Ujenzi Nyumba za Makatibu UWT Mkoa wa Mara Wapamba Moto

Ujenzi Nyumba za Makatibu UWT Mkoa wa Mara Wapamba Moto

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE AGENS MARWA ACHANGIA UJENZI NYUMBA YA KATIBU UWT MKOA WA MARA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Mhe. Agnes Marwa amekabidhi mifuko 10 ya Saruji katika ujenzi wa nyumba ya Katibu wa UWT Mkoa wa Mara ikiwa ni sehemu ya matofali 1000 pamoja na laki tano (500,000) zilizotumika kununua Saruji Mifuko 25 hivyo kufikisha Mifuko 35 ya Saruji na Lori moja la mchanga ikiwa ni mchango wake hadi sasa katika ujenzi huo.

"Nilitoa laki tano ilikuwa nimifuko ya Saruji 25 na matofari 1000 pamoja na Trip 1 ya Mchanga na Leo nimechangia mifuko 10 hii nimchango ambayo binafsi nimetoa katika kuunga Mkono katika ujenzi wa Nyumba ya katibu wetu wa UWT mkoa wa Mara" - Mhe. Agness Marwa Mbunge wa Viti Maalum Mara.

Aidha, Wananchama 33 kutoka CHADEMA, CUF na NCCR wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mkutano wa Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mara Agness Marwa uliofanyika Manispaa ya Musoma katika Kata ya Mwigobero huku wakidai kufanya hivyo nikumuunga mkono Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utendaji kazi wake.
 

Attachments

  • F5-goCiWoAAr1a5.jpg
    F5-goCiWoAAr1a5.jpg
    129.3 KB · Views: 1
  • F2mRy4oXkAEZ1L-.jpg
    F2mRy4oXkAEZ1L-.jpg
    89.2 KB · Views: 1
  • F2mRzWuWQAAonJR.jpg
    F2mRzWuWQAAonJR.jpg
    78.9 KB · Views: 2
  • F57fWHpXEAAnzEH.jpg
    F57fWHpXEAAnzEH.jpg
    125.3 KB · Views: 1
Ajibane kwenye viti maalum hukohuko,2025 ni kimbembe,upinzani wengi watachukua majimbo.
 
Back
Top Bottom