Ujerumani kuiwekea vikwazo Urusi kutokana na tuhuma za kudukua Bunge lake

Ujerumani kuiwekea vikwazo Urusi kutokana na tuhuma za kudukua Bunge lake

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Wizara ya Mambo ya kigeni ya Ujerumani leo imemwita balozi wa Urusi kujadili uwezekano wa kuiwekea Moscow vikwazo kufuatia madai ya udukuzi ya mwaka 2015 dhidi ya bunge la Ujerumani, Bundestag.

Taarifa ya wizara hiyo imesema balozi wa Urusi amearifiwa kuwaUjerumani inalenga kuuomba Umoja wa Ulaya kuiwekea vikwazo Urusi pamoja na raia wa nchi hiyo Dmitry Badin anayeshukiwa kuongoza udukuzi huo.

Mapema mwezi huu Kansela Angela Merkel aliliambia bunge kuwa ana ushahidi wa Urusi kumlenga mara kadhaa kwenye mashambulizi ya udukuzi na kuongeza uwezekano wa kuiwekea vikwazo nchi hiyo.

Inaaminika kati ya mwaka 2012 na 2015 wadukuzi wa mtandaoni walifanikiwa kukusanya data za wabunge kadhaa wa Ujerumani pamoja na kupakua baruapepe mbili kutoka akaunti ya Kansela Merkel.
 
NI aibu kubwa kwa taifa Kama Ujerumani kulialia eti wamedukuliwa! Ina maana hawana counter measures hapo papo hapo? Russia wanadukuliwa Sana sema ni wajanja hawaliilii unajua kwa Nini wanajua wao ni maadui namba moja wa West. Mwaka 2013( Snowden) if IAM not mistaken , katika taarifa iliyoonyeshA marekani kuwadukua washirika wake wa ulaya na wengine , Putin alijibi hivi angeshangaa Sana Kama Urusi isingekuwepo katika wadukuliwa
 
MARA TUNASIKIA KANSELA WAO ALIKUWA AKIDUKULIWA NA WAMAREKANI KTK MAWASILIANO YAKE YA SIMU! MARA SASA TUNASIKIA DATA ZAO ZILIDUKULIWA NA WARUSI!!

WANGETOA VIBALI KWA MA-iT WETU KUWAWEKEA HARDWARE & SOFTWARE FIRE WALLS KULINDA SAVERS ZAO. MAANA NAONA KAMA WAMEZIDIWA MAARIFA NA WAZUNGU WENZAO!!
 
MARA TUNASIKIA KANSELA WAO ALIKUWA AKIDUKULIWA NA WAMAREKANI KTK MAWASILIANO YAKE YA SIMU! MARA SASA TUNASIKIA DATA ZAO ZILIDUKULIWA NA WARUSI!!

WANGETOA VIBALI KWA MA-iT WETU KUWAWEKEA HARDWARE & SOFTWARE FIRE WALLS KULINDA SAVERS ZAO. MAANA NAONA KAMA WAMEZIDIWA MAARIFA NA WAZUNGU WENZAO!!
Na wewe ni mdukuzi?
 
CIA wanakwambia, what happens in Pakstan always has 8 versions of the story....
 
Back
Top Bottom