Ujauzito miezi minne (4) baada ya kujifungua

Malolella

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2012
Posts
366
Reaction score
114
Wana jf popote mlipo heshima kwenu. Nawapongeza kwa mawazo na michango yenu kila panapohtajika ushauri. Kuna rafiki yangu ambaye mkewake kajifungua miezi mi4 iliyopita na kwa bahati mbaya ameconceive tena. Kiukweli wote wamechanganyikiwa yani mke na mume, wamekuja kuniomba msaada wa mawazo wafanyaje maana wanasema itakuwa ni aibu ya mwaka. Nami nikaona niwaombe mawazo yenu ili2jue tunamsaidiaje huyu rafiki. Aksanteni na mbarikiwe..karibu kwa michango ya mawazo yenu.
 
Maisha unapanga mwenyewe na kuishi mwenyewe! Aibu inatoka wapi nao wanaishi kihalali kama couple?

Muambie uuaji sio mzuri. Waendelee kulea mimba huku mtoto akiendelea kunyonya. Mimba ikifika miezi 7 aache kunyonyesha na mtoto apewe maziwa. Na hakuna kubemenda hapo, dogo apate msosi wa kutosha!
 
Mtoto siku zote huwa ni baraka. Hata hivyo mtoto ambaye wazazi hawakupanga kumpata na hasa kama hakupishana muda wa kutosha na mwenzake aliyetangulia inaweza kuwa shida kwa wazazi, kwa mtoto aliyetangulia ambaye bado ni mdogo sana na hata kwake yeye mwenyewe. Sidhani kama kuna ushauri utakaoweza kukubalika na pande zote. Kiafya mama bado anahitaji muda wa kupumzika baada ya kujifungua mtoto aliyetangulia na mwili wake bado unahitaji kujijenga upya baada ya uzazi. Hata hivyo ushauri ninaoweza kuchangia ni kuwa wawasiliane na madaktari bingwa wa masuala ya uzazi (obstetricians na gynaecologists) ambao wao wataweza kuwapa ushauri wa kitaalamu zaidi.
 
Waambie wamshukuru Mungu na awaombe awaongezee baraka maishani, wala sio aibu kabisa huwa inatokea kwa wengi, watoto watapishana kama zaidi ya mwaka.

waambie wasijaribu kutoa huyo anaweza akawa wa mwisho kwao.

nasema tena aina tabu kabisa hata hapa nchini wengi wana watoto hivyo, watakaowasema wawaambie ni baraka za Mungu na wanashukuru.

sielewi kwanini waone aibu, je wangekuwa hawawezi kuzaa kabisa wangeona aibu pia au ndio wangechekwa, mtu akiwashauri watoe eti karibu sana basi huyo hana mema nao.

I hope na wewe hujawashauri wamuue mtoto huyo tumboni, ni dhambi kaa kimya waambie washukuru Mungu wasubirie mtoto.
 
Hofu yao ni kupata mimba haraka.Baraka ni Watoto na Mungu ameleta wajiandae vzr kuwalea wote.
Kumbuka kuna watu wanatafuta hizo Baraka usiku na mchana imeshindikana,kuuwa ni kubaya huwezi jua kuwa hiyo huenda ni mimba yenu ya mwisho.
Leeni halafu msisikilize maneno ya watu wasio watakia mema daima.
 
huyo m/ume nae ameshindwa kuvumilia ndani ya miezi minne tu keshamtungua mwenzake mimba nyingine lol, kusema ukweli ni aibu mtu kushindwa kuvumilia pia w/ume tuwe tunaomba ushauri kwa waliotutangulia jinsi ya kujizuia haya mambo si angetafuta hata mpango wa kando umpe kampani kipindi wanalea
 
Sasa hapo shida iko wapi? Mbona watu mnapenda ku-complicate maisha hivyo?
 
huyo baba anachekesha kweli.aibu ya nini jamani?si mke wake?hao watoto watakua pamoja,hiyo ni baraka bwana.wengine wanawatafuta hao watoto hawawapati.amsaidie mke wake kulea mimba.usimshauri akaitoe.
 
Eti aibu, ujauzito baada ya miezi 4 kujifungua....! raha gani hiyo? kubwa ni kushukuru Mola kwa hali hiyo, King'asti ametoa ushauri mzuri mno juu ya kuweza kuendelea kufurahia maisha!
 
safi sana,baba amelenga,watoto watakuwa mabesti na hamna kwenda kucheza kwa jirani tena......ni baraka......waliozaliwa in gaps kama mimi tungetamani sana tupishane miaka michache....sio unakuwa na kaka yako kakuzidi miaka kumi na mdogo wako umemzidi miaka 10....wailee vyema,na mama apate lishe poa.
 
Nashukuru sana wadau kwa mawazo/michango yenu mizuri. Nilimhoji kwanini hak2mia kinga au njia ya uzazi wa mpango! Akaniambia hajawahi kumwaga ndani kwani alikuwa akikaribia anatoa na kumwaga nje, hivyo hata wao wanashangaa kulikoni. Hapa wote tumepata fundisho kuwa kumwaga nje co njia ya kuzuia mama kupata mimba.
 


Unataka wabemende mtoto wewe, kichanga wa mwaka mmoja na miezi nae atakuwa na mdogo wake aibu sana
 
Waambie tu wakunbuke ile moja ya Amri kumi za Mungu isemayo..."THOU SHALL NOT MURDER!" Mtoto huyo ni baraka kutoka mbinguni, hata Mungu mwenyewe alisema," NILIKUCHAGUA HATA KABLA SIJAKUUMBIA TUMBONI MWA MAMA YAKO".Thanx
 
aibu kuliko kuua? kwani watu wangapi wamepishana mwaka mmoja tuuu? afu mwaka mmoja na miezi sio kichanga huyo, anatembea kabisa. kule umasaini kwetu anafaa kuchumbia kabisa:bowl:
Unataka wabemende mtoto wewe, kichanga wa mwaka mmoja na miezi nae atakuwa na mdogo wake aibu sana
 

Mke na Mune waote wamechanganyikiwa?! Sijaelewa kwa nini wamechanganyikiwa., kwani wametosheka na idadi ya watoto walionao au ni vile kapata ujauzito mwingine ingali anakichanga cha miezi 4!??
 
Mie wa kwangu ana miezi minne na nusu. Mfano ndio mie napata uja uzito wala sitoi japokuwa nlijifungua kwa operation. Nazaa.
 
Tell them to live their life. Naamini ni watu wazima na wamekua,yaani wameshalizidi umri lile suala la "watu watatuonaje". Halafu waambie wamwone daktari (I mean daktari mzuri) awashauri namna ya kufanya kwa ajili ya afya ya dogo,mama na dogo mpendwa (I love him/her already...I can smell the evil one plotting against that precious life,..na Ashindwe katika JINA la YESU!!) aliyemo tumboni.
Pia si jambo la ajabu watoto kupishana kwa mwaka 1 +, infact ina faida zake nyingi tu chache tu zikiwa mama kutumia muda mfupi kumaliza shughuli ya uzazi na urahisi wa malezi (sio wazazi mnalea generations mbili tofauti, first born yupo college last born yupo baby class...haaaaa!!)
ABOVE ALL ELSE waambie wasijaribu kuwazia kuwaza kuua mtoto wao (they call it abortion)!!
 
aibu kuliko kuua? kwani watu wangapi wamepishana mwaka mmoja tuuu? afu mwaka mmoja na miezi sio kichanga huyo, anatembea kabisa. kule umasaini kwetu anafaa kuchumbia kabisa:bowl:

:confused2::confused2::confused2: hawa wazazi watageuka kituko katika jamii wanayo ishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…