The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Wananchi wa Kata ya Nkinga, katika Tarafa ya Simbo, wilayani Igunga, mkoani Tabora, ambao awali walikuwa hawana uhakika wa Kituo cha Polisi na kulazimika kupeleka malalamiko ya uhalifu umbali wa zaidi ya kilomita 80 wilayani Igunga, adha hiyo imeisha baada ya kituo kipya cha polisi kilicho jengwa kwa zaidi ya shilingi milioni 81 kuzinduliwa na kuondoa tatizo hilo. Baadhi ya wananchi wakiwa na furaha wanasema sasa wanauhakika na usalama baada ya kupata kituo hicho cha polisi.