Ujerumani: Marekani kutengana na WHO kutaathiri Afya ya Dunia

Ujerumani: Marekani kutengana na WHO kutaathiri Afya ya Dunia

mkiluvya

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2019
Posts
809
Reaction score
729
Ujerumani imekasirishwa na uamuzi wa rais wa Marekani Donald Trump wa kukata mahusiano na shirika la afya ulimwenguni WHO ikiielezea hatua hiyo kuwa na muvunja moyo na inayorudisha nyuma afya ya dunia.

"WHO inahitaji kufanyiwa mageuzi kama linataka kuleta maadiliko yoyote" aliandika Waziri wa afya wa Ujerumani Jens Spahn katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter, huku akisema Umoja wa Ulaya unapaswa kuchukuwa jukumu kubwa la kulisaidia shirika hilo kifedha na kusema hilo, ndilo litakuwa moja ya vipaumbele vya Ujerumani wakati itakapochukua urais wa kupokezana wa umoja huo Julai Mosi mwaka huu.

Hapo jana Trump alisema anakata mahusiano ya Marekani na WHO anayoishutumu kwa kushindwa kuwajibika zaidi kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona.

1590850817345.png
 
WHO walitakiwa kushtakiwa
Kushtakiwa kwa nini?
Trump is a dying horse. Anatafuta a scapegoat kwa failures za serikali yake.
COVID 19 ni ugonjwa mpya. Kila siku nikujifunza.
Kwa ufahamisho WHO si WAO ni SISI wote, so tunastahili kushtakiwa pia kwani tuna mchango pale kama nchi.
Sasa Trump na uwezo wa mfumo wa serikali yake alileta siasa badala ya kufanyia kazi ushauri aliopewa kuanzia December.
Kidogo kidogo chini ya Trump marekani inajivua ushawishi wake wa miaka yote na ndiyo maana EU wanakuja.
 
Kushtakiwa kwa nini?
Trump is a dying horse. Anatafuta a scapegoat kwa failures za serikali yake.
COVID 19 ni ugonjwa mpya. Kila siku nikujifunza.
Kwa ufahamisho WHO si WAO ni SISI wote, so tunastahili kushtakiwa pia kwani tuna mchango pale kama nchi.
Sasa Trump na uwezo wa mfumo wa serikali yake alileta siasa badala ya kufanyia kazi ushauri aliopewa kuanzia December.
Kidogo kidogo chini ya Trump marekani inajivua ushawishi wake wa miaka yote na ndiyo maana EU wanakuja.
facts tupuuuu.....


Ila ukweli mchungu kama huu hua unawaumiza wengi sana kiukweli hasa wale wamarekani weusi.....
 
Ni mwehu tu asiyeliona hilo. Ukiona mtu anapuuza hili basi aidha ni Zuzu au Msukule.
 
Toeni hela zenu. Marekani kasema hapana
 
Ujerumani ni bonge la taifa, alichoandika
Waziri wa afya wa Ujerumani Jens Spahn katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter ameonyesha mtazamo chanya. Sio tu kwa taifa lao na umoja wa Ulaya bali pia kwa Dunia nzima.
Waziri Ummy Mwalimu unafeli wapi kwa jambo hili tena critical linalohusu afya?
Heshima kwako waziri wa Ujerumani.
 
Toeni hela zenu. Marekani kasema hapana
waambie wajitoe na UN kabisa [emoji2][emoji23] natamani sikumoja wajitoe nakwenye Shirika lao wanaloliita lahaki zabina adamu maana kule kuna maovu namachafu teleee...
 
Amerika iniihitaji zaidi WHO kuliko wengine. Hii ni kujishabadua tu.
Hili gonjwa mbona ndiyo linapurura wamarekani zaidi kuliko wengine duniani. Trump angekuwa mkweli si ajitoe kote aone kama atasurvive. mashirika yote ya UN marekani inaushawishi mkubwa kwa interest zake zaidi. Hili la WHO ni kujitoa aibu kwa failure ya MAGA ya Trump.
 
Ujerumani ni bonge la taifa, alichoandika
Waziri wa afya wa Ujerumani Jens Spahn katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter ameonyesha mtazamo chanya. Sio tu kwa taifa lao na umoja wa Ulaya bali pia kwa Dunia nzima.
Waziri Ummy Mwalimu unafeli wapi kwa jambo hili tena critical linalohusu afya?
Heshima kwako waziri wa Ujerumani.
ameandikaje?
 
Tafuteni pakutoa hela za kuendesha hilo shirika
waambie wajitoe na UN kabisa [emoji2][emoji23] natamani sikumoja wajitoe nakwenye Shirika lao wanaloliita lahaki zabina adamu maana kule kuna maovu namachafu teleee...
 
Tafuteni pakutoa hela za kuendesha hilo shirika
Yeye kashajitoa aache watu waendelee namaisha yao
Kwanza alikua anajifanya yeye ndio kilakitu sasa tuone baada yakujitoa kama maisha hayatasonga

Tuatayapitia magumu sana ila tutayazoea hakuna namna ss

Ajitoe na UN[emoji14]
 
Back
Top Bottom