, asubuhi hana kila kitu, hii imepelekea bank nyingi kuibiwa hela mno mno, sasa sijui bank wanaujua huu utapeli. Kwa hiyo unakuta mwizi siyo mfanyakazi wa bank ila particular zake zimetumina. Hata kwa vijana the same. Wadada wamelizwa sana tena sana. Dating ni social, kutana na watu utapta mke/mume.
 
Wadada hao hao njiani wana ringa afu kwa keyboard wana tafuta mchumba
 
Mimi sina maana nimepewa story tu.

Ukitaka namba nenda katembelee page za wachumba instagram utapewa namba. Ila ujiandae kulipishwa hela.
Dah basi itabidi hao wadada waje huku jamiiforum maana huduma za kuunganishwa ni Bure Sina insta mkuu ila Waite waje huku
 
Habari wadau.

Ukweli wabongo ni Watu wanaojua sana kucheza na fursa.

Wamegundua wanawake wengi sana wanatafuta wachumba wa kuwaoa. Hivyo wajanja wameanzisha page instagram za kuunganishiwa mwenza kwa malipo kiasi kazaa. Na page hizo zinakiwa zinatoa ushauri wa mambo ya mahusiano ili kuvutia followers wajae.

Mbinu wanayofanya.

Kwanza Kwenye page zao wanapost details za mwanaume mwenye kazi nzuri akijifanya anatafuta mchumba wa kike wa kuoa.

Huyo mwanaume anakuwa ni fictional character tu hayupo kiuhalisia. Ila kunakuwa na wanaume kazaa wanaojuana na mwenye dating page kwa ajili ya kujifanya wao ndio huyo mwanaume hewa aliyepostiwa.

Wadada wengi walio single wakiona sifa za huyo mwanaume anaetafuta mchumba wanaenda inbox wakiomba wanganishwe nae. Huko inbox wanaambiwa kuunganishwa ni lazima watoe hela 20,000 ama 30,000 kuonesha wapo serious.

Wakishalipa hizo hela wadada hao wanapewa namba ya mwanaume ambaye ameshapangwa tayari na mwenye dating page. Kwamba wazuge zuge hawa wadada kwa kuwachatisha tu. Na kuwatumia picha hata za uongo. Ili wadada waone hela waliyolipia imefanya kazi. Ila baada ya siku kazaa jamaa akate mawasiliano ama anajifanya amesafiri.

Hivyo wanakuwa wanapiga hela za wadada wanaotafuta wachumba kila siku.

Unakuta per day wenye hizo page wanatengeneza hadi laki 5 kwa urahisi tu.

Nimelijua hilo baada ya kupewa story na boda boda mmoja Ambae ni mmojawapo ya hao wanaume wanaotumika kuwachatisha wanawake waliolipishwa fedha huko instagram kwenye page za kuunganishiwa wachumba.

Unakuta mdada meneja wa bank ana masters ila anachatishwa na muhuni tu dalali wa vyumba anaejua kiingereza. Dada anajiona amepata mume anasubiria kuonana nae. Huku kashaliwa elfu 30 yake na mwenye page
Desperation ya wanawake wanaotaka kuolewa ndiyo inawaweka mjini hawa watu
 
Hivi kwanini Elimu isifutwe?
Huwa naumia sana ninapoona mtu mwenye elimu angalau kuanzia kidato cha nne anatapeliwa mtandaoni
 
Wanawake wanaamini watu haraka sana hapo ndo ilipo shida yao kubwa, miaka miwili iliopita nilizoeana na dada mmoja yuko huko nchi za Gulf nilijuana nae kupitia instagram akaanza kujichangaya bila hata kumset ni basi tu sometimes imani ya Mungu inatuweka mbali na dhulma kwa kuhofia.
Ila nilimueleza kuwa usiamini watu haraka
 
Wanawake wanaamini watu haraka sana hapo ndo ilipo shida yao kubwa, miaka miwili iliopita nilizoeana na dada mmoja yuko huko nchi za Gulf nilijuana nae kupitia instagram akaanza kujichangaya bila hata kumset ni basi tu sometimes imani ya Mungu inatuweka mbali na dhulma kwa kuhofia.
Ila nilimueleza kuwa usiamini watu haraka
Ukiwa muongeaji na uko active mtandaoni, akikucheki ushajibu kila siku unamcheki, hawazi kua huyu kijana ni jobless ndo maana ana muda wa kuchezea ila anachowaza ni kua wewe umefall kwake na unampenda kwelikweli.
 
"Nimelijua hilo baada ya kupewa story na boda boda mmoja Ambae ni mmojawapo ya hao wanaume wanaotumika kuwachatisha wanawake"


Ha ha ha hii kiboko usikute na bida wangu nae ni miongoni Kwa vijana wa huko😂
 
Back
Top Bottom