DOKEZO Ujenzi holela kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti

DOKEZO Ujenzi holela kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Anonymous

Senior Member
Joined
Apr 6, 2006
Posts
118
Reaction score
339
Habari zenu wakuu,

Tukubaliane tu kwamba utalii unatutangaza, unatuingizia fedha za kigeni, kuinua uchumi na kutoa ajira. Lakini utalii usiposimamiwa vizuri madhara yake ni mtambuka na ni makubwa sana!

Ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuna mwamba mmoja anaendelea na ujenzi wa hoteli ya watalii (Hii hapa Serengeti Lake Magadi Lodge | Wellworth Collection Hospitality ). Juu kabisa ya mlima. Usiku akiwasha taa zake anamulika mbuga nzima. Yaani ni kama lightouse, taa imewekwa kilingeni kabisa kuongoza watu usiku.

Ujenzi huo ni kinyume kabisa cha sheria za hifadhi na sheria ya mazingira. Zoning pia inaonesha kuwa eneo lenyewe ni tengefu kwa ajili mazalia ya wanyamapori hasa Faru, Simba, Chui n.k. Kwenye hili watalii wanakerwa sana!

Halafu bado kuna zile changamoto za Kambi za kuhama hama kurundikwa sehemu moja hasa kule Kogatende na Ndutu! Na hivi utalii unavorudi kwa kasi, tusipokuwa makini tutajiharibia wenyewe.

Ajabu ni kwamba wanakazana kuandika "Serengeti shall Naver Die" Lakini kwa matamaa ya fedha wanazidi kuiua!

Tupaze sauti zetu haya masuala ya ujenzi holela yakome. Ifike mahali wenye mamlaka wangetanguliza misingi ya taaluma zao na uzalendo wasitishe vituko kama hivi hifadhini.

TAZ_20201014_YF_1.jpg

Screenshot 2023-06-25 at 00.55.53.png

wellworth-serengeti-lake.jpg

Serengeti-Lake-Magadi-Lodge258.jpeg

Hoteli inajengwa kileleni mwa mlima. Yaani, juu ya mlima ni hoteli yenyewe (lounge/main areas)... Rooms za wageni zimesambaa juu ya mwinuko kuelekea upande wa ziwani (Lake Magadi).

Hiyo sehemu na majengo yanayoonekana chini ni yalipo makazi ya staff.

IMG-20230527-WA0020(1).jpg


Kwa ujumla maeneo husika ni mazalia ya wanyamapori hasa chui. Na ni maeneo maarufu sana kwa migration ya wanyama upande wa central Serengeti kabla hawajaelekea Moru na Southern Corridors.

SHERIA ZIPI ZINAHUSIKA?

1. Sheria ya Mazingira (EMA #20 ya mwaka 2004, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2018) - anzia kuasoma Sehemu VI ibara ya 81-85, 89-90, 92-97, 161, 184, 193, 198 n.k

2. NEMC EIA na Audit Regulations 2005 na 2018.

3. Tourism Investment Manual pia

NB:
1. Wachunguzi wa mambo wanahisi janja janja nyingi ndani ya SENAPA yametokea baada ya GMP kuisha muda wake.

2. Kuna usiri mkubwa unaotia mashaka kwenye mchakato wa EIA, ukizingatia unyeti wa eneo la Lake Magadi.

3. Kwa unyeti wa eneo husika la mradi haiwezekani na ni very unprofessional kwa EIA kuanza na kukamilika ndani ya mwaka mmoja (kwa mujibu wa maelezo yanayoibua mashaka ya msemaji wa TANAPA HQ). Wataalamu wanajua kuwa EIA huchukua muda mrefu kiasi (field - rejea NEMC audit regulations 2005).

4. Ili kulinda maslahi ya wawekezaji wengine ndani ya hifadhi - TANAPA'S TOURISM INVESTMENT MANUAL inaelekeza minimum distance ya 10kilometers kutoka accommodation facility moja hadi nyingine. Well-worth Collection's Lake Magadi Lodge pamoja na kupachikwa juu ya kilima na taa zake kusumbua wageni kwenye lodges za jirani ujenzi wake haukuzingatia umbali elekezeki!

REJEA:

TANZANIA ENVIRONMENTAL MANAGEMENT ACT, 2004

TANZANIA ENVIRONMENTAL IMPACT ASSESSMENT AND AUDIT REGULATIONS, 2005

TANZANIA NATIONAL PARKS ACT

Serengeti National Park Rules | Tanzania

General Management Plan (2006-2016), Serengeti National Park, Tanzania

Ieleweke kuwa, Watalii mbalimbali, Wawekezaji, Wafanyakazi (hata wa TANAPA wenyewe) na waongoza utalii (tour guides) wenye uzoefu wa muda mrefu kuhusu utalii na uhifadhi hawaridhishwi na uwekezaji wa Wellworth Collection ndani ya SENAPA!
 
Kwanza nani kawaambia Mbiga za Wanyama ndio utalii pekee wa maana Duniani? Unajua Watalii wanao tembelea egypt ni Million 15 kwa mwaka? Huku sisi tukiwa na milion 1.5 kwa mwaka? Moroco i apata watalii million 10 na kwa mwaka.

Watalii wanao wanao penda kutembelea mbuga za Wanyama ni wachacha sana Duniani ukilinganisha na utaliu wa fukwe, au Maeneo ya Kihistoria na na Kale, Bahati Mbaya Bongo tumekalili mbuga za Wanyama wakati inaonekana fika sio idadi kubwa inapendelea kutazama wanyama, la sivyo Misiri isingekuwa inapata wataliu Million 15
 
Kwanza nani kawaambia Mbiga za Wanyama ndio utalii pekee wa maana Duniani? Unajua Watalii wanao tembelea egypt ni Million 15 kwa mwaka? Huku sisi tukiwa na milion 1.5 kwa mwaka? Moroco i apata watalii million 10 na kwa mwaka.

Watalii wanao wanao penda kutembelea mbuga za Wanyama ni wachacha sana Duniani ukilinganisha na utaliu wa fukwe, au Maeneo ya Kihistoria na na Kale, Bahati Mbaya Bongo tumekalili mbuga za Wanyama wakati inaonekana fika sio idadi kubwa inapendelea kutazama wanyama, la sivyo Misiri isingekuwa inapata wataliu Million 15
Knowledge gap ni hatari sana!
Ni kweli... Upo sahihi kabisa!
Kimantiki idadi ya watalii wanaoingia Tanzania na kufika Kariakoo Dar ni kubwa sana, sema hatujui kipi ni kipi!
 
Watu wa Ecologia wanatengeneza pesa za hatari make ndio kazi yao hio, wale ndio wanaamua upewe kibali au la, sasa ukiwa na pesa ndefu unapata kibali asubuji na mapema, Wanataka kuiharibi kama Masai Mara ilivyo haribiwa na utitili wa Hoteli
Tupaze sauti ndugu. Hali ni mbaya!
 
Tupaze sauti ndugu. Hali ni mbaya!
Unapazia nani sauti? Hizo ni Projects za watu, wacha wajenge kwanza kwa mabadiliko haya ya Tabia nchi ipo siku hizi hifadhi zitabaki na miti na majani pekee, kama swala la mazingira hakitatiliwa maanani
 
Shida nchi imekomaaa na Hifadhi za wanyama tu wakati kiuhalisia wanayama hawa attract watalii wengi kama vivutio vingine mfano Fukwe, Ncbi zenye utaliu wa fukwe zinapokea wataliii wengi mno kuliko hawa wanao kuja kutazama tembo na ndio hapo sasa tunakomaaa kujaza hoteli Serengeti na kwingineko, huku tukiharibu ikolojia
 
Kwanza nani kawaambia Mbiga za Wanyama ndio utalii pekee wa maana Duniani? Unajua Watalii wanao tembelea egypt ni Million 15 kwa mwaka? Huku sisi tukiwa na milion 1.5 kwa mwaka? Moroco i apata watalii million 10 na kwa mwaka.

Watalii wanao wanao penda kutembelea mbuga za Wanyama ni wachacha sana Duniani ukilinganisha na utaliu wa fukwe, au Maeneo ya Kihistoria na na Kale, Bahati Mbaya Bongo tumekalili mbuga za Wanyama wakati inaonekana fika sio idadi kubwa inapendelea kutazama wanyama, la sivyo Misiri isingekuwa inapata wataliu Million 15

Kwa hiyo hao wanaowekeza hizo vitu hawana akili ila wewe ndo unaona upo sawa?

Elewa kwanza maana ya uwekezaji kisha fikiria unachotaka kiwe kulinganisha na maeneo hayo.
 
Kwanza nani kawaambia Mbiga za Wanyama ndio utalii pekee wa maana Duniani? Unajua Watalii wanao tembelea egypt ni Million 15 kwa mwaka? Huku sisi tukiwa na milion 1.5 kwa mwaka? Moroco i apata watalii million 10 na kwa mwaka.

Watalii wanao wanao penda kutembelea mbuga za Wanyama ni wachacha sana Duniani ukilinganisha na utaliu wa fukwe, au Maeneo ya Kihistoria na na Kale, Bahati Mbaya Bongo tumekalili mbuga za Wanyama wakati inaonekana fika sio idadi kubwa inapendelea kutazama wanyama, la sivyo Misiri isingekuwa inapata wataliu Million 15
Lakini ndo utalii wetu unaotutambulisha Duniani! Si rahisi unavotaka kutuaminisha kuwa unaweza kuibua new attractions na zikashika kasi ghafla kupambana na hayo mataifa uliyoyataja!
That said, tusiruhusu hiko kidogo kilichopo kuharibiwa!!
 
Kwa hiyo hao wanaowekeza hizo vitu hawana akili ila wewe ndo unaona upo sawa?

Elewa kwanza maana ya uwekezaji kisha fikiria unachotaka kiwe kulinganisha na maeneo hayficha

Ficha ujinga wako kwa kukaa kimya!.
 
Habari zenu wakuu,

Tukubaliane tu kwamba utalii unatutangaza, unatuingizia fedha za kigeni, kuinua uchumi na kutoa ajira. Lakini utalii usiposimamiwa vizuri madhara yake ni mtambuka na ni makubwa sana!

Ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuna mwamba mmoja anaendelea na ujenzi wa hoteli ya watalii (Hii hapa Serengeti Lake Magadi Lodge | Wellworth Collection Hospitality ). Juu kabisa ya mlima. Usiku akiwasha taa zake anamulika mbuga nzima. Yaani ni kama lightouse, taa imewekwa kilingeni kabisa kuongoza watu usiku.

Ujenzi huo ni kinyume kabisa cha sheria za hifadhi na sheria ya mazingira. Zoning pia inaonesha kuwa eneo lenyewe ni tengefu kwa ajili mazalia ya wanyamapori hasa Faru, Simba, Chui n.k. Kwenye hili watalii wanakerwa sana!

Halafu bado kuna zile changamoto za Kambi za kuhama hama kurundikwa sehemu moja hasa kule Kogatende na Ndutu! Na hivi utalii unavorudi kwa kasi, tusipokuwa makini tutajiharibia wenyewe.

Ajabu ni kwamba wanakazana kuandika "Serengeti shall Naver Die" Lakini kwa matamaa ya fedha wanazidi kuiua!

Tupaze sauti zetu haya masuala ya ujenzi holela yakome. Ifike mahali wenye mamlaka wangetanguliza misingi ya taaluma zao na uzalendo wasitishe vituko kama hivi hifadhini.

View attachment 2667852
View attachment 2667849
View attachment 2667853
View attachment 2667851
Hoteli inajengwa kileleni mwa mlima. Yaani, juu ya mlima ni hoteli yenyewe (lounge/main areas)... Rooms za wageni zimesambaa juu ya mwinuko kuelekea upande wa ziwani (Lake Magadi).

Hiyo sehemu na majengo yanayoonekana chini ni yalipo makazi ya staff.

View attachment 2667848

Kwa ujumla maeneo husika ni mazalia ya wanyamapori hasa chui. Na ni maeneo maarufu sana kwa migration ya wanyama upande wa central Serengeti kabla hawajaelekea Moru na Southern Corridors.

SHERIA ZIPI ZINAHUSIKA?

1. Sheria ya Mazingira (EMA #20 ya mwaka 2004, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2018) - anzia kuasoma Sehemu VI ibara ya 81-85, 89-90, 92-97, 161, 184, 193, 198 n.k

2. NEMC EIA na Audit Regulations 2005 na 2018.

3. Tourism Investment Manual pia

NB:
1. Wachunguzi wa mambo wanahisi janja janja nyingi ndani ya SENAPA yametokea baada ya GMP kuisha muda wake.

2. Kuna usiri mkubwa unaotia mashaka kwenye mchakato wa EIA, ukizingatia unyeti wa eneo la Lake Magadi.

3. Kwa unyeti wa eneo husika la mradi haiwezekani na ni very unprofessional kwa EIA kuanza na kukamilika ndani ya mwaka mmoja (kwa mujibu wa maelezo yanayoibua mashaka ya msemaji wa TANAPA HQ). Wataalamu wanajua kuwa EIA huchukua muda mrefu kiasi (field - rejea NEMC audit regulations 2005).

4. Ili kulinda maslahi ya wawekezaji wengine ndani ya hifadhi - TANAPA'S TOURISM INVESTMENT MANUAL inaelekeza minimum distance ya 10kilometers kutoka accommodation facility moja hadi nyingine. Well-worth Collection's Lake Magadi Lodge pamoja na kupachikwa juu ya kilima na taa zake kusumbua wageni kwenye lodges za jirani ujenzi wake haukuzingatia umbali elekezeki!

REJEA:

TANZANIA ENVIRONMENTAL MANAGEMENT ACT, 2004

TANZANIA ENVIRONMENTAL IMPACT ASSESSMENT AND AUDIT REGULATIONS, 2005

TANZANIA NATIONAL PARKS ACT

Serengeti National Park Rules | Tanzania

General Management Plan (2006-2016), Serengeti National Park, Tanzania

Ieleweke kuwa, Watalii mbalimbali, Wawekezaji, Wafanyakazi (hata wa TANAPA wenyewe) na waongoza utalii (tour guides) wenye uzoefu wa muda mrefu kuhusu utalii na uhifadhi hawaridhishwi na uwekezaji wa Wellworth Collection ndani ya SENAPA!
Nani miliki wa hiyo Wellworth
 
Nani miliki wa hiyo Wellworth
Mmiliki wa Wellworth ni yule yule Bw. Gullam mmiliki wa Kunduchi Beach & Resort ambaye pia ni mmiliki wa Oleserai tented camps.
Kimsingi jamaa ni waaribifu sana wa mazingira ya asili! kuna vitu wanaendelea kufanya ndani ya hifadhi zetu ni vya aibu na muda si mrefu vitashusha sifa nzuri ya hifadhi zetu!
Hivi kuna nini TANAPA mbona wanapoteza misingi ya uhifadhi kwa kasi sana!?
 
Knowledge gap ni hatari sana!
Ni kweli... Upo sahihi kabisa!
Kimantiki idadi ya watalii wanaoingia Tanzania na kufika Kariakoo Dar ni kubwa sana, sema hatujui kipi ni kipi!
Upo sahihi kabisa! Watalii kwa maana ya utalii ni wale wanotoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa sababu mbalimbali... Itapendeza kama hao wanaofika Kariakoo na miji mingine wakiwekewa taratibu za kuchukua takwimu zao na mchango wao kwenye uchumi na maendeleo ya nchi!

NB: Kwenye hii mada tunajadili juhudi za uhifadhi na biashara ya utalii ndani ya hifadhi hizo! Tukumbuke kuwa hifadhi za taifa zipo kisheria kwa ajili ya kuhifadhi wanyamapori kwa ajili ya vizazi vya sasa na vile vijavyo.
Sasa linapotokea watu wanahoji maswali ni kutokana na zoezi la ujenzi wa miundombinu na mahoteli ndani ya hifadhi kitu ambacho ni kinyume cha sheria!

Hivi nani aliruhusu ujenzi juu ya mlima pale Lake Magadi?
 
Back
Top Bottom