Ujasusi / Upelelezi / Udukuzi: Maana yake halisi na uhatari wake

Ujasusi / Upelelezi / Udukuzi: Maana yake halisi na uhatari wake

mkuu Yericko Nyerere kwenye hayo maandishi niliyokoleza, hauoni kama ni vema kwa jasusi kulinda cover yake kwa kutochukua hatua yoyote ya moja kwa moja zaidi ya kufahamisha mamlaka husika za kisheria (law enforcement agencies) kama police and the like? au huo nao ni uozo wa sheria ya T.I.S.S ya mwaka 1996???!!!!!!!!!!!!!!!
Jasusi on the ground anatakiwa ku pass information kjwa superiors wake wao ndo wataichambua taarifa na kushirikiana na vyombo vingine vya dola. Jasusi wa ground anakusanya taarifa ambazo ni raw. Zile taarifa raw zinachanganwa na taarifa zingine na kufanyiwa uchambuzi halafu ndo inafanyika decision making. Decision making inaweza ikawa ni kushauri chombo fulani labda polisi au watu wa sera au mambo mengine. Na ili taarifa iweze kuonekana ni intel lazima kuwe na concrete evidence bila chembe ya doubts...
 
Jasusi on the ground anatakiwa ku pass information kjwa superiors wake wao ndo wataichambua taarifa na kushirikiana na vyombo vingine vya dola. Jasusi wa ground anakusanya taarifa ambazo ni raw. Zile taarifa raw zinachanganwa na taarifa zingine na kufanyiwa uchambuzi halafu ndo inafanyika decision making. Decision making inaweza ikawa ni kushauri chombo fulani labda polisi au watu wa sera au mambo mengine. Na ili taarifa iweze kuonekana ni intel lazima kuwe na concrete evidence bila chembe ya doubts...
mkuu Freelancer asante sana kwa kunisahihisha kaka.....
 
mkuu Yericko Nyerere kwenye hayo maandishi niliyokoleza, hauoni kama ni vema kwa jasusi kulinda cover yake kwa kutochukua hatua yoyote ya moja kwa moja zaidi ya kufahamisha mamlaka husika za kisheria (law enforcement agencies) kama police and the like? au huo nao ni uozo wa sheria ya T.I.S.S ya mwaka 1996???!!!!!!!!!!!!!!!
Kuna jasusi na wapelelezi
Jasus hana sheria inayomlinda kwa sababu anafanxa kaz kama kivuli na anaweza akazuia kwa kuangamiza kama sniper au whatever kulingana na mission yake without left any single doubts ya mhusika kwan n kosa kufahamika , kwa usiwe na shaka na hilo Kwan wamefumzwa

Wapelelez n kama fbi wanachunguza then wanashirikiana na polis
Lazima ujue kaz kubwa ya wapelez n spies capture na kulinda maslah ya nchi ndan ya nchi
Polis wanalinda raia hawana taaluma ya kukamata jasusi wala kumtambua au namna ya vifaa avitumiavyo

Dunian tunajua kuna cia lkn hakuna nchi inaxowatambua au kuwakaribisha lkn wapo nchi mbalmbali hata tz na wabafanya kaz wakigundulika n kosa kubwa la kidplomasia kt ya nchi hizo
Na huyo mtu atapotea daima

Na majasus wanaingia kupitia shuguli za baloz kama watumish na pia biashara

Tz tunachombo km cia
Je tunachombo kama fbi?
Kimajukumu
Majib tafadhal
Then tumjadil yericko
 
Kuna jasusi na wapelelezi
Jasus hana sheria inayomlinda kwa sababu anafanxa kaz kama kivuli na anaweza akazuia kwa kuangamiza kama sniper au whatever kulingana na mission yake without left any single doubts ya mhusika kwan n kosa kufahamika , kwa usiwe na shaka na hilo Kwan wamefumzwa

Wapelelez n kama fbi wanachunguza then wanashirikiana na polis
Lazima ujue kaz kubwa ya wapelez n spies capture na kulinda maslah ya nchi ndan ya nchi
Polis wanalinda raia hawana taaluma ya kukamata jasusi wala kumtambua au namna ya vifaa avitumiavyo

Dunian tunajua kuna cia lkn hakuna nchi inaxowatambua au kuwakaribisha lkn wapo nchi mbalmbali hata tz na wabafanya kaz wakigundulika n kosa kubwa la kidplomasia kt ya nchi hizo
Na huyo mtu atapotea daima

Na majasus wanaingia kupitia shuguli za baloz kama watumish na pia biashara

Tz tunachombo km cia
Je tunachombo kama fbi?
Kimajukumu
Majib tafadhal
Then tumjadil yericko
Ramark naona unataka kuturudisha katika mjadala huu Ni nini tofauti ya Mwanausalama na Askari wa Upelelezi?
 
Kuna askar upelelez na mplelezi au mchunguz ambaye si askari
 
Nami nauliza hv hao majasusi unaweza ikatokea wakaugua ukichaa?..yaani kuchizi?
 
Yericko Nyerere majasusi hao wanaofuatilia mienendo ya viongozi wa juu wa serikali sio invisible bali ni visible kwa maana kwamba hawa watu wapo visible na wanaonekana sana lakini ni unidentifiable (sio rahisi kuwatambua)

katika kuchagua watu wa kufanya kazi hii ya surveillance huwa wanaangalia sana general appearance ya mtu na hupendelea watu wenye average outlook ambao ni rahisi sana kudharaulika na kuwa ignored pale mtu wa kawaida anapomuangalia (they don't attract much attention to the ordinary people)
Imekaa vizuri hii.. Kwa maneno mengine watu ambao wana blend in kirahisi na hawana identifiable patterns/attributes zinazoweza kuwatofautisha na watu kawaida
 
Fuatana nami.....

Mpelelezi ni mtu anayekusanya taarifa za adui , mshindani wa biashara au serikali adui ila saa nyingine mpelelezi huyo anaweza kufanya kazi ya kumpeleleza adui ila akamgeuka basi wake aliyemtuma kwa sababu mbalimbali .

Mtu huyu huwa anakusanya taarifa hizi kwa siri kwa kuangalia , kusikiliza , kufuatilia na kutumia vifaa vingine kutokana na ukuaji wa tekinolojia lakini lengo ni lile lile kupata taarifa za siri bila mhusika , wahusika kujua kwamba taarifa zao zinachukuliwa .

Shuguli za upelelezi zimekuwepo kwa miaka mingi toka binadamu ameanza kuishi duniani na kila kipindi zinabadilika utokana na ukuaji wa binadamu kimbinu , vifaa na wahusika wenyewe .

Kutokana na kukua kwa tekinologia watu wengi wametumia tekinologia hizo kukusanya taarifa na kuacha njia za asili ya upelelezi ambazo wakati mwingine ni sahihi kabisa kwa wakati huu .

Ili jamii Fulani isonge mbele kwenye maendeo Fulani ni vizuri iwekeze sana kwenye nyenzo na vitendo vya kipelelezi na hujuma kwa kuwa na watu wazuri kila sehemu pamoja na vifaa.

Labda tujiulize sasa kwanini kuna upelelezi , kwanini watu wanakuwa wapelelezi , mtu anavutiwa kukusanya taarifa za siri za mtu au kampuni au serikali nyingine kwa njia ya siri ?

Kwa kweli hakuna maana moja ya kwanini mtu anaamua kuwa mpelelezi au anaamua kusaliti wenzake kwenye upelelezi na kwenda upande wa adui lakini kuna vichocheo vinne vikuu ambavyo vinatumika kwenye shuguli hizi .

Kitu ambacho kinaweza kuwa namba moja ni hela , fedha au uchumi . kama nchi jirani imeshindwa kabisa kuingiza wapelelezi ndani ya baraza la mawaziri ili kupata taarifa kutumia njia za kawaida basi pesa inaweza kutumika katika kuhonga watu haswa wasaidizi au mawaziri wenyewe hata viongozi wengine ili kupata taarifa wanazozitaka .

Ushindani wa viwanda na biashara kati ya nchi au kampuni unategemeana sana na fedha ambazo hutolewa kwa wapelelezi au wachunguzi wengine ili kupata siri za mshindani wake sokoni au popote .
Katika shuguli za kijeshi zinazofanywa na nchi moja dhidi ya nyingine au vikundi vya kigaidi na vya kihalifu fedha hutumika sana na mfano hao ni tunaposikia kuhusu kundi la al shabab kuhonga baadhi ya polisi wa mipakani ili wavushe silaha na watu kwa ajili ya kufanya mashambulizi au wapewe taarifa mapema wakati polisi wanapofanya msako kwenye maeneo yao .

Kichocheo cha pili ni Itikadi ambayo ni Msimamo au mtazamo kuhusu masuala Fulani ya kimaisha , dini , imani , uongozi na mengine mengi hapa kwenye itikadi ndio makundi mengi ya kigaidi yanachipukia na kupata watu wa kujiunga nao wakifuata mtizamo na misimamo ya imani yao . vyama vya siasa navyo vinapata wafuasi wao kutokana na hili la itikadi ingawa wengine wanaweza kuwa sio wasomi wa itakadi wala kuielewa wanafuata mkumbo mpaka wanapoumizwa au kuumiza wengine ndio wanashtuka kitu ambacho wanakuwa wamechelewa .

Kwahiyo ili uwe mpelelezi mzuri wa kundi la kigaidi lazima uelewe itakadi yao , nchi , vikundi au vyama vya siasa na vikundi vingine vya siri .

Ili serikali na wadau wengine waweze kukabiliana na vikundi vya kigaidi ni vizuri kuwekeza sana kwenye suala la kujua itikadi za vikundi wanavyopambana navyo .

Hapa kwenye itikadi ndipo uzalendo unatakiwa kujengwa kwa vijana , watoto na wengine kwenye taasisi za elimu ili wasiweze kuangukia kwenye mikono ya wahalifu na maadui wengine kutokana na itikadi zao mfano china wana ukomunisti , nchi za magaribi wana itikadi zao na mengine mengi .

Wakati mwingine watu au mtu anaweza kuingia kwenye makubaliano na adui baada ya kukamatwa akifanya upelelezi au hata kabla lakini adui anaweza kuona yeye anafaa akampa mafunzo na mbinu nyingine ili aweze kupelelezi kwa niaba ya adui huyo mwisho wa makubaliano kama haya mara nyingi ni watu kuuwawa na hujuma nyingine nyingi dhidi ya nchi yake au watu wake wa karibu .

Mmoja wa wapelelezi maarufu kwenye suala hili anaitwa Kamanda Zig Zag , yeye alikua mfungwa kwenye gereza la uingereza kwenye kisiwa Fulani kisiwa hicho kilivyotekwa na wajerumani yeye akaandika barua kutaka kujiunga na jeshi la kijerumani baada ya muda alipelekwa ufaransa kwa mafunzo kisha akatumwa uingereza ili akalipue kiwanda cha kutengeneza ndege za kivita . Alivyotua uingereza akatoa taarifa kwa mamlaka za uingereza sasa akawa upande wa uingereza tena akatengeneza mlipuko bandia na kuaminisha wajerumani kwamba kweli kimelipuliwa kisha waingereza wakamtuma arudi ujerumani kwahiyo akawa mpelelezi wa uingereza ndani ya ujerumani .wajerumani walimtuma maeneo mengi ulaya kwa kudhani anawasaidia kumbe taarifa zote zilikuwa zinaenda kwao uingereza .

Kuna wakati mtu analazimika kufanya upelelezi dhidi ya mtu au watu baada ya nguvu kutumika au kulazimishwa ili labda asiuwawe au ndugu zake wa karibu asiuwawe mara nyingi wanaweza kutumika wapenzi na wapendwa wengine ili mtu afikie muafaka wa kufanya upelelezi dhidi ya nchi , kampuni , washirika na wengine wa karibu .

Hapa kwenye nguvu wakati mwingine mtu anaweza kusingiziwa kitu au kuingizwa kwenye kashfa au kutengenezwa uwongo ili akubali kufanya upelelezi dhidi ya wengine lakini sio kwa hiari yake .

Pia kuna suala la umuhimu au umaarufu wa mtu au uzuri wake , kuna watu wengi maarufu kama wanamuziki au wacheza mpira na warembo wanatumia fursa hiyo kufanya upelelezi dhidi ya maadui wa nchi zao au washindani wa kibiashara wanajua kwa kutumia njia hiyo wanaweza kuingia chumbani , kulala na wanaume au wanawake , kuchungulia simu au kuweka vinasa Sauti , kujua marafiki au ndugu wa karibu , mipango ya biashara na mengine mengi .

Baadhi ya watu haswa vijana wanajiingiza au wanaweza kuingizwa kwenye shuguli za kipelelezi kwa wao kupenda vile wanavyoona kwenye sinema au kusoma vitabu au kuhadithiwa na wao wanaamua kujihusisha na upelelezi lakini bila kuwa na mafunzo au mtu yoyote anayemuongoza kwenye mambo mbalimbali anayotakiwa kufanya .

Wengine wanaweza kuwa wapelelezi wazuri ndani ya polisi , majeshi na kampuni lakini hawalipwi vizuri au hawaridhiki na baadhi ya vitu matokeo yake ni kuuza siri na mikakati mengine kwa wapinzani au maadui ili kuweza kuleta mabadiliko na mengine ndani ya taasisi yake au kuiua kabisa isiwepo .

Mahusiano binafsi kati ya watu au mtu ni moja ya kichocheo kikubwa cha watu kuweza kufanya upelelezi mara nyingi yanaweza kuwa mahusiano ya kifamilia kuoleana , kuowa au kuolewa hii maarufu inaitwa HONEY TRAP na hii ni ngumu kugundulika kwa sababu ni mambo binafsi sana na yanaweza kuchukua muda mrefu kwenda vizazi na vizazi viongozi na viongozi .

Kama nilivyosema hapo juu upelelezi umeanza siku nyingi na kila jamii inategemea upelelezi ili iweze kujua mwingine ili kuweza kupambana au kushindana nae ili aweze kuwa juu kwenye mambo mbalimbali na upelelezi umebadilika kwa kiasi kikubwa sana .

Ni vizuri taasisi zetu kuwekeza vizuri kwenye upelelezi kupata vijana hodari , wapewe mafunzo ya kutosha , mishahara , motisha , vifaa na kuzidi kuwaongezea ujuzi ili kuweza kupambana katika dunia ya sasa ya sayansi na tekilologia .

Upelelezi usiishie ndani ya jeshi la polisi au JKT , au Usalama wa Taifa tu , hata vyuo vinatakiwa kuwa na wapepelelezi , kampuni za nchini zinatakiwa kuwa na wapepepezi , mashirika ya umma yanatakiwa kuwa na wapelelezi , viwanda vya ndani vinatakiwa kuwa na wapelelezi na wote hawa wanatakiwa kufanya kazi pamoja ili kuleta maendeleo kwa jamii ya watanzania .

Nchi za wenzetu zinaendelea na kuendeleza ushindani mkubwa kwenye nyanja hii , uchina ilishtuka ikapeleka wapelelezi nchi nyingi ili wakalete tekinolojia na maarifa kwao sasa wako mbali , wakati wa vita kuu ya dunia wamarekani waliiba wanasayansi wengi wa ujerumani ambao walisaidia kujenga uwezo mkubwa wa jeshi la marekani na taasisi nyingine ndio maana ikawa mbabe wa dunia kwa kipindi kirefu .

Kumbuka kazi za upelelezi ni ngumu na zenye siri nyingi na kubwa sana , wapelelezi wengi pia wana mafunzo ya kujilinda , kupambana na kushambulia usijaribu kupambana nae kama una uhakika ni bora kutoa taarifa kwa vyombo husika wamshugulikie .

Mwisho upelelezi usitumike katika kutafuta taarifa mbaya tu , hapana , kuna taarifa nyingine nzuri zinaweza kutumika vyuoni , wizarani , kwenye majeshi na sehemu nyingine kwa ajili ya kuboresha au kujenga zana na vifaa vya kisasa

LENGO LA MAELEZO/MAKALA HAYA NI KUFUNDISHA, UKIKAMATWA KWA KAZI HIZI UNAWEZA KUUWAWA , KUTESWA NA KUPOTEZA MENGI.

Mkala haya ni marudio, kwa mara yakwanza niliandika April 21, 2011

.............................

"Kuna watu wasipokuelewa maneno na matendo yako, mshukuru Jah, wewe bado unafikra chanya, wakianza kukuelewa jichunguze ni wapi umeanguka maana umeanza kuwaza kama wao"
My braza Yericko,
Tofautisha upelelezi na intelijensia. Unachokiongelea ni intelijensia na sio upelelezi.
Upelelezi Mara nyingi unakuwa ktk kugundua mbinu za wahalifu, kosa, ama wahusika wa uhalifu kwa kukusanya uchunguzi wao
 
Fuatana nami.....

Mpelelezi ni mtu anayekusanya taarifa za adui , mshindani wa biashara au serikali adui ila saa nyingine mpelelezi huyo anaweza kufanya kazi ya kumpeleleza adui ila akamgeuka basi wake aliyemtuma kwa sababu mbalimbali .

Mtu huyu huwa anakusanya taarifa hizi kwa siri kwa kuangalia , kusikiliza , kufuatilia na kutumia vifaa vingine kutokana na ukuaji wa tekinolojia lakini lengo ni lile lile kupata taarifa za siri bila mhusika , wahusika kujua kwamba taarifa zao zinachukuliwa .

Shuguli za upelelezi zimekuwepo kwa miaka mingi toka binadamu ameanza kuishi duniani na kila kipindi zinabadilika utokana na ukuaji wa binadamu kimbinu , vifaa na wahusika wenyewe .

Kutokana na kukua kwa tekinologia watu wengi wametumia tekinologia hizo kukusanya taarifa na kuacha njia za asili ya upelelezi ambazo wakati mwingine ni sahihi kabisa kwa wakati huu .

Ili jamii Fulani isonge mbele kwenye maendeo Fulani ni vizuri iwekeze sana kwenye nyenzo na vitendo vya kipelelezi na hujuma kwa kuwa na watu wazuri kila sehemu pamoja na vifaa.

Labda tujiulize sasa kwanini kuna upelelezi , kwanini watu wanakuwa wapelelezi , mtu anavutiwa kukusanya taarifa za siri za mtu au kampuni au serikali nyingine kwa njia ya siri ?

Kwa kweli hakuna maana moja ya kwanini mtu anaamua kuwa mpelelezi au anaamua kusaliti wenzake kwenye upelelezi na kwenda upande wa adui lakini kuna vichocheo vinne vikuu ambavyo vinatumika kwenye shuguli hizi .

Kitu ambacho kinaweza kuwa namba moja ni hela , fedha au uchumi . kama nchi jirani imeshindwa kabisa kuingiza wapelelezi ndani ya baraza la mawaziri ili kupata taarifa kutumia njia za kawaida basi pesa inaweza kutumika katika kuhonga watu haswa wasaidizi au mawaziri wenyewe hata viongozi wengine ili kupata taarifa wanazozitaka .

Ushindani wa viwanda na biashara kati ya nchi au kampuni unategemeana sana na fedha ambazo hutolewa kwa wapelelezi au wachunguzi wengine ili kupata siri za mshindani wake sokoni au popote .
Katika shuguli za kijeshi zinazofanywa na nchi moja dhidi ya nyingine au vikundi vya kigaidi na vya kihalifu fedha hutumika sana na mfano hao ni tunaposikia kuhusu kundi la al shabab kuhonga baadhi ya polisi wa mipakani ili wavushe silaha na watu kwa ajili ya kufanya mashambulizi au wapewe taarifa mapema wakati polisi wanapofanya msako kwenye maeneo yao .

Kichocheo cha pili ni Itikadi ambayo ni Msimamo au mtazamo kuhusu masuala Fulani ya kimaisha , dini , imani , uongozi na mengine mengi hapa kwenye itikadi ndio makundi mengi ya kigaidi yanachipukia na kupata watu wa kujiunga nao wakifuata mtizamo na misimamo ya imani yao . vyama vya siasa navyo vinapata wafuasi wao kutokana na hili la itikadi ingawa wengine wanaweza kuwa sio wasomi wa itakadi wala kuielewa wanafuata mkumbo mpaka wanapoumizwa au kuumiza wengine ndio wanashtuka kitu ambacho wanakuwa wamechelewa .

Kwahiyo ili uwe mpelelezi mzuri wa kundi la kigaidi lazima uelewe itakadi yao , nchi , vikundi au vyama vya siasa na vikundi vingine vya siri .

Ili serikali na wadau wengine waweze kukabiliana na vikundi vya kigaidi ni vizuri kuwekeza sana kwenye suala la kujua itikadi za vikundi wanavyopambana navyo .

Hapa kwenye itikadi ndipo uzalendo unatakiwa kujengwa kwa vijana , watoto na wengine kwenye taasisi za elimu ili wasiweze kuangukia kwenye mikono ya wahalifu na maadui wengine kutokana na itikadi zao mfano china wana ukomunisti , nchi za magaribi wana itikadi zao na mengine mengi .

Wakati mwingine watu au mtu anaweza kuingia kwenye makubaliano na adui baada ya kukamatwa akifanya upelelezi au hata kabla lakini adui anaweza kuona yeye anafaa akampa mafunzo na mbinu nyingine ili aweze kupelelezi kwa niaba ya adui huyo mwisho wa makubaliano kama haya mara nyingi ni watu kuuwawa na hujuma nyingine nyingi dhidi ya nchi yake au watu wake wa karibu .

Mmoja wa wapelelezi maarufu kwenye suala hili anaitwa Kamanda Zig Zag , yeye alikua mfungwa kwenye gereza la uingereza kwenye kisiwa Fulani kisiwa hicho kilivyotekwa na wajerumani yeye akaandika barua kutaka kujiunga na jeshi la kijerumani baada ya muda alipelekwa ufaransa kwa mafunzo kisha akatumwa uingereza ili akalipue kiwanda cha kutengeneza ndege za kivita . Alivyotua uingereza akatoa taarifa kwa mamlaka za uingereza sasa akawa upande wa uingereza tena akatengeneza mlipuko bandia na kuaminisha wajerumani kwamba kweli kimelipuliwa kisha waingereza wakamtuma arudi ujerumani kwahiyo akawa mpelelezi wa uingereza ndani ya ujerumani .wajerumani walimtuma maeneo mengi ulaya kwa kudhani anawasaidia kumbe taarifa zote zilikuwa zinaenda kwao uingereza .

Kuna wakati mtu analazimika kufanya upelelezi dhidi ya mtu au watu baada ya nguvu kutumika au kulazimishwa ili labda asiuwawe au ndugu zake wa karibu asiuwawe mara nyingi wanaweza kutumika wapenzi na wapendwa wengine ili mtu afikie muafaka wa kufanya upelelezi dhidi ya nchi , kampuni , washirika na wengine wa karibu .

Hapa kwenye nguvu wakati mwingine mtu anaweza kusingiziwa kitu au kuingizwa kwenye kashfa au kutengenezwa uwongo ili akubali kufanya upelelezi dhidi ya wengine lakini sio kwa hiari yake .

Pia kuna suala la umuhimu au umaarufu wa mtu au uzuri wake , kuna watu wengi maarufu kama wanamuziki au wacheza mpira na warembo wanatumia fursa hiyo kufanya upelelezi dhidi ya maadui wa nchi zao au washindani wa kibiashara wanajua kwa kutumia njia hiyo wanaweza kuingia chumbani , kulala na wanaume au wanawake , kuchungulia simu au kuweka vinasa Sauti , kujua marafiki au ndugu wa karibu , mipango ya biashara na mengine mengi .

Baadhi ya watu haswa vijana wanajiingiza au wanaweza kuingizwa kwenye shuguli za kipelelezi kwa wao kupenda vile wanavyoona kwenye sinema au kusoma vitabu au kuhadithiwa na wao wanaamua kujihusisha na upelelezi lakini bila kuwa na mafunzo au mtu yoyote anayemuongoza kwenye mambo mbalimbali anayotakiwa kufanya .

Wengine wanaweza kuwa wapelelezi wazuri ndani ya polisi , majeshi na kampuni lakini hawalipwi vizuri au hawaridhiki na baadhi ya vitu matokeo yake ni kuuza siri na mikakati mengine kwa wapinzani au maadui ili kuweza kuleta mabadiliko na mengine ndani ya taasisi yake au kuiua kabisa isiwepo .

Mahusiano binafsi kati ya watu au mtu ni moja ya kichocheo kikubwa cha watu kuweza kufanya upelelezi mara nyingi yanaweza kuwa mahusiano ya kifamilia kuoleana , kuowa au kuolewa hii maarufu inaitwa HONEY TRAP na hii ni ngumu kugundulika kwa sababu ni mambo binafsi sana na yanaweza kuchukua muda mrefu kwenda vizazi na vizazi viongozi na viongozi .

Kama nilivyosema hapo juu upelelezi umeanza siku nyingi na kila jamii inategemea upelelezi ili iweze kujua mwingine ili kuweza kupambana au kushindana nae ili aweze kuwa juu kwenye mambo mbalimbali na upelelezi umebadilika kwa kiasi kikubwa sana .

Ni vizuri taasisi zetu kuwekeza vizuri kwenye upelelezi kupata vijana hodari , wapewe mafunzo ya kutosha , mishahara , motisha , vifaa na kuzidi kuwaongezea ujuzi ili kuweza kupambana katika dunia ya sasa ya sayansi na tekilologia .

Upelelezi usiishie ndani ya jeshi la polisi au JKT , au Usalama wa Taifa tu , hata vyuo vinatakiwa kuwa na wapepelelezi , kampuni za nchini zinatakiwa kuwa na wapepepezi , mashirika ya umma yanatakiwa kuwa na wapelelezi , viwanda vya ndani vinatakiwa kuwa na wapelelezi na wote hawa wanatakiwa kufanya kazi pamoja ili kuleta maendeleo kwa jamii ya watanzania .

Nchi za wenzetu zinaendelea na kuendeleza ushindani mkubwa kwenye nyanja hii , uchina ilishtuka ikapeleka wapelelezi nchi nyingi ili wakalete tekinolojia na maarifa kwao sasa wako mbali , wakati wa vita kuu ya dunia wamarekani waliiba wanasayansi wengi wa ujerumani ambao walisaidia kujenga uwezo mkubwa wa jeshi la marekani na taasisi nyingine ndio maana ikawa mbabe wa dunia kwa kipindi kirefu .

Kumbuka kazi za upelelezi ni ngumu na zenye siri nyingi na kubwa sana , wapelelezi wengi pia wana mafunzo ya kujilinda , kupambana na kushambulia usijaribu kupambana nae kama una uhakika ni bora kutoa taarifa kwa vyombo husika wamshugulikie .

Mwisho upelelezi usitumike katika kutafuta taarifa mbaya tu , hapana , kuna taarifa nyingine nzuri zinaweza kutumika vyuoni , wizarani , kwenye majeshi na sehemu nyingine kwa ajili ya kuboresha au kujenga zana na vifaa vya kisasa

LENGO LA MAELEZO/MAKALA HAYA NI KUFUNDISHA, UKIKAMATWA KWA KAZI HIZI UNAWEZA KUUWAWA , KUTESWA NA KUPOTEZA MENGI.

Mkala haya ni marudio, kwa mara yakwanza niliandika April 21, 2011

.............................

"Kuna watu wasipokuelewa maneno na matendo yako, mshukuru Jah, wewe bado unafikra chanya, wakianza kukuelewa jichunguze ni wapi umeanguka maana umeanza kuwaza kama wao"
 
Mkuu, kuna vyuo vyovyote binafsi vinavyotoa taaluma hii ya upelelezi/ujasusi?
 
Back
Top Bottom