Ujenzi wa Gabion, nyumba kwa milioni 2 tu!

goodfool

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2016
Posts
1,668
Reaction score
994
Hamjambo wakuu,

Moja kwa moja kwenye mada,

Wakati nikisubiri zile milioni 3 zangu zijae ili nijenge, nimepata wazo jingine la ujenzi rahisi kabisa.

Ujenzi huu unahusisha mawe na mesh (nyavu), nimeona ni less cost kwa kuwa simenti haihitajiki sana na unaokoa muda

""""" kumbuka nia yangu ni kufanikisha kujenga kwa gharama nafuu zaidi na makazi yenye hadhi, kwa gharama ileile"""""

Nawashukuru watu wachache wa hapa JF walioyeyuka mioyo na kuonyesha nia ya kunisaidia kimawazo hata kitaaluma kabisa, huko PM wapo wengi tu.

Katika ujenzi huu nitapaua kwa zege nyumba ya vyumba viwili tu na kisiitingi rumu.


Hapa napunguza gharama za:-

Mbao,
Ceilings
Bati
Misumari

Katika zoezi hili nitatumia wire mesh za bei nafuu kabisa na nondo chache.

Kwanini tusimiliki nyumba???

Nawasilisha.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio itategemea na Mtu alipo, kama unapoishi hakuna mawe around, si usafiri utakugharimu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…