Ujenzi wa Reli ya SGR uishie Tabora

Ujenzi wa Reli ya SGR uishie Tabora

Mradi wa sgr umetutia madeni. Halafu mradi ukikamilika utatutia madeni zaidi. Pia ramani ya mradi imekosewa. Reli ya sgr inatakiwa iende sehemu ya mizigo mingi. Na mizigo mingi ni shaba ya Zambia, na madini ya cobalt na shaba yaliyopo Lubumbashi/kolwezi/katanga DR Congo.

Sasa hii reli naona imepotea uelekeo wa mizigo mingi mno kwa hiyo haitarudisha hela. Kwa hiyo ni madeni juu ya madeni halafu riba. Mizigo mingi ipo kusini kwa Congo na Zambia. Halafu reli inaelekea mashariki mwa Congo

Hao Rwanda na Burundi hawana mzigo wa maana kuzidi Zambia na Cobalt na Copper ya Drc congo. Ilitakiwa SGR iende kwenye mizigo ya maana huko kwenye migodi ya zambia na Congo.

Hii sgr inayojengwa imekosewa kabisa. SGR ilitakiwa iwe Dar-Kapirimposhi-Lubumbashi(ikiwezekana ipite kwenye migodi ya Copper na Cobalt iliyopo Kolwezi, Mutanda huko Drc ndanindani)
Respect mkuu naona umeichambua copper belt sawa sawa, ukweli huu ukanda ni wenye kipato cha uhakika ukilinganisha na njia ya kati... lakini tukifanya hivi malori yetu yataendelea kupata mizigo???
 
Hahaha wanaoendesha nchi ni wakulima, wachimba madini, viwanda, wafugaji, wavuvi hao ndio wanaofanya tunapata chochote cha kuuza nje ya nchi na hatimae tunapata mishahara ya kuwalipa hao unaosema ndio wanaendesha nchi, kiuchumi hao uliowataja ni liabilities kwa serikali (most of them) anyway elimu ndogo 🚮🚮🚮
Kwa vile unajuwa kuandika neno Liabilities ndiyo unajiona msomi!! Ila tambua bado hujui kitu
 
Back
Top Bottom