Ujauzito nnje ya mfuko

Home First

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2013
Posts
609
Reaction score
247
Wadau habari zenu! Tafadhali naomba kujuzwa kwa anaejua.

Hivi mimba inapokuwa imetunga nnje ya mfuko wa uzazi ni sherti itolewe au kuna njia nyingine mm'badala wa mimba kuendelea kuwepo?!

Nimeuliza hili maana nimekwenda hospitali nikapimwa nakuambiwa mimba yangu iko nnje yamfuko inatakiwa kufanyiwa Op, nikafanyiwa kwa kuondosha ujauzito wangu! Imeniuma ila sijui kama ndivyo ilivyo, naombeni kujuzwa afadhali,

Jokes pembeni.

Nawasilisha.
 
Pole sana dada hiyo ndo njia pekee ya kuokoa maisha yako na kizazi chako.wakiacha iendelee kukuwa itapasua mirija ya uzazi na hatimaye ingeweza kukufanya usizae tena au kupoteza damu nyingi hali ambayo inahatarisha maisha yako...

Lakini pia mtoto hawezi kukua nje ya mfuko wa kizazi na sio mazingira sahihi kwake.

Jitahidi kutoshika tena mimba kwa minimum miezi sita ili kizazi kiwe stable.

Kula vyakula vya kujenga mwili na kuwa free from stress.Pia mpe shem lishe nzuri ili kuandaa mbegu bora kwa ajili ya mtoto.

Watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu Mwamini nawe utafanikiwa na kupata watoto na uzao wa tumbo lako.
 
.....ectopic hiyo, ilikuwa lazima iondolewe. Pata ushauri wa Gynecologist (daktari bingwa wa kina mama) pia Omba sana kwa mwenyezi mungu, kuna chances ya tatizo hili kujirudia.
 
there isn't sadly. ectopic pregnancy inabidi kuondolewa kuokoa maisha ya mama.
 
pole sana aiseee nimeumia mpenzi pole sana Inshaallah utapata mtoto mwingine na kwa kudra ya Mwenyezi Mungu tatizo halitojirudia
 
Sio NNJE, ni NJE

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Just PM , Nitakupa number ya Daktari Bingwa wa wanawake ambaye anaweza kukusaidia au kukupa ushauri zaidi. @ Home First
 

Ushatoa alafu ndo unataka ushauri hata kama ukipata itakusaidia nini? Ungeomba kabla ya apo ningekuona wa maana!
 
ushatoa alafu ndo unataka ushauri hata kama ukipata itakusaidia nini? Ungeomba kabla ya apo ningekuona wa maana!
kuna binadamu wengine kweli hamna utashi wala huruma,ivi ni kweli umechukua muda wako kusoma vizuri au ndo walewale wa kukurupuka na kusaini mikataba mibovu?amekwambia alivyoenda hospitalini wakamtoa na kumbuka pengine kwa hatari iliyokuwepo walimfanyia ili kumuokoa na si kwamba yeye alipenda vyovyote vile asingependa kutoa then aje hapa kuomba ushauri....kuwa na utu basi japo kidogoooo!!
 
pole dear dawa ya hii kitu nikufanya kama ulivyofanywa, hata mie ilinitokea........
 
Sorry hili tatizo la mimba kuwa nje ya mfuko wa uzazi huwa linakuwa tatizo la mwanamke au mwanaume?
 
pole sana dadangu.Mungu ni mwema mtumaini yeye anajibu zaidi ya pole tutakazo kupa binadam hasa marafiki.La msingi ni kumshukuru MUNGU angali una kizazi,na watotot wanatoka kwa Mungu na ni kusudi lake uzae..
 
Sorry hili tatizo la mimba kuwa nje ya mfuko wa uzazi huwa linakuwa tatizo la mwanamke au mwanaume?
Tatizo huwa kwa anayebeba mimba, yupi Kati ya uliowataja huwa anabeba mimba?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…