Ujerumani yaipigia magoti Canada irejeshe injini (ipo kwenye vikwazo) ya mitambo ya gesi ya Urusi Ujerumani, ili kuiokoa Ujerumani na uhaba wa gesi

Ujerumani yaipigia magoti Canada irejeshe injini (ipo kwenye vikwazo) ya mitambo ya gesi ya Urusi Ujerumani, ili kuiokoa Ujerumani na uhaba wa gesi

Sikirimimimasikini

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
2,926
Reaction score
15,634
EU+NATO washindwa tena ktk kutekeleza vikwazo walivyokubaliana na kuviweka wao wenyewe juu ya kuminya matumizi ya gesi ya Urusi ili kuipunguzia Urusi pesa ipatazo toka kwenye biashara hiyo.

Mabeberu waliweka vikwazo ktk vipuri vya miundombinu ya gesi. Ujerumani ilipeleka injini fulani Canada ikafanyiwe matengenezo. Injini hiyo inahusika na mitambo ya gesi ya Urusi kwenye miundombinu iliyopo Ujerumani. Injini ikazuiwa Canada kwa kuwa ipo kwenye list ya vifaa vinavyofanyiwa vikwazo.

Urusi haikusema neno. Yenyewe ikafanya vitendo tu. Ikapunguza gesi iliyokuwa ikiipeleka Ujerumani kwa asilimia 60, yaani ikawa inapeleka gesi ailimia 40 tu. Ujerumani wamechezea mkong'oto mkali ambao umeathiri sekta mbalimbali ikiwemo viwanda na uchumi. Ujerumani yenyewe sasa ndio ikapiga magoti kwa Canada kuwa jamani tunaomba hiyo injini irejeshwe nchini Ujerumani ili tupate gesi kwa asilimia zote (100%), hali ni tete sisi Wajerumani ndio twateseka, na sio Putin...Uchumi waanguka na isitoshe winter yaja.

Wakati Ujerumani yalalamika hivyo, Zelensky anaiambia Canada isiachie injini ile, kwa maneno mengine Zelensky anafurahia Wajerumani kuendelea kuteseka kwa faida yake yeye Zelensky na Ukraine. Mwisho wa siku Zelensky kapuuzwa na injini inarejeshwa Ujerumani.
=======

SmartSelect_20220707-152525_Chrome.jpg

SmartSelect_20220710-070519_Chrome.jpg
 
Ukute so ajabu USA ndio anashawishi Canada asiirudishe ili ulaya I we tegemezi kwake
Ndilo lengo lao hasa, bahati mbaya sijui kama Ujerumani inafahamu kwamba USA inaipaga vita ya kiuchumi kwa kificho/kichini chini - Ujerumani ndio yenye Uchumi mkubwa na viwanda vigi barani Ulaya, hivyo USA inatumia kila mbinu kuhujumu uchumi wa Ulaya pamoja na viwanda ili bara la Ulaya liwe tegemezi kwa Merikani kwa nyanja zote - Ufaransa iliwahi kufanyiwa mchezo mbaya na Merikani, sasa sijui kwa nini Viongozi wa Ulaya hawajifunzi kitu, wanaendeshwa puta na Uncle SAM kama makoloni yake-mtu uwezi kuamini kama Nchi za Ulaya ni huru Kwelli!!
 
Ndilo lengo lao hasa,bahati mbaya sijui kama Ujerumani inafahamu kwamba USA inaipaga vita ya kiuchumi kwa kificho/kichini chini - Ujerumani ndio yenye Uchumi mkubwa na viwanda vigi barani Ulaya, hivyo USA inatumia kila mbinu kuhujumu uchumi wa Ulaya pamoja na viwanda ili bara la Ulaya liwe tegemezi kwa Merikani kwa nyanja zote - Ufaransa iliwahi kufanyiwa mchezo mbaya na Merikani, sasa sijui kwa nini Viongozi wa Ulaya hawajifunzi kitu, wanaendeshwa puta na Uncle SAM kama makoloni yake-mtu uwezi kuamini kama Nchi za Ulaya ni huru Kwelli!!
Us alimshawishi mfaransa asimuuziwe manowari ya kijeshi mrusi wakati Urusi ameshailipia kisa Urusi kavamia Cremea lakini baadae US akanzunguka mfaransa kwenye dili la kutengeneza manowari ambayo mfaransa alishapata go ahead kwa nchi nyingine
 
Kwa wanaoamini ushirikina wanaweza sema Ulaya magharibi wamelogwa na USA maana si kwa uzwazwa huu.
Kisiasa wana cha kujifunza kwa Waafrika, hatuchelewi kuamia upande wa pili ili tunufaike huku USA wakisema hali hyo kwao kwamba, they dont have permanent enemy or friend just permanent goal.
 
Back
Top Bottom