Upo sahihi kabisa! Watalii kwa maana ya utalii ni wale wanotoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa sababu mbalimbali... Itapendeza kama hao wanaofika Kariakoo na miji mingine wakiwekewa taratibu za kuchukua takwimu zao na mchango wao kwenye uchumi na maendeleo ya nchi!
NB: Kwenye hii mada tunajadili juhudi za uhifadhi na biashara ya utalii ndani ya hifadhi hizo! Tukumbuke kuwa hifadhi za taifa zipo kisheria kwa ajili ya kuhifadhi wanyamapori kwa ajili ya vizazi vya sasa na vile vijavyo.
Sasa linapotokea watu wanahoji maswali ni kutokana na zoezi la ujenzi wa miundombinu na mahoteli ndani ya hifadhi kitu ambacho ni kinyume cha sheria!
Hivi nani aliruhusu ujenzi juu ya mlima pale Lake Magadi?