KERO Ujenzi wa barabara ya Safina Olasiti hadi Morombo-Arusha

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Naipongeza Serikali kwa ujenzi wa barabara hii. Changamoto iliyopo ni kuwa Mkandarasi anayejenga barabara ya Safina Olasiti hadi Morombo hajaweka alama ambazo zinawataka/kuelekeza watumiaji wa barabara kutumia njia mbadala.

Hili linasabisha usumbufu kwa watumiaji wa barabara/njia hizo.

Pia barabara/njia ambazo watumiaji wanalazimika kutumia zimeharibika hasa kipindi hiki cha mvua.

Tunaomba Mkandarasi aelekezwe kuweka vibao elekezi na kurekebishwa barabara/njia mbadala ili kuepuka usumbufu kwa wananchi.

Mkazi wa Olasiti Arusha.
 
Mbona barabara nzuri tu hiyo mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…